Panya Road wavamia Chamazi

Panya Road wavamia Chamazi

Kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia nilizopenyezewa na raia wema ni kwamba genge hatarishi la Panya Road limefanya uhalifu usiku huu katika maeneo ya Chamazi (Jimbo la Mbagala) na sasa wamekusanyika karibu na eneo la chuo cha afya cha Muhimbili lililopo Chamazi, wakilenga kuendelea na uhalifu wao kama kawaida. Hivi sasa wananchi wako roho juu wakihimizana kufunga milango ya nyumba zao na kuepuka kutoka nje ili kujilinda na uhalifu wa genge hili la kimafia linalozidi kutikisa jiji la Dar es Salaam siku hadi siku.

Nimeuweka uzi huu hapa kwa makusudi. Panya Road wametufikisha hapa baada ya kushindwa kudhibitiwa kikamilifu na vyombo vya ulinzi.

Tutapeana taarifa baadaye kadri ninavyozipata kutoka eneo la tukio. Wananchi wanaishi kwa hofu kubwa kufuatia kundi hili linalojibadilisha kila kukicha kutoka genge la wahalifu na kuwa kundi la kigaidi. Serikali inapaswa kuchukua hatua kuwalinda raia na mali zao na ikibidi wananchi wamilikishwe silaha nzito kwa ajili ya kujilinda wao wenyewe na mali zao. Kuna haja ya kuanzisha mafunzo ya lazima ya kijeshi kwa wananchi ili kuwajengea uwezo wa kujilinda.
majeruhi%20issa%20joseph.jpg


Scorpion ndo funga kazi yao hao .. Wamwachie huko aliko waone kama hawa panya watasikika
 
toa taarifa polisi immediately
Hujui kama vituo vya Polisi vyote Dar Vinafungwa jioni hadi Asubuhi Saa Moja ndio vinafunguliwa kama mnabahati watu wa Patrol wakipita ndio ahuheni yenu la sivyo jifungieni tu... ila msisahau kulipa kodi na Anzisheni Sungusungu tu mitaani mwenu maana hamna njia nyingine za kuwalindeni...
 
Nadhani pale Chamazi kuna kituo cha polisi. Vipi huna namba zao uwapigie wachukue hatua za haraka? Hilo eneo la Muhimbili hakika ni hatarishi sana. Lipo wazi kwa vile halijajengwa ijapokuwa limezungukwa na makazi ya watu. Nakumbuka pia jirani na hilo eneo kuna Bar nadhani inaitwa Last Card. Mliopo Chamazi mtanisahihisha

Mara hii ushasahau maamuzi ya Kukurupuka ya Serikali yako ya CCM kuwa vituo vyote vidogo vya Polisi vifungwe saa12 jioni?ile last card inayotazamana na kigango Katoliki ni ya General mmoja mstaafu wa JWTZ.
 
Dar hivi kweli mmekosa hata wanaume kumi wa ukweli ambao wanaweza kuwa paka road kwaajili ya kuwakabili hao panya?....hebu siku moja mjitutumue muache kulalamika ovyo
Wanaume wa dar ni lege lege ila ninachoshangaa ni kwamba hawa panyaroad wanavamia maskini tu mbona hawaendi kwa ma sonko? Oysterbay,mbezi beach, mikocheni, upanga na kwingineko?
 
Daaaah! Bora niendelee kubaki mkoani maana huku huwatunasahau kufunga milango makusudi....usiku kucha na unakuta flat yako na sabufa vpo salama
 
Hawa panya road watashugulikiwa,katika historia Ya Tanzania hakuna kikundi cha uhalifu kinachodumu,kulikuwa na komando yosso nini panya road time is the real master.
 
Wananchi wa Dar siku tukigeuka paka hao panya watakoma.Tuache kulialia,tuchukue hatua.
 
Wananchi wa Dar siku tukigeuka paka hao panya watakoma.Tuache kulialia,tuchukue hatua.
 
Mi nadhani mob justice itawafaa hao panya road. Wanaume wa dar jipangeni, hizi thread za kulaani,kulialia na kupeana tahadhari hazitowasaidia.
Komaeni!
 
Back
Top Bottom