Hapana,
Kikwete akiamua kufanya kweli kweli, mawaziri wengi kwenye serikali ya Ben pamoja na Ben mwenywe watakalia mkeka wa misumari, vile vile baadhi ya mawaziri wake mwenyewe watakalia mkeka huo huo wa misumari lakini yeye mwenyewe ataukwepa kirahisi.
Kwenye Serikali ya Ben, wengi wenye makosa ya kutumia madaraka yao vibaya na pengine kumshauri vibaya rais ni mawaziri, hayo hayana ubishi na watakalia kikaango kwa ajili hiyo. Ben mwenyewe ananing'inizwa juu ya kikaango hicho pamoja nao kwa kujifanya mjasiliamali huku akijifaidisha kibiashara kwa kutumia nafasi yake kama kiongozi wa nchi huku angali amepanga Ikulu. Katika serikali ya Ben, Kikwete hana rekodi ya kuingia mkataba wowote wenye utata kwa niaba ya nchi. Kuna comments, zinazohuzu sovereignty ya nchi, alizowahi kutoa kuhusiana na ununuzi wa rada wakati akiwa waziri wa mambo ya nchi za nje lakini yeye mwenyewe hakuwa ameshiriki katika mkataba ule.
Kwenye serikali yake mwenyewe, ataweza kuwaning'iniza mawaziri wake wote wenye skendo mbalimbali na hivyo yeye mwenye kubaki hana hatia yoyote kwa vile mawaziri atakaowaning'iniza ni wale waliokuwa wanamshauri vibaya ikiwa ni kinyume cha kiapo chao, na hivyo kuwa amejisafisha na kuwa safi kabisa.
nakuunga mkono mzee, kama kikwete akifanya kweli, watakao kalia msumari ni hao mawaziri etc, na kwa Mkapa naombea Bunge limvue kinga, na hata kama hato fungwa, wamfilisi mali zake na kumbakizia kidogo, zakumwezesha kumalizia siku zake, na ku-black list kwamba he was one of the worst president in Tanzania, ambaye hafai kuwekwa kwenye kumbuku za Viongozi, wastaafu.