Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

Dr. Slaa ana akili sana! Kwa nini aende Arumeru? Kwani hakuna wanachama wa CHADEMA huko?Fanya kazi ya chama mzee, achana na mawazo ya namna hiyo. Fanya mikakati ya kijana Nassari kuchukua jimbo hilo.
 
'danganya toto kula indi bichi' teh teh, usikubali DR. wanajua wewe ni tishio urais 2015
 
Hata mimi nisingependa Dr Slaa aende kugombea tena ubunge Arumeru kwa sababu wajibu wa kukijenga chama ni mkubwa kuliko huo wa ubunge. Tunahitaji kuweka misingi imara na madhubuti kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao na bila mtu makini wa kusimamia misingi hiyo, lengo litakuwa vigumu kutimia.
 
Hataki tena ubunge..inamaana bado ana ndoto za urais?

hajasema hivo, amesema hataki tena ubunge, anachotaka kwa sasa ni kuimarisha CDM ili Tanzania ibadilike kupitia yeye kuimarisha chama ndani na nje ya bunge.

Ninachokiona kwenye uzi huo, ni kwa kiasi gani JF imekuwa chanzo cha habari. Mawazo ya REJAO SIJAYAONA
 
Ushauri wangu kwa Dr. Slaa asikubali, ataonyesha kuwa anauroho wa madaraka kama wenzake magamba na pia kama akishindwa atajishushia heshima yake ktk jamii ya kiTZ
 
Kamanda usidanganyike. Wanaokwambia ugombee ni magamba. Unafanya kazi ya nguvu kukiimarisha chama.
 
hajasema hivo, amesema hataki tena ubunge, anachotaka kwa sasa ni kuimarisha CDM ili Tanzania ibadilike kupitia yeye kuimarisha chama ndani na nje ya bunge.

Ninachokiona kwenye uzi huo, ni kwa kiasi gani JF imekuwa chanzo cha habari. Mawazo ya REJAO SIJAYAONA
Owk owk...ametumia akili na busara sana kufanya huo uamuzi. Kwa sasa Tanzania hatuitaji kuwa na viongozi wazee kama yeye. Tunataka vijana watakaoleta mabadiliko na mbinu mpya za kumkomboa mtanzania.
 
Kumbe hawa Tanzania Daima wanacopy huku JF halafu wanaenda kuuza gazeti lao...hapa inabidi haki miliki izingatiwe!!
 
Hili bila shaka ni wazo la ccm,wanataka kumpeleka njia waliyompitisha Mzee mrema.kwa mfano akishinda watafanya mbinu na kumfungulia kesi mahakamani na huko basi,kesi inacheleweshwa hadi karibu na uchaguzi mkuu 2015 halafu inaanza kusikilizwa mfululizo,wakiwa wamelikataa ombi lake la kusitisha na kumruhusu ahudhurie katika kampeni za urais.
Jambo amhalo litampotezea muda mwingi na kumdhoofisha kisiasa kwani anakuwa busy na utetezi mahakamani,kama tunavyoona sasa hivi kule arusha kwa mh Godbless lema.
Ambako wanafanya mchezo kama huo,na pale wanaweza chakachua hukumu ikawa ni pamoja na kumzuia kushiriki uchaguzi kwa kipindi fulani mathalani miaka mitano,na hapo lengo lao linakuwa limetimia,
Kumbukeni walijaribu mchezo huu kwa mh slaa katika uchaguzi uliopita kwa kumletea yule mume mtalakiwa wa mama mshumbuzi. Jaribio lililoshindwa lakini likamuathiri kwa kiasi fulani kisaikolojia na pia kitaswira kwa wapiga kura ambao hawakuujua mchezo ule ulivyokuwa.
Cha msingi mzee slaa atumie mvuto alionao kwa sasa kwa kutembelea matawi ya chama na kufanya uhamasishaji na uhai wa chama katika kila kona ya nchi,,badala ya kukaa na kuongelea kutoka dar es salaam tu.
Atumie nafasi hii huku akiwa anafanya utambulisho wa timu ya vijana wabunge wa sasa na hata wale wasiokuwa bungeni,manufaa ya hii inakuwa ni kuwapa nafasi kutambulika na kusikika katika sehemu zote nchini na itamfanya asilazimike kusafiri nchi nzima wakati wa kampeni.kwani anakuwa na kikosi cha kutosha kuifanya kazi hiyo,na yeye ana kwenda sehemu zile zenye kuhitaji nguvu za ziada ambazo ni kambi kongwe za ccm.

Kumbukeni anapambana kumn'goa baba mwenye nyumba na familia yake yote na wakwe,mashemeji,binamu,washenga,makuwadi wa ufisadi na kila aina ya watu waliojikita pale kutuangamiza watanzania kiuchumi.
 
Nampongeza Dr Slaa kwa msimamo wake, yeye si mpenda madaraka awaachie wananchi wa jimbo husika wamtafute mgombea anayejua matatizo yao.
Mungu akuzidishie hekima ili usonge mbele kutekeleza majukumu ya chama chako.
 
Katu Dr. Slaa usigombee Ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwani Joshua Nasari anatosha. Endelea kukiimarisha chama.
 
Akigombea itathibitisha dhana ile ile tunayoikataa kuwa hakuna watu wengine wa kuongoza. Moja ya mafanikio ya kiongozi ni kuweza kuandaa watu wengi zaidi kuchukua nafasi yake, hivyo ni bora kuandaa wakazi wa Arumeru kuchukua uongozi wao. Tusijenge mazoea kuwa fulani ndio anaweza. Ni mantiki inaowafanya baadhi ya viongozi wetu wawepo kwenye utawala tangu uhuru hadi leo. Kuna namna nyingi tu za kulitumikia taifa nje ya bunge
 
Kwanza Slaa kugombea Arumeru mashariki ni dharau kwa Wakazi wa Meru. Hili ni wazo mfilisi za watu wasiomtakia mema mzee wa watu.:embarassed2:
 
arumeru na karatu kuna ukaribu gani? Sishauri dk kufanya hivyo. Si lazima kuwa mbunge ndipo uwe na ushawishi. Tayari cdm ina vichwa vya kutosha kwa sasa. Tena ishu nyingine ya spika kuanza kumwambia dk, 'tafadhali mh kaa chini!' haipendezi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom