Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

Joshua anafaa na anaweza sana , tusitumie bomu kuua sisimizi jamani. ile ni nafasi ya kijana Nassary na tayari ameshajijenga sana kisiasa Meru

Niwaambie kitu?kile kiti mnakipoteza tena kwa huo ukaidi wenu na mungu akipenda tutakutana hapa hapa na kusutana na mimi nitawakumbusha hii michango yenu ya kunibeza wakati huo ukifika...lengo hapa lingekua na kuchukua kiti kile bila kujali silaha gani inatumika kuua sisimizi,ccm wana viti vingi cdm inahitaji kuongeza viti pale bungeni.
 
Umetoa wazo watu wote wamelipinga unakomaa nalo tuuuu! we vipi umetumwa? ushindwe.
tatizo langu kama umenifuatilia mimi huwa sijali kama namfurahisha ama namuudhi mtu bali hupenda kusema kile ambacho kipo ila watu wengi hawapendi kukisikia,mimi huwa nasema tu ili wasikie kwa nguvu!
 
Joshua Nasari ni kijana machachari anayekubalika pia

Madame WiseLady umenena ukweli Arumeru ni ya Joshua Nasari kamanda ambaye kusema na kufikili vinaenda pamoja. Mleta hoja ana mapepe ya mapepo akaombewe, pamoja na kwamba katiba inatuita wahaini kumuita Dr. Slaa Rais, mwache aendelee kutuongoza kwa matumaini makubwa mioyoni mwetu.:lol::lol::lol::lol::lol:
 
Kabla ya kuleta upupu hapa kashauri kwanza ccm wenzako namna ya kujivua gamba

ccm nao wakaidi na nyie hawasikii na ndio mana tunataka mtu kama slaa arudi akawachemshe tena kama enzi zile za EPA pale mwembe yanga!those were the days bwana sio sasa wabunge wengi lakini wabunge posho,slaa ni mtu wa kutetea maslahi yetu sisi wananchi sio posho ndio mana nampenda,yule ni new sokoine!
 
Kwa hadhi ya dkt.SLAA kusimama na MAGAMBA kwenye kinyang'anyiro cha ubunge ni kumdhalilisha kisiasa. Pia MAGAMBA wako tayari kuhamishia jeshi,vifaru mizinga, usalama wa taifa maguruneti, silaha zote za kivita vigagura na wachawi wao kwenye jimbo husika kuhakikisha dkt SLAA anashindwa.

Hadhi ipi aliyonayo?Hata tarime kwa chacha wangwe ccm walipeleka hayo majeshi,vifaru na mizinga lakini hayakufua dafu mbele ya mguvu ya umma ambayo cdm ilikua nayo,acheni kuiogopa ccm kupita kiasi,huo ni unyonge!
 
kim, unatumia nguvu nyingi sana ktk hoja zako! Hivi hujui kwamba tatizo la nchi hii ni system nzima ya uongozi? Hivi wewe unaamini dr akirudi mjengoni ndio tanzania itageuka kuwa paradise?. Binafsi sijaona fursa ambayo dr kaipoteza kwa kutokuwa mbunge kama ni nyaraka za serikali amezidaka anaweza kufanya kama alivyofanya wakati alipoitoa kwa umma ile list of shame. Na je hakuna mbunge wa cdm unayemuamini kwamba akitumwa na dr kitu fulani akakiseme /kukifanya bungeni atakifanya? Na je dr hawezi akaitisha press conference na waandishi wa habari na akanena lake jambo? Na je unaimani/evidence kwa kiasi gani kwamba hitaji la wana arumeru ni dr kuwa mbunge wao? Nina wasiwasi na uelewa wako kuhusu watu na demokrasia na muktadha wa siasa kwa ujumla.
akisemea bungeni kama mbunge ndio inanoga na kuinyima usingizi serikali,bila kuwa mbunge wapinzani wake watasema mwacheni aseme yuko katika jitihada za kufanya propaganda kukijenga chama chake,leo hii akiongea sam ruhuza mwenye cheo sawa na dr slaa(wote ni makatibu wakuu tu wa vyama vyao)neno lake linaweza kuwa na uzito kama akiongea kafulila ambae ni mheshimiwa mbunge?
 
nyie wachaga mna tabu sana.tamaa ya utajiri itawaua.hapo mnaitumia siasa kama kivuli tu hamna lolote wabaguzi wakubwa nyie.yaani mnafikiria uchaguzi mtu hajazikwa?kweli hiki ni chama maslahi
Una uhakika mwanzisha mada ni mchaga?...na je ni mwanachama wa CDM?...
 
Mkuu mimi naamini matendo yetu hapa duniani ndio yatafanya tupumzike kwa amani huko tuendako na si kwa maombi ya wanadamu,kwa hiyo hata mzee sumary matendo yake ndio hukumu yake,na si kwake ni kwa wanadamu wote

Mkuu nakuunga mkono,hata tukahamisha makazi yetu kwenye nyumba za ibada,hatutabadilisha hukumu ya Mungu. Swala la kuombea marehemu ni kupoteza muda.
 
...ni mazuzu wachache tu waliobakia na upofu wa kutokuona kuwa huu ni mwisho wa mwisho wa CCM
 
kweli mengi yamenenwa na wadau ila tatizo kubwa la Tanzania nchi yetu ni system ya elimu tunayoitoa mashulen,mavyuoni haimjengi mtu kufanya mambo kaajili ya watu wote bali inampa uwezo wakuona mahitaji yake tuu,Chadm chukueni jukumu la kuwaanda watanzani kuwa watu watakao fanyamambo kwamanufaa ya taifa siyo masilai ya m2 binafsi.Arumeru msimamishen mtu mwenye sifa hzo
 

Naam! Upendo wa shetani ni kuhakikisha unaishia pale alipo yeye - Jehanamu. Ushauri kutoka kwa mafisadi na magamba ni wa kuepukwa kama ukoma.
Ati shetani akizeeka anakuwa malaika mwema ni kweli?
 
tatizo langu kama umenifuatilia mimi huwa sijali kama namfurahisha ama namuudhi mtu bali hupenda kusema kile ambacho kipo ila watu wengi hawapendi kukisikia,mimi huwa nasema tu ili wasikie kwa nguvu!
Akili yako haina akili!
 
Dr slaa ni material ya urais tuu..cha msingi tuhakikishe hilo jimbo ni letu
 
Noooooo..... Bad idea, UNAMSHUSHA Dr. Slaa,
abaki na kujenga CDM.....
 
Nakubaliana na wale wote waliopinga hii idea ya Dr. Slaa kugombea jimbo la Arumeru. Kwanza kabisa itakuwa ni kujishusha kwa maana ya kwamba ameona ya kuwa amekosa urais na jimbo lake la Karatu hana tena ndo ameamua kugombea ubunge. Dr. Slaa ni zaidi ya ubunge wakuu. Kwa mtazamo wangu sasa hivi anao wasaa wa kutosha kuzunguka nchini na kufuatilia matatizo ya watu nchi nzima kinyume na ambavyo angekuwa mbunge kwani mara nyingi angekuwa limited kwenye jimbo lake. Watanzania wote wanahitaji kumfahamu Dr. Slaa na hasa vijiji. Kwa maana hiyo anaweza kujifahamisha kwa watanzania walio wengi kama atakuwa akifanya kazi na kuzunguka nchini nje ya majukumu ya kibunge. Jamani, tumwache Dr. Slaa atengeneze mazingira ya kuchukua uongozi wa nchi mwaka 2015 na tusimpe majukumu ambayo yanaweza kutekelezwa na vijana waliopo chini yake. CHADEMA ni chama kubwa na kuna vichwa vyenye akili sana ambavyo hata leo ukitaka vichukue nafasi za ubunge kwa nchi nzima vinaweza; lakini tunahitaji raisi ambaye ni Dr. Slaaaaaaaaaaa (aka bullets). Simjui kwa undani huyo Joshua Nasari ila kama wana Arumeri wanamkubali kwa nini tuwazue?
 
Nimekua kimya nikijaribu kufuatilia hoja zenu waungwana,mnaodai ukatibu mkuu wa slaa ni mkubwa kuliko ubunge,hoja yenu dhaifu sana,umaarufu wa slaa hautokani na ukatibu mkuu wake bali ulitokana na ubunge sasa kwa nini asirudi bungeni akamalizie kazi aliyoianzisha?au mnataka asubiri nafasi ya ubunge wa kuteuliwa na rais mwaka 2013 mwishoni kufuatia muafaka wa haya mazungumzo ya upenuni kati ya jk na mbowe?kama hamjui ndio tunakoelekea!

Na nyie mnaodai eti slaa ni rais mnamdanganya pamoja na kujidanganya nyie!na pia mnaosema eti sijui ataibiwa kura na kufirisika kisiasa pia ni uongo!hivi kura huwa zinaibiwaje?ndugu zanguni amkeni msikubali kudanganywa na wanasiasa,tatizo wanasiasa wetu wa africa huwa hawasemi ukweli kwa kuogopa kuwajibika kutokana na kushindwa chaguzi ndio huwa wanakuja na kisingizio cha kuibiwa kura wakishindwa,hivi hamjiulizi kama wizi wa kura upo kwanini cuf inairesa ccm pemba?au kwanini Ndesambura anaitesa kila wakati ccm moshi mjini?au kwanini Mzee Said Arfi makamu mwenyekiti wa cdm amekua kwa muda mrefu hata wakati slaa hajulikani amekua akiitesa ccm huko mpanda kwake?au zitto kwa nini anitesa ccm?Huwezi kuiba kura,huwa mnakua mmeshindwa tu,msidanganyike na watu kujaa kwenye mikutano yenu ya kampeni au hapa jf watu wengi kuonekana wanaipenda chadema,wengi sio wapiga kura!
Huenda unapiga kura USA au Uingereza lakini si Tanzania. Unachosema ni kuwa watu washinde kwa kura nyingi ili wasiibiwe. je, mgombea wa upinzani akishinda kwa kura 1000 ni halali tu aibiwe? Je hujaona sehemu ambako watu wamebeba mapanga na Marungu ndipo mpinzani anatangazwa mshindi? Labda unaandika ukiwa kwingine si hapa Africa na hasa Afrika mashariki.
 
Una uhakika mwanzisha mada ni mchaga?...na je ni mwanachama wa CDM?...

Ndio mimi ni mmachame ila kwa sasa siko tena chadema,nilikua huko kipindi cha uenyekiti wa Mzee Mtei na tulifanya kazi nzuri sana mpaka mwalimu nyerere alitusifu jinsi tulivyoanza tukaingia kwenye record ya kuwa chama cha kwanza cha upinzani kupata kiti bungeni japo ikaingia mizengwe ya bwana premji kukimbilia mahakani.Baadae akaja mzee Makani nae tukafanya nae kazi nzuri tu.Tulifanya siasa za kistaarabu,hatukumtukana mtu,hatukuandamana andamana wala kususa susa ovyo,hatuwahi kumwagia mtu yeyote asiekubaliana na sisi tndikali usoni..tulifanya siasa tu na wabunge tulipata wa kutosha na walifanya kazi nzuri pale bungeni kwa kushirikiana na wenzetu wa cuf na nccr,mbowe na slaa waulizeni wanajua haya ninayosema,walikua wabunge wetu tu.Mambo yalibadilika Freeman alipoukwaa uenyekiti!
 
Back
Top Bottom