Part 3: TISS bado safari ngumu

Part 3: TISS bado safari ngumu

Mbona kila linalofeli nchi hii lawama ni kwa TISS !?

TISS haiwezi kufanya kila kitu. Jambo la msingi ni kuboresha taasisi zetu nyingine zifanye kazi kwa ubora.

Hii kuitegemea TISS ifanye kila kitu ndio inaturudisha nyuma. Kukitokea rushwa lawama kwa TISS, mikataba mibovu lawama kwa TISS. Wakati huo huo kuna taasisi zinazohusika na hayo mambo.

Tukiachana na hayo, mimi ukiniuliza ni kwa nini tunapiga hatua za polepole kwenye maendeleo, ntakwambia tatizo ni elimu.

Elimu yetu imetengeneza lundo la wasomi ambao mchango wao kwenye taifa hili ni kiduchu sana. Sana sana taifa linaingia hasara ya kuwahudumia tu.
Hivi leo yule mtoto wa dada au mjomba akimismanage uchumi hata MOSSAD wa ripoti wataishia kuficha ushauri
 
TISS wamebaki kuvaa miwani mieusi na mikwala mingi kumbe uwezo wao ni kwenda Facebook, Instagram na twitter kusaka watu wanaoikosoa serikali ili wawaumize!

Tuna Idara ya Ajabu sana awamu hii tangu tupate uhuru
Nasema hivi tuna Idara ya Ajabu sana tangu tupate uhuru.

Mimi nina imani zaidi na sungusungu wa mtaani kwetu kuliko TISS.
Angalau sungusungu wetu wanalinda watu wote kitaa bila kujali vyama vyao lakini TISS ya siku hizi imegeuka kuwa Idara kama Idara nyingine za CCM
Hakika, ulinzi shirikishi hauchagui nyumba wala kada, ni bora zaid yaTISS, hawa TISS kazi yao ni kulinda ccm na maslahi yake
 
Hata mm nashangaa mkuu.

Yaani TISS inachukuliwa kama mungu wa pili ni kosa sana hata nchi zilizoendelea kama marekani CIA kuna sehemu zina feli pia.

Pia Tiss sio private entity kwamba kuna robo, nusu au mwaka inatoa report kuonyesha walipofanikiwa au walipofeli ila wengi wetu humu tunafanya kuhisi na mihemko ya kukosoa TISS kana kwamba hawana mazuri zaidi ya mabaya tu mkuu.
Haya ya kulinda maslahi ya ccm kamwe hatuwez kuyaita mazur ya TISS, kuchunguza fb na Twitter na insta ili kuwabain wanaompinga jiwe katu si sehemu ya hayo mazur, pengine ungetuletea hapa hayo mazur
 
Sasa wewe ndugu yangu, kama TISS ipo imara utawapata wapi hao viongozi wabovu? Kazi mojawapo ya TISS ni kuhakikisha viongozi bora wanapendekezwa na kushika nyadhifa mbalimbali za utumishi wa umma. TISS ikiwa imara hakuna chama cha siasa kitaleta za kuleta wala kikundi chochote hakiwezi kufua dafu mbele ya TISS. Elewa TISS ndio nchi. Kama wewe ni mtu binafsi, chama, kikundi, n.k unataka ufanye utakavyo basi tafuta nchi yako.

Nchi sio taasisi moja, nchi ni muunganiko wa taasisi zote.

Marekani pamoja na kuwa na taasisi za kiusalama kubwa zaidi ya nne, wana Donald Trump sasa hivi.
 
Mkuu Easy Chair Mark III ,hichi kipengele kina Faida gani kama tunataka kusonga mbele ?.Yani Mh Rais asikosolewe kabisa ?

"Kumbuka ya kwamba, hata kuwaangamiza Watu RAIA wema ambao ni wakosoaji wa Rais au Serikali kwa nia njema, pia ni mafanikio KWA TISS, kulingana na natakwa ya Sheria mbalimbali, Kanuni NA Miongozo inayotumika ktk uendeshaji wa shughuli za TISS".
 
Mimi naona issue siyo TISS Bali ni mfumo (structure)autoi mwanya kwa taasisi kuendesha na kuzalisha njia Bora za kukuza uchumi..TISS wanatekeleza maagizo nazaidi wame priorities katika ulinzi wanchi na wananchi hasa siasa za ndani hawajikiti kiuchumi sana japo nayenyewe wapo but not to that extent watakiwa kuwekeza katika technology hasa ya viwanda ili Tanzania tuvuke.
 
Same tatizo na uajiri wa askari polisi..
Unaopelekea baadhi ya askari kuonyesha tabia mbaya zinazokwenda kinyume na mwenendo mwema wa jeshi la polisi..ktk kutekeleza majukumu yao..
Mkuu kila kinachotokea kinaakisi malezi na makuzi ya watu wa jamii husika.
Nimekaa mahali katika shughuli inayonipa fursa ya kushuhudia vizazi tofauti katika nchi yetu jinsi vilivyo kitabia,perceptions,matumizi ya akili,etc.Amini ndugu zangu kama tutaendelea hivi,ipo shida kubwa inakuja mbele.
Kizazi cha watu wanaojua kuwaza,kuamua na kutenda kwa usahihi kilirithiwa na kizazi cha watu wanaowaza,kuamua na kutenda bila kutathmini kama ni sahihi au la,nacho sasa kinarithiwa na kizazi cha watu wasiowaza,wasioamua wala wasiotenda,no guts at all.
Tujiulize,tumefikaje hapo?
Sasa usije ukawalaumu Tiss ilhali wanaruhusiwa kurecruit maafisa toka jamii isiyofikiri wala isiyotaka responsibilities kabisa,na bado ndani ya jamii hiyo hiyo,kutokana na corruption na undugulization,tiss inarecruit mbegu mbovu zaidi ktk jamii mbovu!
10 years ago nilikuwa nainteract na vijana ambao ukimwambia kesho njoo ofisini twende mahali sikuhitaji kumfundisha dressing code,leo hii nainteract na vijana ambao hata chupi yake tu anaionyesha nje,sasa mtu huyu ambaye chupi tu kuificha ni shida,unategemea aingie tiss na kuwa na siri hata akilewa pombe?
Wapo vijana wa tiss nawajua,yaani hadi najiuliza where are we going as a nation?!Tunakosea wapi,the problem is so deep rooted.
Katika situation ya hivi,tiss ilipaswa kuwa makini sana ili kupata wenye unafuu toka jamii hii iliyochoka kichwani.Ilihitaji sana mkono wa wazee wetu kutumia busara zao kongwe kuandaa kizazi kipya kwa njia sahihi.You just trigger it,na wanaendeleza mengine wenyewe.
Wazee hawawezi kwenda na sayansi ya sasa,ila hawashindwi kuandaa kizazi chenye maadili ya kupambana na changamoto za sasa.
Zamani tulikuwa tunatumia nguvu nyingi kuelekeza vitu vidogo kwa watoto wadogo ndani ya nyumba,sasa hivi tunatumia nguvu kubwa kuelekeza vitu vidogo hata kwa vijana wakubwa wa chuo kikuu,tunakoelekea tujiandae kutumia nguvu kubwa kutiisha jamii hata katika level za wafanyabiashara,askari,hakimu etc.Tatizo linazidi kupanda kichwani and who knows,maybe kuna siku tutalazimika kumtiisha hadi Rais na makamu wake ikulu,huku watu wa kufanya hivyo wakiwa hawapo,maana jamii itajaa watu wasiowaza na kutenda!Sijui nani atatukomboa.
 
Haya ya kulinda maslahi ya ccm kamwe hatuwez kuyaita mazur ya TISS, kuchunguza fb na Twitter na insta ili kuwabain wanaompinga jiwe katu si sehemu ya hayo mazur, pengine ungetuletea hapa hayo mazur
Ulijuaje mabaya ukashindwa kujua mazuri pia? Na unaweza kuweka ushahidi kwa hicho unachosema au hisia na mihemko?
 
Napenda kukujibu kama ifuatavyo:-
1.MAFANIKIO:-
Yapo, ingawaje mafanikio yenyewe ni "Hasi" KWA umma ( i.e. Negative Achievements), instead of Positive Achievements.

NB: Kutokana na Sheria na Kanuni zilizopo zinazosimamia TISS hivi sasa, ni vigumu sana kupata "Mafanikio Chanya" ambayo yataridhiwa na umma mpana zaidi wa wananchi wa Tz.Mafanikio yanayopatikana hayaweezi yakahesabiwa kuwa ni faida machoni pa wananchi wengi, ingawaje KWA mujibu wa Sheria na Kanuni za TISS inahesabika kuwa ni mafanikio.

Kumbuka ya kwamba, hata kuwaangamiza Watu RAIA wema ambao ni wakosoaji wa Rais au Serikali kwa nia njema, pia ni mafanikio KWA TISS, kulingana na natakwa ya Sheria mbalimbali, Kanuni NA Miongozo inayotumika ktk uendeshaji wa shughuli za TISS.

2. KUFELI:-
Kutokana na Sheria na Kanuni zilizopo zinazosimamia TISS, suala LA kufeli au kushindwa kupata Mafanikio Chanya yenye tija kwa maslahi mapana ya umma linakuwa ni jambo LA kawaida lisiloweza kuepukika.
Kufeli au kushindwa KWA TISS kunatokana NA kuwepo kwa Sheria, Kanuni NA Miongozo mibaya, iliyopitwa na wakati ambayo inatumika ktk kusimamia uendeshaji wa shughuli za kila siku za taasisi hii ya TISS. Kamwe Haramu haiwezi kuzaa Halali, haitatokea hata siku moja.

3.USHAURI:-
Njia pekee ya kuifanya TISS iwe Taasisi yenye manufaa kwa maslahi mapana ya umma wa wananchi wa Tz, kwanza kabisa ni:-
( i ) Kubadilisha Sheria, Kanuni, na Miongozo mbalimbali inayotumika ktk uendeshaji wa Kazi za kila siku za Taasisi hii nyeti, bila kusahau kuirekebisha Katiba ya nchi, ili ziendane NA mahitaji NA mazingira ya sasa ya Uchumi shindani KWA nguvu ya Soko, Maendeleo ya Sayansi NA Teknolojia, Utandawazi, etc.
( ii ) Kufanya Mapinduzi ya Fikra kupitia "ELIMU BORA"
ELIMU BORA ndio silaha nzito zaidi ya kuwezesha maendeleo endelevu mahali popote pale duniani.
Bila ya Elimu bora hakuna maendeleo wala mabadiliko Chanya yanayowezekana kutokea,
Mapinduzi ya fikra kupitia Elimu ni suala LA lazima KWA kila MTU ili kuleta maendeleo ya kweli.
ELIMU (Intelligence) ndio nyenzo kuu kabisa ktk kufanikisha utekelezaji WA majukumu yake yote ya Taasisi za UJASUSI mahali popote pale duniani, ndio maana zinaitwa "INTELLIGENCE SECURITY AGENCY"
Nakubaliana na wewe mkuu

Hivi ndio ilitakiwa iwe ili tuweze kupima MAFANIKIO, KUFELI na kipi kifanyike lakini kuja moja kwa moja na lawama as if Tiss hawana mazuri ndio sikubaliani nalo mkuu.
 
una logic ila hizo inaendelea zinachosha kwann usimwage mtama 1 kw 1
 
Nakuelewa sana, ila edit jina lako juu, lisomeke "my son drinks water ",,badala ya lilivyo
 
Ulijuaje mabaya ukashindwa kujua mazuri pia? Na unaweza kuweka ushahidi kwa hicho unachosema au hisia na mihemko?
Kwasababu yanaonekana hadharan, ushahid utaupata siku usipokuwa miongon mwao
 
Mbona kila linalofeli nchi hii lawama ni kwa TISS !?

TISS haiwezi kufanya kila kitu. Jambo la msingi ni kuboresha taasisi zetu nyingine zifanye kazi kwa ubora.

Hii kuitegemea TISS ifanye kila kitu ndio inaturudisha nyuma. Kukitokea rushwa lawama kwa TISS, mikataba mibovu lawama kwa TISS. Wakati huo huo kuna taasisi zinazohusika na hayo mambo.

Tukiachana na hayo, mimi ukiniuliza ni kwa nini tunapiga hatua za polepole kwenye maendeleo, ntakwambia tatizo ni elimu.

Elimu yetu imetengeneza lundo la wasomi ambao mchango wao kwenye taifa hili ni kiduchu sana. Sana sana taifa linaingia hasara ya kuwahudumia tu.

Ukisikia matumizi mabaya ya ubongo kufikiri, ndio kama haya sasa!
 
Mbona kila linalofeli nchi hii lawama ni kwa TISS !?

TISS haiwezi kufanya kila kitu. Jambo la msingi ni kuboresha taasisi zetu nyingine zifanye kazi kwa ubora.

Hii kuitegemea TISS ifanye kila kitu ndio inaturudisha nyuma. Kukitokea rushwa lawama kwa TISS, mikataba mibovu lawama kwa TISS. Wakati huo huo kuna taasisi zinazohusika na hayo mambo.

Tukiachana na hayo, mimi ukiniuliza ni kwa nini tunapiga hatua za polepole kwenye maendeleo, ntakwambia tatizo ni elimu.

Elimu yetu imetengeneza lundo la wasomi ambao mchango wao kwenye taifa hili ni kiduchu sana. Sana sana taifa linaingia hasara ya kuwahudumia tu.
Kwa hiyo TISS wamefanya nini baada ya kuona elimu yetu ni mbovu?
 
Hii ni mada ya watu wenye akili? mjinga Kama wewe unatakiwa upite kimya kimya tu, kwa sababu hujui hata nilichokiandika, hata Rais akisoma hapa kuna mahali atapata point za kufanyia kazi
😂😂😂😂Hapo pa Rais umeniua mbavu
 
Usalama wa taifa unaoshindwa kujua twiga wanapanda ndege, ndege zinatua migodini kuchukua dhahabu na kuondoka, meli zinapakua mizigo na kuondoka! Watafutiwe jina jipya.
 
Hawawezi kumdhibiti, kwa kuwa lengo lao ni kuuishikilia huo muhimili mpaka watakapo muweka mtu wao 2020.
FB_IMG_1568747148995.jpg
 
Back
Top Bottom