Osama bin Laden killed!

Osama bin Laden killed!

Status
Not open for further replies.
Ukijaribu kufuatilia sana diplomasia ya Marekani utapata wazimu, juzi wamedai wamemuua Osama, wanayemwelezea kuwa alikuwa mtu "hatari," leo nasoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa Marekani "inafikiri" kuwa Al-Zawahiri ndiye atakuwa mrithi wa Osama, kwa jinsi walivyomwelezea huyo jamaa ninanukuu Gazeti la Mwananchi

"Zawahiri ndiye aliyekuwa anaongoza Kundi la Al-Qaeda, katika kuishambulia Marekani kwa akitumia silaha nzito za maangamizi.Makachero sita wanaopambana na ugaidi na baadhi ya watu wanaomfahamu Zawahiri, walikiambia Kituo cha Televisheni cha Al Jazeera kuwa kwa miaka mitatu sasa, Zawahiri amekuwa kimya, akiendesha operesheni za chini kwa chini.

"Sasa amekuwa kimya akiendesha operesheni za Mtandao wa Al Qaeda kisayansi na kwa kutumia utalaamu wa hali ya juu," mmoja wa maafisa hao alisema.Mwaka 2008, Zawahiri aliandika kitabu kilichokuwa kinaelezea historia na umahiri wake katika kutumia sila nzito za mabomu aina ya nuclear na mtazamo wenye misingi ya dini wa Mtandao wa Al-Qaeda, kuhusu kuua watu wengi kadiri iwezekanavyo.

Kitabu hicho pia, kinaonyesha jinsi Zawahiri alivyoandaa mpango wa kulipua majengo ya Marekani Septemba 11 mwaka 2001. Hali kadhalika, kinaonyesha namna Zawahiri alivyotekeleza mapango huo akishirikiana na mshirika wake wa karibu bin Laden.

K
wa hili unafikiri ni nini kitakachofuatia??.. ..ni kuanza kumtafuta Al-Zawahiri na kuanza kupiga nchi za watu kwa kisingizio cha kumtafuta, usishangae kama watamuua wakaja na jina jingine la mtu "hatari" na kuendeleza uonevu wao, umepata kitu..........?????
 
mwanaume alietimia hawezi kupanga mashambulizi ya mauaji ya raia popote pale duniani mbaya zaidi waliokufa kwenye ubalozi wa marekani tz walikua ni waislam wewe chunguza majina yale huyu jamaa hakua na lolote bora kaenda mie wala simuungi mkono mtu anaepanga mauaji ya raia!bible inasema ukiua kwa upanga na wewe utakufa kwa upanga
huyu jamaa alikuwa mwanaume
 
Hi thread imejaa vitu muhimu kuhusu ugadi..thanx kwa taarifa mkuu.
 
hili ndo ***** kabisa watalikamata with no time...
 
Kwani kuwaua watu hatari ni uonevu?

mkuu sijakataa wasiuliwe, kama ni hivyo basi watoe list ya watu "hatari" wajulikane sio mchezo wao wa kupokezana kijiti... watu wasiokuwa na hatia waliouliwa Afghanistan eti kisa ni Osama anatafutwa wewe unaona ni sawa?? na waliouliwa Iraq eti ni silaha za maangamizi zinatafutwa ilikuwa sawa?? huo ndio mimi nianouita uonevu!!!!
 
Mbona habari zinatoka upande mmoja tu-western-wenyewe al-qaida hawajasema lolote!. Je tunajiuliza maswali wenyewe kisha tunaji jibu wenyewe?.
 
KUNDI la Al Qaeda, huenda likamteua Ayman al Zawahiri, ambaye ni mzaliwa wa Misri, kuwa kiongozi wake, baada ya kuuawa kwa muuasisi wake, Osama Bin Laden, mapema wiki hii.


Kitabu hicho pia, kinaonyesha jinsi Zawahiri alivyoandaa mpango wa kulipua majengo ya Marekani Septemba 11 mwaka 2001. Hali kadhalika, kinaonyesha namna Zawahiri alivyotekeleza mapango huo akishirikiana na mshirika wake wa karibu bin Laden.

Kwa hiyo Osama Bin Laden alishirikishwa tu katika issue ya September 11?
 
Kumbe Osama kaonewa.....aliyepanga mashambulizi ya Sept 11/2001 ni Zawahiri..! WAMAREKANI ni nouma kwa kumtungia mtu kashfa..na wanaiaminisha dunia uongo kuwa kweli
 
Former Deputy Assistant Secretary of State under three different administrations Steve R. Pieczenik says he is prepared to tell a federal grand jury the name of a top general who told him directly 9/11 was a false flag attack

Top US government insider Dr. Steve R. Pieczenik, a man who held numerous different influential positions under three different Presidents and still works with the Defense Department, shockingly told The Alex Jones Show yesterday that Osama Bin Laden died in 2001 and that he was prepared to testify in front of a grand jury how a top general told him directly that 9/11

habari zaidi nenda kwa website: infowars
 
mkuu sijakataa wasiuliwe, kama ni hivyo basi watoe list ya watu "hatari" wajulikane sio mchezo wao wa kupokezana kijiti... watu wasiokuwa na hatia waliouliwa Afghanistan eti kisa ni Osama anatafutwa wewe unaona ni sawa?? na waliouliwa Iraq eti ni silaha za maangamizi zinatafutwa ilikuwa sawa?? huo ndio mimi nianouita uonevu!!!!
Hiyo list mbona iko mitandaoni siku nyingi tu nenda
FBI — Most Wanted Terrorists
FBI - Ten Most Wanted
 
Calln demselvs "mbwa wa dunia." sifa hii mbaya na ya kjnga inakuzwa pia na wapumbavu wanaowaabudu na kuwaona kama mungu mtu.
Inasiktsha na inauma sana kuona namna bnadam wenzetu wanavoangamizwa kwasababu ya umelo wa taifa moja.
Ninachoamini mimi n kwamba kla lenye mwanzo halkos kuwa na mwsho. Ukowap utawala wa wakatl na wababe warumi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom