Pay stubs za mshahara wa Rais

Pay stubs za mshahara wa Rais

Hukushukuru na kurdhika aliposema mshahara wake uliouhitaji kuujua bali ulitaka na posho, baadaye utataka ujue anazitumiaje.
Hakuna haja ya kuendelea kuwajibu watu wenye akili ya kusukumwa. Kwanini maswali yamekuwa yakiongezeka kila anapotoa jibu ikiwa na maana muuliza maswali anasubiri aambiwe cha kuuliza.

Wewe hata kusoma na kuelewa naona hujui.
 
Tafuteni kazi ya kufanya mshahara wa rais mshaujua kama unataka salary slip nenda ikulu ukaulizie.

Acheni mambo ya kike kufatilia mambo ya watu.. Nyummbu wakubwa!
 
Magufuli ni mtu wa 'stunts'...

Mara kapiga simu kwenye TV..

mara apige simu tena ataleta pay slip

mara aende bank mwenyewe.....mradi kila siku ana 'new stunts'....

kila siku yupo kwenye headline...asipofukuza huyu kaibukia huku....
Chief The Boss, Hivi ni jinai kwa JPM kama binadamu kujitimizia mahitaji yake ya kimsingi mwenyewe?

Iweje kitendo cha Vladimir Putin kupigwa picha akijiwekea mafuta mwenyewe kwenye gari lake kionekane ni kitendo cha mfano wa uwajibikaji, huku JPM kwenda kwenye tawi la Benki kupata huduma ionekane ni stunt?

Hayo mambo ni madogo mno kuweza kumkosoa mtu, ikilinganishwa na kazi anayowafanyia watu wake.
 
Rais Magufuli, wakati akiwa mapumzikoni huko Chato, iliripotiwa akinukuliwa kuwa akirudi Dar atatoa pay stubs za mshahara wake ili Watanzania anaowatumikia waujue.

Mpaka kufikia sasa, licha ya yeye kurudi Dar kwa zaidi ya wiki mbili sasa (niko tayari kusahihishwa maana siikumbuki vizuri tarehe aliyorudi), sijasikia wala kuona popote pale ambapo hivyo vitu alivyoahidi kuvitoa, kuwa kavitoa.

Naona hata watu walio wengi washasahau tena maana suala lenyewe hata halijadiliwi tena. Ni kama vile lishasahaulika....limekuwa upepo uliokwishapita.

Mimi hili suala siwezi kulisahau na msimamo wangu bado uko palepale. Watanzania walipa kodi wana haki ya msingi kabisa ya kujua pesa zao zinatumikaje.

Kwenye matumizi ya pesa za walipa kodi uwazi ni jambo la lazima.

Nasubiri kuziona hizo pay stubs za mshahara wa rais na asiishie hapo tu. Atuambie malipo yake yote yanayogharamiwa na walipa kodi.

Naamini yeye akifanya hivyo basi hata viongozi wengine wa umma nao wataufuata mfano wake.
fikiria hivyo hivyo...jpm alishasema hamna atakaechomoka, unahisi kasahau...ngoaj utapewa updates. mwizi anakimbizwa kimya kimya...
 
Hivi mshahara wa Rais unawasaidia nini?

Onesheni mfano kwa kuweka wazi pay slips zenu kama si muhali.
Rais wa nchi LAZIMA aonyeshe anapata net pay bei gani na anakatwa kodi bei gani!Nchi nyingi duniani viongozi wake hufanya hivi!By the way si alihaidi atatoa akifika tu Dar?

Ni aibu mm nikatwe kodi lkn wao hawakatwi kodi
 
Mwanamme kushikilia kuona pay slip ya mwanamme mwenzio ni majanga!

Hujiamini?

Hoja hapa sio mwanaume wala mwanamke, mbona hausemi chochote kuhusu yeye kutokutimiza ahadi yake ya kuonyesha slip? Nimeshakwambia hiyo ni pesa ya wananchi nnalipa kodi, kama tuna utawala bora na wa uwazi na alisema atatuwekea hadharani tusihoji? Nisijiamini kwa lipi? Majanga ni pale unapotetea kitu ambacho unaemtetea hajatimiza wajibu wake. Hiyo sio tu kwamba kwa sababu ni mwananume, hata kama angekua mwanamke ningehoji maadam analipwa pesa ya wananchi.

Na sio hivyo tu, ikumbukwe hili jambo limeshawahi kuleta sintofaham sio mara moja hadi ikulu wakakanusha kuhusu mshahara wa mkuu wa nchi, kuna tatizo gani likitolewa maelezo?
 
kwani yeye wale wanaolipwa 40 millions zinamsaidia nini? aoneshe na yeye salary slip yake ili tujue kweli kakomaa na wavuta pesa ndefu.
Yy mwenyewe anavuta pesa ndefu sana,tena afadhali hao akina Msechu wanakatwa PAYE,yy hakatwi hata senti

Anavuta mpunga mrefu huyu kama net pay
 
Pia kumbuka, mwanamme kusema kuwa ataipunguza hiyo mishahara mikubwa ni kujiamini.



mwanaume kushtaki wanaume wenzio ktk media kisa mishahara ya wanaume wenzio ni kukosa kujiamini na atapunguza kwa kigezo kipi ikiwa tayari watu washasainishana barua za mikataba ya ongezeko la mishahara akipunguza kibabe lazima sheria ichukue mkondo wake hadi muda huu hana pa kuanzia ni kosa kuingilia mshahara wa mtu au kuuchezea fuatilia kwa umakini ule mchoro wa january makamba nyani anavyopata tabu kurukaruka ktk matawi ya mti kuna watu chini wanamungalia tu na drama zake utapata jibu ..........
 
Back
Top Bottom