Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

...Slaa hawezi kugombea Ubunge Arumeru...kwanza yeye slaa ana malengo makubwa sana katika siasa mojawapo ni kufanya kazi za chama ili chama kiendelee kukua na hatimaye kushika dola...pili dk. slaa ana ndoto za kuwa mr. president wa nchi hii...hivyo kurudi bungeni na kuenda kubishana na akina Anna kilango malekela wanaotumia hisia zaidi katika kuelezea mambo badala ya hoja ni natari sana kwake maana atajichafua tu....huyu mama mara nyingi huwa analia kuhakikisha tu kuwa naonyesha hisia badala ya nguvu ya hoja
 
Jamani ubunge anaweza simama popote..Mrema alisimama Temeke na kazi waliiona magamba..So Arusha ipo ok sana kwa Slaa. Ila wana Arumeru wanajua thamani ya Slaa kwa Jimbo lao??
Ila aliyekuwa amesimama mwaka jana ni Chachu ya kutosha..Jimbo hilo Chadema wanalo..CCM kwishiney
 
Slaa abaki kukijenga Chama ili 2015 tuhitimishe kazi. Nasaari bado anafaa kuiwakilisha CDM
 
Wapendwa wa Chadema,
Mimi naomba Dr Slaa awanie ubunge Arumeru kusudi arudi Bungeni kuweka nguvu mpya

Tunashukuru kwa wazo lako, lakini nisingependa agombee ubunge kwa sasa. Sisi tunamwitaji kwa mambo mengi ya kuimarisha chama na kama majembe CDM wanayo na ndio maana huko bungeni CCM wanahaha. Je tukiwatumia tena hili jembe CCM si watachanikiwa? Tuwaache CCM wakabidhi nchi kwa amani.
 
Sio vibaya Slaa, akigombea ubunge Arumeru, mbona Mbowe nae aligombea urais akashindwa vibaya hakaamua kujisalimisha kwenye ubunge.

Kama Slaa, anawaza kuwa Rais wa Tanzania ni kujidanganya najua Pro-Chadema JF mtachukia mie kusema haya maneno lakini huo ndio ukweli, bora ajitose Arumeru.

Hapo kwa red; Hicho ni kiswahili cha watoto wa wala madafu au ndo lugha mama yenyewe ya wala madafu?
 
Binafsi napendekeza CHADEMA imsimamishe Dr.SLAA kwenye kinyang'anyiro cha ubunge huko Arumeru. Hii itaipa chadema kwanza nafasi kubwa ya kukinyakua kiti hicho kwa kuwa Slaa kwa sasa ni heavy weight politician na pia watanzania wenye uchungu na nchi hii tumekuwa tukiukosa mchango wa Dr pale bungeni.

Wengi tunaukumbuka ujasiri wake akiwa anga zile, kiukweli Mboe anapwaya kwenye nafasi ya kiongozi wa upinzani pale bungeni,waziri mkuu Pinda na serikali yake wanahitaji kuchangamshwa na mtu machachari wa aina ya Slaa,Lema au Tundu!....

Mboe amekua na huruma huruma hivi,sasa slaa kama atafanikiwa kushinda ubunge(nina uhakika atashinda)basi mh.mboe awe muungwana kwa kumpisha bwana Slaa kiti cha kiongozi wa upinzani!hii imekaaje wadau,yote ni katika kuimarisha makali ya bunge.

Mkuu, ni haki yako kutoa pendekezo kama hilo hapo juu.
Lakini binafsi sikuungi mkono.
Kwa wakati huu ambao nchi inayumba CDM inatakiwa kupigana ndani na nje. Ndani kwa maana ya bungeni na nje kwa maana katika jamii.
Walioko bungeni wanapigana vyema chini ya uongozi shupavu wa Mhe. Mbowe. na walioko nje ambao kwa asilimia kubwa ni BAVICHA nao pia kwa busara za Mhe. Slaa wanafanya kazi nzuri sana.

Kwa hiyo, kumuondoa Mhe. Slaa na kumpeleka bungeni kutafanya vita vya nje kupwaya.
Wacha dr. aendelee huku aliko aweze kupata nafasi zaidi ya kuimarisha CDM.
 
Mwacheni rais wetu........asigombee ubunge.......atajidhalilisha..............tunajiandaa kwa ajili ya kukabidhiwa ikulu 2015 kwani baadae kikwete atajiunga cdm
 
Dr silaa anamchango mkubwa sana ktk kukifanya chadema kiwe kama kilivyo leo na hayo yote yalianzia bungeni(kwenye issue ya mafisadi) karibu watz wengi sana walimfahamu kupitia bunge nashauri kwa maslahi ya chama agombee ubunge Arumeru bila kujali kama atashinda au la!hii itasaidia chadema kuhit sana maskio ya watanzania wengi yatakuwa kwa chadema hata asiposhinda chama kitajizolea umaarufu na wanachama kibao kama waliowapata igunga,akiwa nje ya bunge hasikiki sana kama alivyokuwa bungeni na watanzania wengi wangependa kumsikia na kuona zaidi anayofanya,tofauti na sasa anafanya mengi na anaonekana mara chache,agombee na aendelee na ukatibu mbona mbowe ni mbunge na ni mwenyekiti,
 
Jamani jambo usilo lijua ni kama usiku wa giza.Kwa taarifa yenu uchaguzi wa Arumeru mashariki ni tofauti sana na chaguzi zingine unazozihafamu.Binafsi nampenda Dr Slaa,ila kwa Arumeru hata kama mpinzani wake ni jiwe atamshinda.Hizo ndio siasa za Meru.Hivi sasa Dr Silaa atakuwa anatokea Koo gani kule Meru????
Ana lipi common na wananchi wa Meru? As far as I am concerned lile jimbo ni la mtu wa nyumbani(Meru),aliyezaliwa pale,anayepajua pale na mwenye nia ya kushirikiana na watu wale
 
Hiyo level alikwisha ivuka, yeye ni mgombea Urais, na hata hakipokonywa basi atabaki kuwa hazina ya Chadema kwa kutoa ushauri na kujenga chama!

mzee kwani slaa ndio mtu wa kwanza kugombea urais hapa nchini?mbona mrema ambae aliitikisa serikali ya ccm na kukaribia kuwa rais leo mbunge na anatoa mchango wake kwa taifa,mbona cheyo pia yuko bungeni,mbona chairman mboe licha kugombea urais huko nyuma leo tunapata mchango wake kama mbunge?kwani mnataka kusema slaa alizaliwa kuwa mgombea urais tu au?kumbukeni nafasi ya urais ni moja tu hivyo kama mwanasiasa ni lazima uwe flexible kutizama chances nyingine za kulitumikia taifa lako,kuna mtu kasema huko nyuma eti jamaa ni presidential material!sijui alikua na maana gani..
 
wala usihangaike mkuu, DR. ni mtu makini sana na ndiyo maana anawanyima usingizi kila kukicha wanajaribu kutafuta jambo kumwondolea umaarufu ila cha ajabu ndiyo wanamwongezea tu; mambo haya anapanga mwenyezi wacha wahangaike. Kinachowauma zaidi Dr anapendwa na wananchi zaidi ya 80% kote nchini sasa hilo ndiyo linawachanganya kabisaa -- nafikiri cha msingi ni kuanza kutafuta mtu wa kuchapisha zile karatasi za kura - sasa hvi zitoke china. :lol:
Hivi kumbe dr slaa ni mgombea urais wa "kudumu" wa chama kinachojinasibu kwamba ni cha kidemokrasia?demokrasia iko wapi sasa hapo..
 
Joshua nassari anaweza kwanza walichachukua kura zake siungi mkono hoja ya silaa kugombea jimbo la meru labda amsaidie kampeni tu Nassari anaweza hana tofauti na mnyika huyu ni kamanda
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amewekwa njia panda kutokana na matakwa ya wafuasi na mashabiki wa chama hicho kumtaka agombee ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki, unaotarajiwa kufanyika Aprili mosi mwaka huu.

Hata hivyo, wakati shinikizo hilo likiwa hivyo, umeibuka mgongano wa mawazo miongoni mwa wanachama, wasomi na wadau kutokana na baadhi yao kupinga shinikizo hilo, wakidai kuwa kazi aliyonayo Dk. Slaa kwa sasa ya kukiimarisha chama akiwa nje ya Bunge ni kubwa na muhimu sana kuliko ubunge.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima kwa kufuatilia mijadala ya makundi hayo katika mitandao ya kijamii, umebaini kuwa wengi wanamtaka Dk. Slaa awanie kiti hicho, kwa matumaini kuwa CHADEMA watakinyakua kirahisi kutokana na umaarufu wake.

Katika maoni yao, wafuasi wa CHADEMA na wadau wengi walikwenda mbali zaidi wakisema kwamba kwa umaarufu aliojijengea Dk. Slaa tangu akiwa mbunge wa Karatu kwa vipindi vitatu na baadaye kugombea urais mwaka 2010 na kuteka nyoyo za wananchi, anaweza kugombea jimbo lolote nchini na kuibuka mshindi.

Walisema kuwa jambo hilo halitakuwa la kushangaza kwani linatokana na umaarufu wa kukubalika mahali popote nchini, huku wakitoa mfano wa Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema, ambaye aligombea ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Temeke jijini Dar es Salaam mwaka 1996 na kuigaragaza CCM wakati huo akiwa NCCR-Mageuzi.

Hata hivyo uamuzi wa Dk. Slaa kushinikizwa agombee ubunge katika jimbo hilo umepingwa vikali na baadhi ya wasomi na wadau, wakidai huo ni mkakati unaochochewa na Chama cha Mapinduzi (CCM) ili kuhakikisha anarejea bungeni ambako atakuwa ametingwa zaidi na majukumu ya kibunge badala ya kukiimarisha chama.


"Unajua Dk. Slaa kama angekuwa ni mtu wa kutaka madaraka, tayari CCM wangekuwa wamekwisha kumshawishi Rais Jakaya Kikwete amteu mbunge katika vile viti vyake 10 ili arudi bungeni na kuacha kuwasumbua kama anavyofanya sasa. Akiwa mbunge hawezi kuzunguka kila sehemu kuimarisha CHADEMA kama sasa," alisema kigogo mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.


Dk. Slaa ambaye alishika nafasi ya pili katika kinyang'anyiro cha urais mwaka 2010 nyuma ya Kikwete, amejizolea uungwaji mkono miongoni mwa makundi hasa vijana, hatua iliyokifanya CHADEMA kunyakua majimbo mengi na viti vya udiwani kwenye uchaguzi huo.

Tayari mchakato wa kusaka wagombea katika jimbo hilo lililoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wake, Jeremiah Sumari (CCM), unaendelea ndani ya vyama kwa kutoa fomu kwa ajili ya kujiandaa na kampeni zitakazoanza Machi 9 hadi 29 mwaka huu.

Ushindani mkubwa unatarajiwa kuwa baina ya vyama vya CCM na CHADEMA, ambapo mtoto mkubwa wa marehemu Sumari, Sioi Sumari, amekuwa miongoni mwa wanachama wa kwanza wa CCM walioomba kuteuliwa kuwania nafasi hiyo, huku kada kijana aliyegombea kiti hicho mwaka 2010 kupitia CHADEMA, Joshua Nasari, akiwa ameomba kuteuliwa tena na chama chake.


"Dk. Slaa majukumu aliyonayo kwa sasa ni zaidi ya kuwa mbunge, kasi ya uwajibikaji na umahiri wa wabunge wa CHADEMA unayoiona ni kutokana na kazi nzuri ya kuwapika wabunge hao inayofanywa na yeye, kuna kazi kubwa zaidi ya hiyo?" alihoji mdau mmoja katika mtandao wa kijamii akiwapinga wanaokataa katibu mkuu huyo asigombee ubunge.


Maoni hayo yalipingwa na mchangiaji mwingine, akisema kama sheria inamruhusu Dk. Slaa, anaweza kugombea lakini ni bora awaachie vijana, awape mafunzo wawe tishio kama yeye.


"Mwacheni Dk. Slaa afanye kazi ya kuimarisha chama kwa mipango ya baadaye, tena azidi kuwapika wabunge vijana ili CHADEMA iwe na mvuto kwa sera zake. Maendeleo ya nchi hii yanahitaji mabadiliko makubwa, si bungeni peke yake, bali na kukijenga chama kujiandaa kwa uchaguzi ujao," alisema mchangiaji mwingine.


Mdau mwingie alisema kuwa mkakati wa kumtaka katibu huyo agombee, umeanzishwa na unashabikiwa na maadui wa CHADEMA, wakitaka aingie kwenye shindano la Arumeru ili wammalize kwa kutumia Tume ya Uchanguzi.


"Wanajua wakimmaliza Arumeru, hataweza kufurukuta tena mwaka 2015 kwenye urais au hata ubunge. Nadhani Dk. Slaa ajikite kwenye mambo ya Katiba Mpya zaidi. Kwa sasa, CHADEMA walio bungeni wanamwakilisha vya kutosha," alisema msomi mmoja.


Hata hivyo, Dk. Slaa alipotafutwa na gazeti hili aweze kuzungumzia juu ya hatua hiyo, alisema kwa kifupi: "Siwezi kulizungumzia jambo hilo, maana nilikwisha kusema muda mrefu kuwa sitaki tena ubunge na isitoshe mimi si mwenyeji wa Arumeru."


Alisisitiza kuwa kwa sasa ana kazi moja ya kukijenga chama chake cha CHADEMA ili kiweze kushika mizizi kwenye maeneo yote nchini.


Source:
Tanzania Daima
 
Wanaomshauri dr slaa agombee ubunge hawana nia njema ..zaidi ya kushiriki mkakati wa kumuuwa kisiasa kuelekea mwaka 2015 ambako tayari wanamuonaa ni tishio kubwa kwenye urais....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom