BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,792
- 287,994
Nathan Peter (pichani) au Padre Haule ambaye ni Kasisi wa Kanisa Anglikana Tanzania ameamua kujilipua kwa kuandika yafuatayo katika kuchangia andiko langu katika ukurasa wangu:
"Kama unatumwa na wenye mihimili hiyo sawa usintamaze kwani nawe ni wao, lakini Kama unajituma, Anza kutafiti alipo mzee mtikila na anachokifanya kwa Sasa."
Maneno ya Padre huyo siyo ya kupuuza. Anagusia wenye mihimili na anaongea kuhusu Mtikila pasipo kumtaja Mtikila yupi! Inawezekana Padre anajua kilichompata Mtikila anayemtaja na sababu za kumpata hayo yaliyompata. Kuna uhusiano gani kati ya yaliyompata Mtikila na yanayoweza kumpata Askofu Mwamakula, hatujui. Labda Baba Padre anajua! Askofu anajua kuwa huyo Padre ni kada wa chama kimoja cha siasa nchini ingawa hajui uhusiano wake na hao wenye mihimili au Mtikila
Nilipokuwa mdogo, jirani kulikuwa na Kambi ya Jeshi kule Ipyana na Kibugujo (Kyela)! Tulifundishwa kutokuwapuuzia watu tukikutana nao maporini! Kuna mmoja alikuwa anajifanya kichaa na kuishi mwituni kumbe kule msituni alikuwa ameweka ofisi yake shimoni! Bila shaka ujumbe wa Padre kwa Askofu Mwamakula umefika!
Ni vizuri Padre na wengine wakatambua kuwa Askofu ataongoza hayo "Matembezi ya Hiyari" nchi nzima na wala hahitaji kufanya utafiti wa kazi anayoifanya huyo Mtikila aliyetajwa! Askofu alizaliwa siku moja na atakufa siku moja iwe kwa ugonjwa, risasi, sumu, ajali, uzee, au kuliwa na wanyama wakali, nk haijalishi!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
"Kama unatumwa na wenye mihimili hiyo sawa usintamaze kwani nawe ni wao, lakini Kama unajituma, Anza kutafiti alipo mzee mtikila na anachokifanya kwa Sasa."
Maneno ya Padre huyo siyo ya kupuuza. Anagusia wenye mihimili na anaongea kuhusu Mtikila pasipo kumtaja Mtikila yupi! Inawezekana Padre anajua kilichompata Mtikila anayemtaja na sababu za kumpata hayo yaliyompata. Kuna uhusiano gani kati ya yaliyompata Mtikila na yanayoweza kumpata Askofu Mwamakula, hatujui. Labda Baba Padre anajua! Askofu anajua kuwa huyo Padre ni kada wa chama kimoja cha siasa nchini ingawa hajui uhusiano wake na hao wenye mihimili au Mtikila
Nilipokuwa mdogo, jirani kulikuwa na Kambi ya Jeshi kule Ipyana na Kibugujo (Kyela)! Tulifundishwa kutokuwapuuzia watu tukikutana nao maporini! Kuna mmoja alikuwa anajifanya kichaa na kuishi mwituni kumbe kule msituni alikuwa ameweka ofisi yake shimoni! Bila shaka ujumbe wa Padre kwa Askofu Mwamakula umefika!
Ni vizuri Padre na wengine wakatambua kuwa Askofu ataongoza hayo "Matembezi ya Hiyari" nchi nzima na wala hahitaji kufanya utafiti wa kazi anayoifanya huyo Mtikila aliyetajwa! Askofu alizaliwa siku moja na atakufa siku moja iwe kwa ugonjwa, risasi, sumu, ajali, uzee, au kuliwa na wanyama wakali, nk haijalishi!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula