Pale unapowaacha dakika mbili peke yao...

Pale unapowaacha dakika mbili peke yao...

Hahaaa hahaaa... Aisee mi huwa naamini kuwa mtoto unavyotaka awe ndio atakavyokuwa.. Ukimfeed with the correct info na behaviors ataziishi tu maana akiwa mdogo ubongo wake hauna kitu so ukimpa matango pori ataendelea nayo vivo hivyo ukimpa vitu sahihi
Daah ndio maana tunawaona kina Junior na vituko vyao sio kwa malezi haya, yaani mtoto anafanya uharibifu unamchekea
 
Duh! vp ukimkuta mwanao anafanya ivyo utampiga?
Hahahahahahah siwezi mpiga mkuu Mara ya kwanza nitamkanya ila akirudia ni kichapo

Nakumbuka siku hiyo baba alikasirika sana ila hakutuchapa alituambia tusirudie kuogesha kuku ni vibaya, halafu akagomba kweli...kumbe alisema ili tusifanye tena na kweli tukaacha
 
Nimecheka sana. Mlikuwa mngundua nini. Umenikumbusha Baba yangu aliniagiza nikamtose kuku kwenye maji kwa mara moja aliyetoka kuatamia ili utitiri umtoke. Nilipofanya hivyo kuku agaogelea hadi ng'ambo ya mto, nikamrudishia tena, dada na kaka wanatoka shule wakanikuta naendelea kumtosa. Kuku hadi manyoya yote yakaisha. Nikambiwa mle mbichi mama akaniokoa kwa kumkaanga
Hahahahahahah yaan hapo ulikuwa unaenjoy anavyoogelea eti. Na ungemla mbichi ukome ukorofi...

Yaani sijui hata tuliwaza nini ila tulikuwa tunashindana tu nani kuku wake atatakata zaidi hahahahahh......hatukuchapwa ila tulisababisha hasara kubwa maana kuku walishindwa kutotoa kwa sababu ya yale maji maji
 
Hahahahahahah yaan hapo ulikuwa unaenjoy anavyoogelea eti. Na ungemla mbichi ukome ukorofi...

Yaani sijui hata tuliwaza nini ila tulikuwa tunashindana tu nani kuku wake atatakata zaidi hahahahahh......hatukuchapwa ila tulisababisha hasara kubwa maana kuku walishindwa kutotoa kwa sababu ya yale maji maji
Hiyo midomo hapo kwenye avatar ni yakwako?
 
Hahahahahahah siwezi mpiga mkuu Mara ya kwanza nitamkanya ila akirudia ni kichapo

Nakumbuka siku hiyo baba alikasirika sana ila hakutuchapa alituambia tusirudie kuogesha kuku ni vibaya, halafu akagomba kweli...kumbe alisema ili tusifanye tena na kweli tukaacha
ila nakushauri usimnyime mtto fimbo.
 
Ki binamu changu, kilikuwa kinatamani simu yangu yake ya kuchezea hazitaki, kuna simu yangu nyingine siku hiyo nimeisahau, na Mara nyingi alikuwa anaipenda acheze game, siku hiyo nimetoka akaichezea mwisho ikachafua akatafuta Maji na sabuni na dodoki, kaweka kwenye beseni oshaa sugua baadae akaianika juani.
Narudi kuuliza simu akasema imechafuka kaifua kaanika juani dah!😁😁😁😁
 
Kuku gani? Wa kienyeji?
Hii thread imenikumbusha tukiwa wadogo tuliwachukua kuku waliokuwa wanatamia tukawa tunawaogesha na kuwasugua miguu kwa brush,, halafu tunawarudisha kwenye mayai na Yale maji maji wakashindwa kutotoa
 
Back
Top Bottom