Part 3: TISS bado safari ngumu

Part 3: TISS bado safari ngumu

Nafahamu kwamba Tiss inahusika na kukusanya taarifa na kuzuia baadhi ya matukio ya kiusalama, lakini core component ya utendaji wa hizo taasisi upo chini ya uongozi na wafanyakazi wa hizo taasisi.

Leo hii kila kitu lawama kwa TISS, wakati ukiangalia ni management mbovu, utendaji mbovu, na ubunifu sifuri ndio unaosababisha kukwama kwa vitu vingi.
Inteligensia ipo kila mahali, uchumi, utawala, shuleni, viwandani, technologia. We kama unadhani TISS haihusiki upo nyuma sana. Unaishi dunia ya kale mno.
 
Mbona kila linalofeli nchi hii lawama ni kwa TISS !?

TISS haiwezi kufanya kila kitu. Jambo la msingi ni kuboresha taasisi zetu nyingine zifanye kazi kwa ubora.

Hii kuitegemea TISS ifanye kila kitu ndio inaturudisha nyuma. Kukitokea rushwa lawama kwa TISS, mikataba mibovu lawama kwa TISS. Wakati huo huo kuna taasisi zinazohusika na hayo mambo.

Tukiachana na hayo, mimi ukiniuliza ni kwa nini tunapiga hatua za polepole kwenye maendeleo, ntakwambia tatizo ni elimu.

Elimu yetu imetengeneza lundo la wasomi ambao mchango wao kwenye taifa hili ni kiduchu sana. Sana sana taifa linaingia hasara ya kuwahudumia tu.
TISS ndio nchi yenyewe kama hujui. Hata ungekuwa na elimu kiasi gani huwezi kufanya jambo lolote la maana kama TISS hawataki. Nakuhakikishia hata kama una uwezo wa kujenga kiwanda kikubwa kiasi gani, kilichopo eneo halali kabisa kama TISS hawataridhika na wewe huwezi! Wewe ni 'mgeni' kwenye utawala wa nchi. Nchi ina wenyewe, sisi wengine hata tungekuwa na cheo kikubwa kiasi gani kama TISS wakisema NO! Huwezi kwenda tofauti nao 'ukaishi'. Hata huyu mzee wetu vituko anavyofanya vya kuwaumiza wenzake ni kwamba TISS wameridhia. Wakisema hatutaki hiki lifanyike hana ubavu wa kukataa. Maan ukiwakatalia wanachokisema kwa maslahi ya nchi basi wewe utaondoka ili Taifa libaki salama. Kwa hiyo kwa ujumla TISS ndio mhimili wa nchi. Hakuna anayeweza 'kukohoa' mbele ya TISS kama wakisema hili hapana. Kwa hiyo hata Musiba TISS waliamua wamwache afanye atakavyo, lakini wangesema MUSIBA 'stop' misiba yako hatuitaki hangekuwa na jeuri ya kuendelea kufanya chochote. Hivyo ndugu yangu jua ya kwamba hakuna mwenye ubavu kuliko TISS ndani ya nchi yoyote duniani. TISS ikiwa dhaifu nchi itakuwa dhaifu tuuuu! Tunaiombea TISS ya nchi yetu iwe imara kwa Taifa imara.
 
Tatizo la hii nchi ni CCM. Maana hawa ndio wanatumia vyombo vya umma kulinda mafisadi, utawala wa mafisadi, interests za mafisadi. Nchi itabadilika sana kama taasisi hii itafanyiwa marekebisho ya sheria juu ya utendaji wake. Chombo hiki kinapaswa kuwa huru bila kuingiliwa na mtu yeyote.
Maccm hawataki kusikia haya.
 
Inteligensia ipo kila mahali, uchumi, utawala, shuleni, viwandani, technologia. We kama unadhani TISS haihusiki upo nyuma sana. Unaishi dunia ya kale mno.
Huyu jamaa kwa kweli yupo nyuma sana! TISS ipo kila mahali hadi chumbani kwake lakini hajui eti! TISS ni mpiga debe, muuza nyanya, mwalimu, mkulima, padri, mchungaji, Askofu, Shehe, Profesa, Daktari, Hakimu, Rubani, mfagiaji wa stendi, mfagiaji wa ofisi, sekretari, vibaka, watekaji, majambazi n.k. Yaani tumezungukwa na TISS kila mahali. TISS ni kila kitu, kila mahali, kila kazi. Ukisikia majambazi wamekamatwa kwenye msitu fulani ujue ndani ya hao majambazi alikuwamo TISS akatoa taarifa ya mahali walipo. Ndio ulinzi wa nchi wenyewe. Sasa utajuaje genge la wahuni lipo mahali fulani bila anayejua hilo kukwambia? Ndio maana tunasema acha uhalifu maana utanaswa tu. Hii maana yake tutawatuma watu wetu wawe na hali uliyonayo ili tukupate. Ukiwa kibaka tutakuletea kibaka wetu atuchoree ramani. Ukiwa afisa wa serikali mwizi tutakuletea afisa awe katika ofisi yako ili mpange wizi na sisi tukukamate. Funzo ni kwamba usifanye uhalifu ukifikiri hutakamatwa, utanaswa tu. Kama wewe ni mpenda rushwa tutakuletea 'mtoa rushwa' tukunase.
 
Hata mm nashangaa mkuu.

Yaani TISS inachukuliwa kama mungu wa pili ni kosa sana hata nchi zilizoendelea kama marekani CIA kuna sehemu zina feli pia.

Pia Tiss sio private entity kwamba kuna robo, nusu au mwaka inatoa report kuonyesha walipofanikiwa au walipofeli ila wengi wetu humu tunafanya kuhisi na mihemko ya kukosoa TISS kana kwamba hawana mazuri zaidi ya mabaya tu mkuu.
Watu wanakosoa ili walipofanya ndivyo-sivyo wasahihishe makosa yao ili kuepuka athari mbeleni. Wakisharekebisha hayo makosa ndio huzaa hayo mazuri.
 
Nafahamu kwamba Tiss inahusika na kukusanya taarifa na kuzuia baadhi ya matukio ya kiusalama, lakini core component ya utendaji wa hizo taasisi upo chini ya uongozi na wafanyakazi wa hizo taasisi.

Leo hii kila kitu lawama kwa TISS, wakati ukiangalia ni management mbovu, utendaji mbovu, na ubunifu sifuri ndio unaosababisha kukwama kwa vitu vingi.
Sasa wewe ndugu yangu, kama TISS ipo imara utawapata wapi hao viongozi wabovu? Kazi mojawapo ya TISS ni kuhakikisha viongozi bora wanapendekezwa na kushika nyadhifa mbalimbali za utumishi wa umma. TISS ikiwa imara hakuna chama cha siasa kitaleta za kuleta wala kikundi chochote hakiwezi kufua dafu mbele ya TISS. Elewa TISS ndio nchi. Kama wewe ni mtu binafsi, chama, kikundi, n.k unataka ufanye utakavyo basi tafuta nchi yako.
 
Kuna msemo mmoja unasema "KUMKOSOA MWENYE DIGRII UNATAKIWA KUWA NA DIGRII AU MASTAZ"

Kukosoa taasisi nyeti kama TISS inabidi ujue mfumo ambao unatumuka katika recruitment, utendaji, level za reporting, mipaka, nk.

Na kuyajua yote hayo ni kwa yule mwajiriwa tu na si wa cheo vha kawaida bali mtu mwenye cheo.

Vinginevyo ni porojo na upotoshaji uliotukuka.
"Elimu SI kupanda kidato".
 
Hata CCM kama wanafanya mabaya ni kwa sababu TISS imeruhusu au imezembea kutimiza wajibu wake. Hakuna mbabe mbele ya TISS. Kwa asili TISS haina maslahi na chama wala mtu yeyote wa cheo chochote! Ina maslahi na nchi. Ipo tayari 'kumpoteza' yeyote kama anahatarisha maslahi ya nchi.
 
Hata CCM kama wanafanya mabaya ni kwa sababu TISS imeruhusu au imezembea kutimiza wajibu wake. Hakuna mbabe mbele ya TISS. Kwa asili TISS haina maslahi na chama wala mtu yeyote wa cheo chochote! Ina maslahi na nchi. Ipo tayari 'kumpoteza' yeyote kama anahatarisha maslahi ya nchi.
Uvccm ndio tithi
 
Nafahamu kwamba Tiss inahusika na kukusanya taarifa na kuzuia baadhi ya matukio ya kiusalama, lakini core component ya utendaji wa hizo taasisi upo chini ya uongozi na wafanyakazi wa hizo taasisi.

Leo hii kila kitu lawama kwa TISS, wakati ukiangalia ni management mbovu, utendaji mbovu, na ubunifu sifuri ndio unaosababisha kukwama kwa vitu vingi.
Utendaji mbovu, je huko hakuna TISS? kwamba hawa jamaa wanatuharibia nchi tuwatoe fasta. Wako wapi?
 
Watu wanakosoa ili walipofanya ndivyo-sivyo wasahihishe makosa yao ili kuepuka athari mbeleni. Wakisharekebisha hayo makosa ndio huzaa hayo mazuri.
Mnasahihisha kwa kutumia tafiti gani au mihemko na hisia tu?
 
TISS wapo katika kila Taasisi unayoifahamu hapa nchini

Logic ya mleta Mada haizungumzii kusambaa kwao kwa kila Eneo ,analenga Matokeo ya Kazi zao au wewe umeelewaje Mkuu ?.Matokeo yenye Faida zaidi ya Hasara ndio Muhimu zaidi ,kuliko kulinda Madaraka ya wana Siasa.
 
Kuna msemo mmoja unasema "KUMKOSOA MWENYE DIGRII UNATAKIWA KUWA NA DIGRII AU MASTAZ"

Kukosoa taasisi nyeti kama TISS inabidi ujue mfumo ambao unatumuka katika recruitment, utendaji, level za reporting, mipaka, nk.

Na kuyajua yote hayo ni kwa yule mwajiriwa tu na si wa cheo vha kawaida bali mtu mwenye cheo.

Vinginevyo ni porojo na upotoshaji uliotukuka.

Kila kitu au Ubora wa kitu kinapimwa kwa Ufanisi wake na Ufanisi ni Matokeo tu ,kuisifia tu Taasisi flani ni kubwa/Imara bila ya kuipima kwa kuambatanisha na Matokeo ya Sifa unazo ipatia kueleweka itakuwa ni ngumu kwa wale wanao fikiri zaidi.

TISS haitakiwi kuishia ktk Ulinzi wa kuangalia Adui anatokea wapi ,waende mbele kwa kuangalia Maslahi mapana ya Nchi na sio ya Mtu mmoja au kakikundi flani.Mleta Mada ameelezea Maendeleo ktk Nchi nyingine ,usifikiri yalikuja hivi hivi tu.
 
Basi nadhani tatizo sio kwa wakosoaji. Bali lipo kwako unayechambua mambo kwa kutumia moyo badala ya ubongo.
Mnasahihisha kwa kutumia tafiti gani au mihemko na hisia tu?
 
Basi nadhani tatizo sio kwa wakosoaji. Bali lipo kwako unayechambua mambo kwa kutumia moyo badala ya ubongo.
Nakubaliana kwamba mleta uzi katumia MOYO badala ya UBONGO sawa sawa.

Binafsi mleta post angeleta tafiti kujua MAFANIKIO, KUFELI na USHAURI kipi kifanyike ili Tiss ifanye vizuri zaidi ningemuelewa lakini anapondea mwanzo mwisho kana kwamba hawana MAFANIKIO
 
Nakubaliana kwamba mleta uzi katumia MOYO badala ya UBONGO sawa sawa.

Binafsi mleta post angeleta tafiti kujua MAFANIKIO, KUFELI na USHAURI kipi kifanyike ili Tiss ifanye vizuri zaidi ningemuelewa lakini anapondea mwanzo mwisho kana kwamba hawana MAFANIKIO
Usiwe zipu ya pochi ndugu. Tafakari upya.
 
Mimi nahisi waliomo TISS nawenyewe hawajui nini sababu yawao kuwapo hapo au hawajui nn majukumu yao

Wapo baadhi wanajitambua lakini wapo wengi ambao hawajitambui.
Tatizo kubwa ni Elimu duni, ulimbukeni ktk kazi kulikochangiwa na Sheria mbaya zinazosimamia kazi zao.
 
Nakubaliana kwamba mleta uzi katumia MOYO badala ya UBONGO sawa sawa.

Binafsi mleta post angeleta tafiti kujua MAFANIKIO, KUFELI na USHAURI kipi kifanyike ili Tiss ifanye vizuri zaidi ningemuelewa lakini anapondea mwanzo mwisho kana kwamba hawana MAFANIKIO

Napenda kukujibu kama ifuatavyo:-
1.MAFANIKIO:-
Yapo, ingawaje mafanikio yenyewe ni "Hasi" KWA umma ( i.e. Negative Achievements), instead of Positive Achievements.

NB: Kutokana na Sheria na Kanuni zilizopo zinazosimamia TISS hivi sasa, ni vigumu sana kupata "Mafanikio Chanya" ambayo yataridhiwa na umma mpana zaidi wa wananchi wa Tz.Mafanikio yanayopatikana hayaweezi yakahesabiwa kuwa ni faida machoni pa wananchi wengi, ingawaje KWA mujibu wa Sheria na Kanuni za TISS inahesabika kuwa ni mafanikio.

Kumbuka ya kwamba, hata kuwaangamiza Watu RAIA wema ambao ni wakosoaji wa Rais au Serikali kwa nia njema, pia ni mafanikio KWA TISS, kulingana na natakwa ya Sheria mbalimbali, Kanuni NA Miongozo inayotumika ktk uendeshaji wa shughuli za TISS.

2. KUFELI:-
Kutokana na Sheria na Kanuni zilizopo zinazosimamia TISS, suala LA kufeli au kushindwa kupata Mafanikio Chanya yenye tija kwa maslahi mapana ya umma linakuwa ni jambo LA kawaida lisiloweza kuepukika.
Kufeli au kushindwa KWA TISS kunatokana NA kuwepo kwa Sheria, Kanuni NA Miongozo mibaya, iliyopitwa na wakati ambayo inatumika ktk kusimamia uendeshaji wa shughuli za kila siku za taasisi hii ya TISS. Kamwe Haramu haiwezi kuzaa Halali, haitatokea hata siku moja.

3.USHAURI:-
Njia pekee ya kuifanya TISS iwe Taasisi yenye manufaa kwa maslahi mapana ya umma wa wananchi wa Tz, kwanza kabisa ni:-
( i ) Kubadilisha Sheria, Kanuni, na Miongozo mbalimbali inayotumika ktk uendeshaji wa Kazi za kila siku za Taasisi hii nyeti, bila kusahau kuirekebisha Katiba ya nchi, ili ziendane NA mahitaji NA mazingira ya sasa ya Uchumi shindani KWA nguvu ya Soko, Maendeleo ya Sayansi NA Teknolojia, Utandawazi, etc.
( ii ) Kufanya Mapinduzi ya Fikra kupitia "ELIMU BORA"
ELIMU BORA ndio silaha nzito zaidi ya kuwezesha maendeleo endelevu mahali popote pale duniani.
Bila ya Elimu bora hakuna maendeleo wala mabadiliko Chanya yanayowezekana kutokea,
Mapinduzi ya fikra kupitia Elimu ni suala LA lazima KWA kila MTU ili kuleta maendeleo ya kweli.
ELIMU (Intelligence) ndio nyenzo kuu kabisa ktk kufanikisha utekelezaji WA majukumu yake yote ya Taasisi za UJASUSI mahali popote pale duniani, ndio maana zinaitwa "INTELLIGENCE SECURITY AGENCY"
 
Back
Top Bottom