Samiaagain2025
JF-Expert Member
- Dec 2, 2020
- 2,926
- 3,054
Mtume Yohana(mbatizaji) aliwekwa gerezani kwa kosa la kumkosoa Gavana kwa kuoa mtoto wa ndugu yake.Kwa hiyo kazi ya mtumishi wa Mungu haiishii hapo unapodai wewe.Popote pale kwenye uovu lazima akemee.Ndiyo maana mtumishi wa Mungu lazima awe kichwa na si mkia.Yaani pamoja na mengine,yampasa aelewe mambo yote na awe na uwezo kukemea mabaya.Kazi ya kiongozi wa kikristo ni moja tu kuwaambia watu tubuni na kuiamini injili, kinyume cha hapo hamna kiongozi wa kikristo hapo ni mbwa mwitu tu aliye ndani ya uongozi wa kanisa
Hakuna kiongozi wa kikristo anayetumwa na Mungu kuhubiri kuhusu katiba au tume za uchaguzi sababu katiba duniani kila nchi ina zake na zinatofautiana kati ya nchi na nchi na tume zinatofautiana kati ya nchi na nchi na nchi zingine hazina kabisa sababu hazifanyi chaguzi hutawaliwa kifalme nk lakini injili ni ile ile kwa mataifa yote dunia nzimandio maana Yesu akaagiza viongozi wake waende duniani pote wahubirie watu watubu na kuiamini injili ambayo ni ile ile jana leo na hata mile haibadiliki.Katiba zitabadilika injili haibadiliki.TUME ZA UCHAGUZI ZITABADILIKA INJILI HAIBADILIKI
Mtaalamu mmoja alisema ili nchi iendelee inatakiwa kila mmoja asimame kwenye nafasi yake afanye kile alichopewa mkulima alime sana kwa nguvu zake zote na akili zake zote az
Hivyo acha kupotosha.