Ipi ni tuhuma Mkuu?Ile ni tuhuma, kawaida ya tuhuma ina majibu mawili
Ipi ni tuhuma Mkuu?Ile ni tuhuma, kawaida ya tuhuma ina majibu mawili
Wakuu habari za weekend nimepenyezewa habari kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye kwa sasa anatuhumiwa kughushi vyeti amerejea jioni ya leo akitokea Afrika ya Kusini.
Habari hizi zimethibitishwa na mpenyezaji kwani walikuwa wamepanda ndege moja kutokea huko kwa Madiba.
Dokezo zaidi linaonyesha Makonda atakuwa kwenye uzinduzi wa shughuli flani maeneo ya Kurasini!
Ohooo!Atakuwa kafata mke wake wasepe maana aliondoka kwa kukurupuka akasahau mke.
Wapi hii central police au oysterbay.. huyu Daudi ni muhalifu kama muhalifu mwengine.
Hatuna haja ya kwenda huko maana taarifa wanazo na zimewafikia kwa njia moja au nyingine na yamkini si ngeni kwao! Nijualo ni kuwa Mungu hutawala juu ya falme za watu! Ameruhusu wafalme watawale kwa haki na wasipofanya haki ataishinikiza haki mwenyewe!Tatizo tumebebeshwa akili na watu wachache.
Ukitaka vyeti nenda Ikulu utavikuta ndiyo mwajiri wake
Mimi na wewe ni wapiga kelele tu
HONGERA KWA KUTUMIKA.USAFI WA BWANA YULE NI KUONESHA VYETI FULSTOP.Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam mchapa kazi
Mchapa kazi na mbunifu.
Anayethubutu na asiyeogopa MTU kwa jina wala wadhifa wake
Mtetezi wa kizazi kinachopotea kwa madawa ya kulevya
Mbunifu wa ajira kwa vijana
Shujaa asiye tetereka
Mkuu wa Mkoa mwenye anayetaka mabadiliko
Mkuu wa Mkoa aliyetukanwa sana
Mkuu wa Mkoa asiyekataa tamaa
Mkuu wa mkoa atakayepiga vita mpaka mwisho madawa ya kulevya
Mkuu wa mkoa aliyetajwa sana kuliko wote toka Uhuru.
Mkuu wa mkoa wa kwanza kijana Dar
Mkuu wa mkoa asiyeangalia wala kujali unatoka chama gani anachotaka ni uwajibikaji tu.
Mkuu wa mkoa anayeaminika na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mkuu wa mkoa anayeandamwa hata na wabunge vita ya Madawa ya kulevya ktk mkoa wake
Mkuu wa Mkoa aliyeanzisha vita ya madawa ya kulevya Dar es salaam na sasa imeenea nchi mzima.
Mkuu wa mkoa aliyetoka familia masikini kabisa baba hajasoma kabisa na mama ni darasa la saba lakini amepata shahada moja na kuwatumikia wanainchi vile inavyopaswa.
Mkuu wa mkoa ambaye amesababisha baadhi ya watanzania kushikiwa akili na baadhi ya watu na hatimaye kuwafuata kila wasemalo na kuliamini.
Mpaka Leo 12 March 2017 hakuna aliyetuwekea ushahidi wa vyeti zaidi ya episode za Mch Gwajima tu.
Thubutu! Press conference mwisho chalinze, mjini ni mwendo wa machozi tu makanisani kuvutia huruma ya watanzaniaWelcome home mheshimiwa....
Ni matumaini yangu umeshaandaa vyeti na soon utakua na press conference
He who alleges must prove!!Kwa mujibu wa mfumo wetu wa sheria (commonwealth) Gwajima &Co. wana jukumu la kuthibitisha madai/tuhuma zao dhidi ya RC Makonda. Vinginevyo wakae kimya milele.