Part 3: TISS bado safari ngumu

Part 3: TISS bado safari ngumu

Ukitaka kufanikiwa kimaisha, jifunze kwa watu waliofanikiwa, jenga urafiki na watu wenye mafanikio, jipendekeze kwao, jifanye mjinga siku ipite, kumbe lengo lako kuna kitu unachokitafuta.

Usijifanye mjuaji, kubali kukosolewa, pokea mawazo ya watu mbalimbali kisha uyachuje na kuchukua yale unayoona yanaweza kukusaidia, hiyo ndo siri ya mafanikio.

Idara yetu ya usalama wa taifa inatakiwa iige mafanikio ya idara zilizofanikiwa zaidi Duniani, MOSSAD, MI6,CIA,PSIA(Japan) huwezi kufanikiwa kwa kuendelea kuiga mifumo iliyoshindwa, na ndo maana kila kitu chetu hakiendi, tumebakia kuwa watu wa kulia lia kila siku na umaskini usio koma.

Sikushangaa kumwona waziri mkuu wetu akizindua Gereza, kuzindua Gereza ni mkosi, ni balaa, ni nuksi, ni laana, ni futureless.

Duniani pote ktk ufuatiliaji wangu wa habari za mataifa mbalimbali sijawahi kuona kiongozi mkuu wa serikali kwa level ya waziri mkuu akizindua Gereza, bali huwa nawaona wakizindua viwanda.

Kuzindua Gereza ni ishara ya kukata tamaa, unazindua ili nani akalale humo?

Wakati Uholanzi wanafunga magereza sisi tunazidi kuyajenga, 95% ya uhalifu inasababishwa na hali mbovu ya uchumi na si vinginevyo.

Ni idara ya usalama wa taifa pekee ndo yenye uwezo mkubwa wa kutengeneza mazingira ya utawala bora yanayopelekea uchumi imara kwa watu wake, hili Japan na Israel wamefanikiwa sana.

Kwa sasa Israel ina kiwango cha maisha bora mno kwa watu wake kuliko nchi nyingi tu za Ulaya.

Israel ni nchi ya 20 Duniani kwa kuwa na uchumi bora, na ni nchi ya pili Duniani baada ya Marekani kuwa na makampuni makubwa ya Technology na kampuni zingine kubwa kuzidi kuwekeza Israel na siyo China ambayo wengi wanaisifia, huu ni utundu uliotukuka wa vijana wa MOSSAD.

Mossad wanatumika kuhakikisha Israel iko salama kwa kitu, haki, Demokrasia, utu, uzalendo vimetamalaki Israel.

Sasa unawezaje kuwaiga Rwanda hao choka mbaya badala ya kutamani kuwa Kama Japan au Israel?

Binafsi huwa natamani kuwa na pesa nyingi na mafanikio Kama MO Dewji, sitamani kuwa maskini.

Huwa natamani sana kuiona Tanzania ikifanikiwa kiuchumi Kama Australia, ukiwa ktk nchi hii huhitaji maneno ya magazeti ya kisiasa kuwa eti nchi uchumi umekua, mandhali ya nchi na watu wake pekee yatosha kukujulisha kwamba hii ni nchi yenye uchumi mzuri.

Naporudi nyumbani Tanzania huwa nakaribishwa na mandhali iliyopauka kimaskini na nyuso za watu waliokata tamaa kwa ugumu wa maisha, Halafu nikienda kwenye kibanda cha magazeti nakutana na habari ya uchumi wa Tanzania kuzidi kupaa, naishia kucheka kwa huzuni.

Mtu mmoja alikuwa akitibiwa India eti kila siku gharama za matibabu ni sh mil 150, huyu naye mlishindwa kumdhibiti kwa wizi mkubwa wa kishamba hivi?

INAENDELEA
Mkuu unakosea tena.
Hakuna mahala idara za usslsma zikawa Think Tanks za maendeleo ya kiuchumi.

Pengine nikufungue macho....

"An intelligence agency is a government agency responsible for the collection, analysis, and exploitation of information in support of law enforcement, national security, military, and foreign policy objectives. ...Intelligence agencies can provide the following services for their national governments.

-Give early warning of impending crises;

-Serve national and international crisis management by helping to discern the intentions of current or potential opponents;

-Inform national defense planning and military operations (military intelligence);

-Protect sensitive information secrets, both of their own sources and activities, and those of other state agencies;

-Covertly influence the outcome of events in favor of national interests, or influence international security; and Defense against the efforts of other national intelligence agencies (counter-intelligence).
Ref: Wikipedia

Kifupi Tiss ni kulinda mafanikio na kuimarisha usalama wa nchi.
 
Mkuu hata ww unaruhusiwa kusifia hayo mazuri.
Siwezi kusifia au kuponda kwa kutokana na mihemko na hisia tu dhidi ya Tiss kuliko hali halisi mkuu.

Maana ukiwa unaandika MAKALA lazima utakuwa na tafiti ya kutosha ambayo yatajikitika kwenye vitu vifuatavyo (1)MAFANIKIO (2) KUFELI (3) KUSHAURI ili wasomaji tufanye COMPARISON ya asilimia ngapi wamefanikiwa,wamefeli na kipi kifanyike sio zinaletwa LAWAMA za jumla jumla kwamba taasisi haina MAFANIKIO zaidi ya KUFELI tu mkuu.

Nafikiri jamaa ana chuki binafsi dhidi ya IDARA, sijui imemfanyia nini kibaya?
 
Mkuu unakosea tena.
Hakuna mahala idara za usslsma zikawa Think Tanks za maendeleo ya kiuchumi.

Pengine nikufungue macho....

"An intelligence agency is a government agency responsible for the collection, analysis, and exploitation of information in support of law enforcement, national security, military, and foreign policy objectives. ...Intelligence agencies can provide the following services for their national governments.
-Give early warning of impending crises;
-Serve national and international crisis management by helping to discern the intentions of current or potential opponents;
-Inform national defense planning and military operations (military intelligence);
-Protect sensitive information secrets, both of their own sources and activities, and those of other state agencies;
-Covertly influence the outcome of events in favor of national interests, or influence international security; and Defense against the efforts of other national intelligence agencies (counter-intelligence).
Ref: Wikipedia

Kifupi Tiss ni kulinda mafanikio na kuimarisha usalama wa nchi.

Kwa hiyo hili jukumu la kuteka ni la kulinda mafanikio au usalama wa nchi?
 
Vijana wa TISS siku hizi wala hawajifichi na hawajui kutunza siri. TISS anashinda baa halafu anajitambulisha kabisa akilewa. Na ukimfuatilia unagundua kweli huyu ni TISS. Hawajui kuwa ufanisi wa kazi yao unategemea usiri na kutojulikana kwao. Wanaume wa MOSAD na CIA hata mke wake hawezi kujua kama mumewe ni agent. Na ikitokea akajulikana basi anaacha kazi mara moja kwa sababu ni rahisi kuwa compromised akishajulikana. Sasa hawa UVCCM sijui hawajui maadili ya kazi zao. Mpaka kwa michepuko yao hawachelewi kuropoka kuwa wao ni TISS na wako juu ya sheria.

Binafsi nawadharau sana !!!
 
Sikushangaa kumwona waziri mkuu wetu akizindua Gereza, kuzindua Gereza ni mkosi, ni balaa, ni nuksi, ni laana, ni futureless.

Duniani pote ktk ufuatiliaji wangu wa habari za mataifa mbalimbali sijawahi kuona kiongozi mkuu wa serikali kwa level ya waziri mkuu akizindua Gereza, bali huwa nawaona wakizindua viwanda.

Kuzindua Gereza ni ishara ya kukata tamaa, unazindua ili nani akalale humo?

Wakati Uholanzi wanafunga magereza sisi tunazidi kuyajenga, 95% ya uhalifu inasababishwa na hali mbovu ya uchumi na si vinginevyo.
 
Mbona kila linalofeli nchi hii lawama ni kwa TISS !?

TISS haiwezi kufanya kila kitu. Jambo la msingi ni kuboresha taasisi zetu nyingine zifanye kazi kwa ubora.

Hii kuitegemea TISS ifanye kila kitu ndio inaturudisha nyuma. Kukitokea rushwa lawama kwa TISS, mikataba mibovu lawama kwa TISS. Wakati huo huo kuna taasisi zinazohusika na hayo mambo.

Tukiachana na hayo, mimi ukiniuliza ni kwa nini tunapiga hatua za polepole kwenye maendeleo, ntakwambia tatizo ni elimu.

Elimu yetu imetengeneza lundo la wasomi ambao mchango wao kwenye taifa hili ni kiduchu sana. Sana sana taifa linaingia hasara ya kuwahudumia tu.
Mzee hao ndio kionambali chetu. Ndio watu tunaowategemea watuvushe hapa tulipo. Kushindwa kwao ndio kushindwa kwetu. Hao ndio wanaotakiwa kutoa viashiria hatarishi kabla havijatokea, ndio watu wenye darubini ya kuakisi kushindwa au kufanikiwa kwa malengo yetu.
Kama hawawezi tutaendelea kupiga kwata palepale tulipo. Hao ndio wazalendo namabri wani. Hawana kuremba wala kusuka, hata kama kiongozi anakosea haraka sana wanaelewa ni nini kifanyike ili kunusuru na kurekebisha mambo kwa haraka na ufanisi wa hali ya juu.
 
Watawala waione TISS kuwa ni chombo cha nchi na si cha dola . Nao wajivunie taifa lao na si watawala maana huja na kuondoka na taasisi iko palepale.
mkuu TISS wanawajibika kwa kila hatua na kila maamuzi ndani ya nchi hii, kauli za viongozi kubariki wananchi kuua vibaka ni kielelezo TISS hawawezi kunusa tena bali wameshikwa pabaya na Viongozi wa kisiasa... tatizo la ukosefu wa ajira, upotevu wa raia, maisha kuwa magumu na ukosefu wa huduma za kijamii kama maji ni kielelezo pia taasisi hii nyeti imesahau majukumu yake na kujipatia majukumu mengine kama vile PSU na kuratibu usalama wa chama na viongozi wa chama pekee.

NOTE... TISS inatakiwa kuundwa upya kwa malengo mapya kwa maana ujamaa siyo agenda yetu tena.
 
Hiyo Australia inaikuta Tanzania kwa uzuri?
Duh? Uzuri upi mkuu? Labda wa papuchi, Kuilinganisha Australia na Tanzania ni sawa na kulingalisha mavi na keki.
Hapa kila raia serikali inajua anaishije, na akikwama kwa lolote iwe ajira, Elimu, matibabu au makazi serikali inajua namna ya kumsaidia, huko Tanzania mnaambiwa hapa kazi tu wakati hata kazi hakuna.
Yaani wananchi wa Tanzania hawana tofauti na mbwa koko anayeishi kwa kusakua jalalani na kuiba chakula kwa Binadamu akikuta mlango wazi.
 
Kuna msemo mmoja unasema "KUMKOSOA MWENYE DIGRII UNATAKIWA KUWA NA DIGRII AU MASTAZ"

Kukosoa taasisi nyeti kama TISS inabidi ujue mfumo ambao unatumuka katika recruitment, utendaji, level za reporting, mipaka, nk.

Na kuyajua yote hayo ni kwa yule mwajiriwa tu na si wa cheo vha kawaida bali mtu mwenye cheo.

Vinginevyo ni porojo na upotoshaji uliotukuka.
Akili Uliyonayo wewe ni ndogo mno, ndo maana hujaielewa mada yangu hata kidogo, ungekuwa na akili usingehangaika ku comment ujinga kiasi hiki...
 
ORODHA YA WAKURUGENZI WAKUU WA 'TISS' TANGU UHURU.

Idara ya usalama wa Taifa (TISS) imeundwa kwa sheria ya bunge namba 15 ya mwaka 1996 (Tanzania Intelligence and Security Service act No. 15 of 1996) iliyosainiwa na Rais Benjamin Mkapa tarehe 20 mwezi Januari mwaka 1997. Sheria hiyo ndio inayoipa mamlaka Idara hiyo kufanya kazi zake ndani na nje ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Pamoja na idara hii kusajiliwa kisheria mwaka 1996, lakini ilkuwepo tangu wakati wa utawala wa kikoloni chini ya ofisi ya Gavana wa Tanganyika. Baada ya Uhuru mwaka 1961 ilihamishiwa ofisi ya Rais.

Tangu idara hii kuanzishwa hadi sasa imeongozwa na Wakurugenzi 9 akiwemo Diwani Athumani Msuya aliyeapishwa jana.

Wa kwanza ni mzee Emilio Mzena, huyu aliongoza mwaka 1961 hadi mwaka 1975. Ndiye Mkurugenzi wa TISS aliyeongoza idara hii kwa miaka mingi zaidi kuliko wengine (miaka 14). Aliaminiwa na Mwalimu Nyerere baada ya idara yake kuzima majaribio kadhaa ya kumpindua.

Wa pili ni Dr.Lawrence Gama (PhD). Huyu alipokea kijiti kutoka kwa Mzena. Aliongoza kwa miaka mitatu tangu mwaka 1975 hadi mwaka 1978, kabla ya Mwalimu Nyerere kumuondoa katika nafasi hiyo na kumteua kuwa mkuu wa mkoa wa Dodoma.

Wa tatu ni Dr.Hassy Kitine (PhD) ambaye aliongoza idara hii kwa miaka miwili toka mwaka 1978 hadi 1980. Kitine alichaguliwa kuongoza idara hiyo nyeti akiwa kijana wa miaka 36 tu. Anakumbukwa kwa jinsi alivyoiwezesha TISS kushirikiana na Idara ya Usalama na Utambuzi Jeshini (MI) Chini ya Meja Jenerali Tumainieli Kiwelu, kuiteka nyara ndege ya makomandoo kutoka Libya iliyokuja kumsaidia Idd Amin katika vita ya Kagera.

Mwaka 1980 Mwalimu Nyerere alimteua kijana mwingine mwenye miaka 35 Dr.Agustine Mahiga (PhD) - ambaye ni waziri wa sheria kwa sasa - kuwa Mkurugenzi mkuu wa 4 wa TISS. Aliongoza idara hiyo hadi mwaka 1983, alipomuondoa na kumpeleka kuwa Kaimu Balozi wa Tanzania (Minister Plenipotentiary) nchini Canada.

5. Baada ya Mahiga kwenda Canada, Mwalimu Nyerere alimteua Luteni Jenerali Imrani Kombe kuwa Mkurugenzi mkuu wa 5 wa TISS mwaka 1983. Nyerere alipong'atuka alimuacha kombe kwenye idara hiyo na alidumu hadi mwaka 1995.

June 30 mwaka 1996 Jenerali Kombe aliuawa na Jeshi la polisi kwa madai kuwa walifananisha gari lake (Nissan Patrol) na gari iliyokua imeibiwa na mtuhumiwa Ernest Mushi maarufu kama "White".

Alimininiwa risasi 4 kifuani licha ya kushuka kwenye gari na kunyoosha mikono juu kama ishara ya kusurrender. Askari waliohusika na mauaji hayo walihukumiwa kunyongwa lakini Rais Kikwete aliwapunguzia adhabu mwaka 2011. Bado kifo cha Jenerali Kombe kina maswali mengi kuliko majibu.

Mwaka 1995 Rais Mkapa alimteua Kanali Apson Mwang'onda kuwa Mkurugenzi Mkuu wa 6 wa TISS ambaye aliongoza idara hiyo hadi mwaka 2005 alipostaafu.

Mwaka 2005 Rais Jakaya Kikwete alimteua Othman Rashid kuongoza idara hiyo hadi mwaka 2016 alipostaafu. Othmna Rashid alikuwa Mkurugenzi wa 7 wa idara hiyo.

August 24 mwaka 2016 Rais John Magufuli alimteua Mchungaji Dr.Modestus Kipilimba (PhD) wa Kanisa la City Harvest Church la jijini Dar es Salaam kuwa Mkurugenzi Mkuu wa 7 wa TISS. Kabla ya uteuzi huo Kipilimba alikua Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya taifa (NIDA).

Mchungaji Dr.Kipilimba amedumu katika nafasi hiyo hadi September 12 mwaka huu alipotenguliwa uteuzi wake na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna wa Polisi CP Diwani Athumani Msuya.!

By Malisa
Hongera kwa kuweka kumbukumbu sawa!.
 
Mkuu unakosea tena.
Hakuna mahala idara za usslsma zikawa Think Tanks za maendeleo ya kiuchumi.

Pengine nikufungue macho....

"An intelligence agency is a government agency responsible for the collection, analysis, and exploitation of information in support of law enforcement, national security, military, and foreign policy objectives. ...Intelligence agencies can provide the following services for their national governments.

-Give early warning of impending crises;

-Serve national and international crisis management by helping to discern the intentions of current or potential opponents;

-Inform national defense planning and military operations (military intelligence);

-Protect sensitive information secrets, both of their own sources and activities, and those of other state agencies;

-Covertly influence the outcome of events in favor of national interests, or influence international security; and Defense against the efforts of other national intelligence agencies (counter-intelligence).
Ref: Wikipedia

Kifupi Tiss ni kulinda mafanikio na kuimarisha usalama wa nchi.
Well said!.
 
magereza lazima yajengwe kwa kasi ili wachochezi kama wewe muhifadhiwe huko, Israel ndio wanaongoza kwa kuvunja haki za wapalestina, usijitoe akili.
Kama jina lako ndilo hilo uchumi kwako ni sawa na makalio kwa maana nayo yana kazi muhimu tena maalum.
 
Mbona kila linalofeli nchi hii lawama ni kwa TISS !?

TISS haiwezi kufanya kila kitu. Jambo la msingi ni kuboresha taasisi zetu nyingine zifanye kazi kwa ubora.

Hii kuitegemea TISS ifanye kila kitu ndio inaturudisha nyuma. Kukitokea rushwa lawama kwa TISS, mikataba mibovu lawama kwa TISS. Wakati huo huo kuna taasisi zinazohusika na hayo mambo.

Tukiachana na hayo, mimi ukiniuliza ni kwa nini tunapiga hatua za polepole kwenye maendeleo, ntakwambia tatizo ni elimu.

Elimu yetu imetengeneza lundo la wasomi ambao mchango wao kwenye taifa hili ni kiduchu sana. Sana sana taifa linaingia hasara ya kuwahudumia tu.
Hasara ipi ya kuwahudumia wasomi? kuna mahali watu wanatibiwa bure? kuna mahali serikali inapeleka chakula for free?, wapi serikali imepeleka mashuka na blanket kwa sisi walala vibarazani? Hiyo mikopo wanayopewa wanafunzi ndo unaita gharama? wakati unaskia inaitwa mikopo?

Gharama ipi aise?
 
wewe unashangaa kuzindua gereza.

kuna siku utashangaa mheshimiwa anazindua ebola kuingia Tanzania. na wabunge watampongeza kwa kuzindua ebola.
 
Mbona kila linalofeli nchi hii lawama ni kwa TISS !?

TISS haiwezi kufanya kila kitu. Jambo la msingi ni kuboresha taasisi zetu nyingine zifanye kazi kwa ubora.

Hii kuitegemea TISS ifanye kila kitu ndio inaturudisha nyuma. Kukitokea rushwa lawama kwa TISS, mikataba mibovu lawama kwa TISS. Wakati huo huo kuna taasisi zinazohusika na hayo mambo.

Tukiachana na hayo, mimi ukiniuliza ni kwa nini tunapiga hatua za polepole kwenye maendeleo, ntakwambia tatizo ni elimu.

Elimu yetu imetengeneza lundo la wasomi ambao mchango wao kwenye taifa hili ni kiduchu sana. Sana sana taifa linaingia hasara ya kuwahudumia tu.
Inteligensia ipo kila mahali, uchumi, utawala, shuleni, viwandani, technologia. We kama unadhani TISS haihusiki upo nyuma sana. Unaishi dunia ya kale mno.
 
Back
Top Bottom