Paul Makonda afunguka

Paul Makonda afunguka

Big up Makonda Lowasa nani kwan siku zote ukweli humuweka mtu sehemu huru, na Watz hatutaki kuusikia ukweli

Huyu dogo hajitambua kuwa anatumika kama kifaa kufanya kazi chafu hata kama yeye akubiliani nazo.Katukana na kupiga Warioba,Sasa anamkashifu Lowassa. Lakini yupo kimya kwa manyangau waliochota Escrow kwani hajatumwa hilo.Mwisho wake atatupwa jalalani baada kumaliza kazi chafu.
 
Lowasa akiwa Rais wilaya kinondoni ataweka mkuu wa wilaya mpya. siku njema

Mkuu Lowassa sio mjinga,sana sana atampeleka chuo cha mafunzo Marekani au Uingereza ajifunze uchumi,uongozi na demokrasia.Ili apate mwanga wa kujitambua.
 

Chini ya utawala wa CCM, kila mtu, hata zezeta wa kiwango chochote anaweza kupewa cheo cha DC au RC. Haishangazi. Kwani wana kazi gani hasa?

Hii ndiyo principle ya sandakarawe. Kwa wale wanaokumbuka michezo ya utotoni.
 
Pichani Chini, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Akipiga usingizi wakati wenzie wanapiga kitabu enzi hizo MUccobs

IMG-20150220-WA0028.png
 
Baada ya kuona picha hii nachukia kuwa mtanzania. Hii ni nchi ya aibu Sana, its more than nepotism...

Mkuu MK254 naweza kupata uraia wenu bila kuoa binti toka Nyeri?

Mkuu Ulukolokwitanga ukifanikiwa na mie nahitaji uraia wa huko.. Ikishindakana hata wa Somalia utanitoa lol..
 
Last edited by a moderator:
Kama kazi ya Nyerere anapewa Makonda, basi Ukiona hivyo ujuwe siku za CCM zinahesabika
 
Ahaa hapo ni kichuguu na mlima.....jipime kabla ya kutamka yaliyomo moyoni mwako!
Anatafuta "kick" msemo wa vijana hii ni baada ya Nape kukomaa na mzee wa mvi enzi zile za jengo la umoja wa vijana na nyota yake ya uongozi ikang'aa kwa kuanza na Ukuu wa Wilaya mara cheo alichonacho sasa hivi kwenye chama. Labda na yeye anahisi atapita humu humu
 
huyu kibaraka kumbe ndo hizi kazi zake za utumwa ama mama wa nyumbani kweli ukuu wa wilaya kautumikia na kuu tolea jasho la kwa style zote. Pole kuwadi wa Riz one

Kwahiyo ataendelea na majukumu yake ya kumfunga kamba za viatu Riz1 licha ya kuwa DC?Hii kali!
 
Nimeamini watu wana nondo za uhakika.

Molemo,

Huyu bwana Tunamjua nje ndani,,,na yeye anatufahamu vizuri....nadhani atakumbuka lile sekeseke alipo pewa uwaziri mkuu na kada mwenzie pale MUCCOBs Bunge likamkataa kwa sababu ya Kupostpond mwaka kila Muda wa mtihani ukikaribia....Haaminiki Huyu kiazi.
 
Tanzania ya leo inataka watu kama akina MAKONDA, MWIGULLU na MUHONGO. haogopwi mtu na pesa zake anaogopwa Mungu tu, safi sana Makonda

Tafadhali sana huwezi linganisha Muhongo ,Mwigulu na Mpumbavu huyu Makonda.usirudie tena.
 
hata ufunguke vp makonda hutaweza kuwa msafi kwamba wewe uliwapiga wazee wa chama na kwamba ulishindwa kutumia vikao halali vya chama ukamtukana mwanachama mwenzio hadharaniii
 
Mkuu mpya wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda amefunguka na kutoa ya moyoni kuhusiana na shutuma kadhaa anazorushiwa kufuatia uteuzi wake.

Akizungumza na gazeti la Tanzania Daima Msemaji huyo wa Chipukizi wa UVCCM anesema ni kweli yasemwayo kwamba anatumika kumzima Waziri Mkuu Mstaafu Edward Ngoyai Lowassa anayetarajiwa kuomba uteuzi wa kugombea urais kupitia CCM.

""Hivi kati ya anayetumika kukibomoa chama na yule anayetumika kukiimarisha ni yupi ana Faida?....vijana ndiyo walinzi wa chama na sitakubali kiharibiwe na watu wachache wenye masilahi ya madaraka""" Alinukuliwa Makonda akisema

Source : Tanzania daima.

- Enzi za Kibanda lilikuwa gazeti la kuheshimika siku hizi limekuwa tawi la Mawio masikini njaaa bwana

Le Mutuz
 
Back
Top Bottom