Pale unapowaacha dakika mbili peke yao...

Pale unapowaacha dakika mbili peke yao...

Watoto wanafurahisha sana...

Utotoni nakumbuka nilichoraga passport ya mshua kurasa kwa kursa kwa rangi za maji za kucholea...



Cc: mahondaw
 
Hayo ni malezi mabaya ya watoto..watoto wanatakiwa wakaripiwe kwa ukali wanapofanya uharibifu mara ya kwanza ili asirudie tena nashangaa comment nyingi za watu humu eti wanasema baada ya kufanya uharibifu unaishia kuwaangalia tu huna la kufanya,seriously!!?..hakuna kitu nisichokipenda kama kutiana hasara hata kama ni mtoto inatakiwa ajue ukomo wa utundu wake mwisho ni wapi..sasa nipekidogo amepewa hasara ndani ya miezi mitatu lakini ameendelea kumchekea mtoto tu kashindwa hata kumkaripia?
 
Watoto jamani, daaah!! jana tu usiku mwanangu ametoka shule, akawa hajabadili t-shirt ya shule. Mama yake anasema alisikia ukimya kama wa sekunde kadhaa, ile kuhamaki, dogo ameshika mkasi anacharanga t-shit yake ya shule akiwa ameivaa. lol!!
 
Haaa haaaa haaa wa kwangu, nilijitutumua nikanunua TV flat screen size 43 Inch, narudi toka job nakuta amepasusua na nyundo TV ikiwa na miezi 3 niliishia kushika kiuno huku yeye ananikimbilia kuniwawooo, kwakweli alichonifanyia Mungu anamuona!
hahhahahhhah
 
Ha ha haa....kuna jamaa yangu nimemuuzia simu juzi, kesho yake anatoka kazin akakuta watoto washafanya Yao kwenye charger yaani haifai, ikabidi anunue mpya buku teni..
 
Afu ukute kuna mzazi atawakung'uta watoto kama punda *****.

I have 2 little boys ambao wamefatana. sidhani kuna ambacho sijakiona bado. Wakiwa kimya ujue kinachofata ni mapigo ya moyo kuongezeka.

Mmoja akiwepo kutatulia kidogo. Wait wawe pamoja.[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

May Allah grant the gift of parenthood to all those that seek it. Ameen.
Ameen
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] vituko vya watoto bana

Wakwangu alishawahi kuchukua goroli akarusha kwenye screen ..nilipomuuliza akanijibu alikua anajaribu aone Kama itapasuaka

Siku nyingine akaja na mpya akajitupa kwenye meza(coffee table) nilimchapa kwakweli
 
Hii thread imenikumbusha tukiwa wadogo tuliwachukua kuku waliokuwa wanatamia tukawa tunawaogesha na kuwasugua miguu kwa brush,, halafu tunawarudisha kwenye mayai na Yale maji maji wakashindwa kutotoa
 
Back
Top Bottom