Paukwa... Pakawa!

Zakumi,

Hapo umenena mkuu.

Kwenye Biblia kua sentenso inayosema "mwanadamu siku zake ni miaka 70"!

Sasa unajiuliza, je ukishajipatia kila kitu kama Johnson Lukaza alivyojichumia kabla hata ya kuwa na miaka 35, je ile mingine 35 iliyobakia atafanya nini?

Zaidi Uchotaji huu laiti ungekuw ani mara moja na utumike kama mtaji au msingi, bali huendelea milele.

Sasa kwenye uchotaji, kunakuja rushwa na kuvunja sheria nyingine ambako hufikisha kupotea au kutoweka kwa ushahidi muhimu.

Nikirudi kwenye nia halisi ya kusema kuwa hili ni changa la macho, kwa kina Jeetu Patel na Lukaza, sijui ni vipi tunaweza kuwashikisha adabu. Je hatuwezi kuwashitaki kwa kutumia ile sheria ya uhujumu uchumi na hata kuwafilisi?

Inapokuja kwa Yona na Mramba, hata ukiwaingiza kina Chenge, Lowassa, Karamagi, Meghji, Msabaha, Mgonja, Mboma na wengine, inakuwa kama ni tosha kuwamaliza kisiasa kwa kuwashitaki kwa uzembe, matumizi mabaya ya madaraka na kupotea kwa mali za umma kutokana na maamuzi mabovu na uongozi mbaya.

Nafikiri doa hili litanata kama gundi kuliko kutafuta wapi walificha hela!

Rev Kishoka:

Kama unatafuta mtaji basi ni lazima uwe na business plan. Na ukiwa na business plan basi ata pesa ya mkopo wa benki itakufanya uwe tajiri. Bottom line: watu hawana business plans na sio wafanya biashara.

Kama mchangiaji mmoja alivyosema wanasiasa wa bongo hawajuhi biashara. Na ukiwaondoa kwenye siasa, hawawezi kuishi.

Hivyo sita-entertain any idea kuwa mtu achukue pesa na akafanye biashara. Serikali ina wafanyakazi wengi na kila mmoja akisema achukue mara moja tu kama mtaji, hatutafika mbali. Na huu ndio mwanzo tulipoanzia, kila mtu alifikiri kuwa atachukua mara moja tu. Lakini imeonekana it's very easy kuichukua hiyo pesa kuliko kuifanyia kazi.

Binadamu wengi ni kama mkondo wa maji unaotiririka. Wakishaona njia nyepesi za kupita, basi ubunifu wa njia nyingine unakuwa hautumiki.

Kama ulisoma vitabu vya Abunuwasi, kuna jamaa alikuwa anapendwa na mfalme kwa sababu ya porojo zake na kila siku alikuwa anaalikwa kwenye meza ya chakula. Jamaa alijisahahu kufanya kazi. Taabu aliipata pale mfalme alipofariki na yeye kutotakiwa na warithi.

Watanzania wakiweza kuziba mapengo ya wizi wa mali za umma basi watu wataanza kuwa wabunifu wa njia zingine.
 
You nailed it Zakumi...Hata Mwinyi alishawahi kuwaambia wenzie lakini naona wanayapuuzia na kudhani ni uswahili as usual...Lakini ndo ukweli huo...Tanzania ya sasa imebadilika na hivyo wasitegemee ufisadi kuendelea kwa urahisi kama ilivyokuwa before.

Jmushi1:

Mimi ni Minimalist. Nachoangalia ni vitu gani fundamental vinavyoweza kukick-off something.

Idadi ya watanzania waliosoma, mwenye mwelekeo na ujuzi ambayo inaweza kukick-off maendeleo ya nchi hipo. Idadi hii sio kubwa lakini inaweza kufanya kazi za kutosha.

Ukichukua profiles ya wajerumani waliokuja kuanzisha koloni Afrika mashariki na vitu walivyovifanya katika kipindi cha muda mfupi japokuwa vilikuwa vya kutunyonya huwezi ukalalamika kwanini tupo masikini. It's simple as that.

Kinachotukwamishwa ni mentality za hawa wazee na ambazo baadhi ya vijana tumerithi.
 
Naona merikebu imekwama kwenye gati, hekaya ya Paukwa Pakawa imekuwa kweli, ushahidi hautoshi....Kesi zimeharisha (sic)!
 
Sijakuelewa mkuu.....

Kesi ya Yona, Mramba, Lukaza na Mgonja zimeishia wapi? Kama watu walipelekwa selo kijeshijeshi, tangu wametoka na dhamana miezi karibu mitatu sasa bado tunaendelea na upepelezi? au ndio Paukwa Pakawa?
 
Kesi ya Yona, Mramba, Lukaza na Mgonja zimeishia wapi? Kama watu walipelekwa selo kijeshijeshi, tangu wametoka na dhamana miezi karibu mitatu sasa bado tunaendelea na upepelezi? au ndio Paukwa Pakawa?

Na utekelezwaji wa mapendekezo (maagizo?) ya Kamati ya Mwakyembe umeishia wapi?
 
Sasa leo tunasoma kuwa Mramba anadai alimpelekea Rais Barua, Rais akaridhia. Mwendesha mashitaka anadai kuwa Mramba na Yona hawakumhusisha MWanasheria mkuu!

Hii kesi ikoje?

Zaidi, nauliza, ofisi ya Mwanasheria Mkuu ilihusika na mikataba mingine yote mibovu iliyoitia nchi yetu hasara. Je hatima ya uamuzi mbovu na uzembe uliofanywa na Mwanasheria Mkuu uliofikia kwa Taifa kupoteza hazina ili kuwafaidisha Wawekezaji, je tutasikia hivi karibuni waliokuwa wahusika wa mikataba niliyoitaja hapo mwanzo kuwa wanafikishwa mahakamani?

Je wale waliokiuka taratibu za kiuzabuni na utendaji kwa kisingizio cha Udharura na kutuletea Richmond?

Je wale waliokimbilia kuingia mkataba wa TRL nao tuwaweke wapi? Hata wale waliorudi na kuweka mkataba mpya wa ATCL na kukodisha Airbus mbovu ambao wamepewa madaraka mapya nao tuwafanyeje?

Je tukihamia kwa wale waliouza haki yetu kwa kugawa ardhi za kule Loliondo na Grumeti je haki ya Mtanzania itakuwa lini?

Ama kweli Paukwa Pakawa!
 
Back
Top Bottom