They have nothing to lose except their chains.Mmmmmh hao panya Road wamerudi tena
Anzisheni Doria za mitaamkuu, lakini nadhani pia tangu polisi walipoacha kukaa vituoni usiku kundi hili limepata kasi ya kuendelea kuwatesa raia na kuwanyima raha kabisa. serikali inapaswa kufikiria upya uamuzi wake wa kufunga vituo ili polisi wachache waliopo washirikiane na wananchi kutokomeza kundi hili la kigaidi.
Hata hii ni taarifa, sasa tuone .toa taarifa polisi immediately
Mbona vituo vya polisi naskia vinafungwa saa 12 jioni kwa ajili ya kuogopa majambazi. Chezea nchi ya Tanganyika!Chamazi hakuna kituo cha polisi?
Au nao wametoka nduki?
Akili ndogo za mifugo ya TANAPAMzunguko mdogo wa hela mitaani ni moja ya kichocheo cha matukio haya.
Kwa mtazamo wangu,hawa ni vijana waliokata tamaa ya maisha na wako tayari kwa lolote kwani wanaona hawana cha kupoteza.
Mkuu, ni kweli kabisa wala hujakosea. Hata mimi kuna siku nilipita pale nikaona ule uwazi na giza nene linalotanda pale wakati wa usiku huwachochea panya road kufanya uhalifu wao.Nadhani pale Chamazi kuna kituo cha polisi. Vipi huna namba zao uwapigie wachukue hatua za haraka? Hilo eneo la Muhimbili hakika ni hatarishi sana. Lipo wazi kwa vile halijajengwa ijapokuwa limezungukwa na makazi ya watu. Nakumbuka pia jirani na hilo eneo kuna Bar nadhani inaitwa Last Card. Mliopo Chamazi mtanisahihisha
Mafunzo ya nn,itapelekea kuongezeka kwa matukio ya uhalifu.Ni kweli. Hili kundi hata sijui limeibukaje wakati Dar ilikuwa imenza kuwa tulivu. Serikali inapaswa kuwapa wananchi mafunzo ya kijeshi na kuwamilikisha silaha kwa ajili ya kujilinda na makundi ya kipuuzi kama hili la Panya Road.
hawa mbwa wanaojiita panya road, kamwe hawawezi kustawi kwenye maeneo ya wanaume kama haya. thubutu!NATAMANI SANA WAFIKE HUKU KWETUView attachment 420413