Osama bin Laden killed!

Osama bin Laden killed!

Status
Not open for further replies.
hii story ya Osama
ina matata sana na ina maswali mengi..
kila mtu ana choice ya kuamini au kutokuamini yuko hai au la...
lakini ukweli wa mambo anaujua Obama na Secret Service Team yake..
binafsi naamini kweli kaaga dunia, maswali ya lini, vipi, nani kamuua ....
ni magumu yanaumiza kichwa..siku ntaamini yuko hai ni siku ntakapomwona
kwenye TV au katoa yale mavideo yake tena.. (lakini hata hapa yaweza kuwa Mtu fake)
hakuna ajuae ukweli bali wale wanaosema wamemua... dahhhh hili swali linazidi kunijia kichwa
itakuwa vipi kama bado yuko hai na aka prove yuko hai?? Is US gona be the most hated country in the planet???
 
Haya mambo hayo tena!.
Kumbe hapa JF kweli tunao great thinkers!
Obama's no-win decision on bin Laden photos - CNN.com
President Barack Obama faced a no-win decision over whether to release photographs of Osama bin Laden's corpse. In the short term, the president was right not to make public the graphic images, because doing so might inflame public opinion in Muslim-majority countries and actually feed support for al Qaeda's agenda.
In the longer term, however, Obama may be forced to release the photos -- with time, conspiracy theories are likely to mount, and the photos may eventually be leaked anyway. And, of course, visual proof of bin Laden's death would serve as a powerful endpoint in this chapter of American history.
There were compelling arguments on both sides of this issue. Releasing the photos would have mitigated skepticism about bin Laden's death, hopefully snuffing out any nascent conspiracy theories about the late al Qaeda leader's fate. For a president who has already been forced to dignify inane and insulting charges about his origins, the chance to avoid another round of absurdity must have been tempting.
Releasing the photos also may have had the less obvious benefit of deterrence if the images had a visceral effect on other terrorists, militants and rogue leaders. It is entirely possible that seeing the photos could lead such individuals truly to understand that their murderous ways place their lives at risk.

Mengine hayo:
'Deathers' take over where 'birthers' left off - CNN.com
With "birthers" mostly silent, "deathers" are now pushing a new conspiracy theory.
The release of President Obama's birth certificate last week apparently tamped down -- to a large degree -- skeptics who questioned whether he could legally serve as president because they said he wasn't a natural-born citizen. Now, a surprisingly diverse crop of people are questioning whether Osama bin Laden is actually dead.
Some media outlets and bloggers are calling them "deathers."
Their claims follow a wide range: Some believe that the world's most-wanted terrorist was not the man killed Sunday, others think bin Laden is dead but was killed many years ago, and still others believe that the September 11 mastermind is alive -- and secretly being interrogated.
One Fox Business News host is not going quite that far. Judge Andrew Napolitano at one point declared that "Osama bin Laden is dead," but he later seemed unconvinced. Napolitano also questioned the president's authority to kill him.
 
Ni wazi Bin Laden aliamini maeneo aliyokuwepo ni ya jeshi na kwahivyo rada zao zitaweza kuwadetect wamarekani.Chopper walizotumia ni za tofauti,shambulizi la kushtukiza.Yeye alijidhatiti zaidi kuweka migeti kibao,barb wires na kuta ndefu.Kosa hilo,wameingia juu kwa juu saa sita usiku kwa ghafla na kimya kimya,yani in a few minutes wamo chumbani mwake.Naona aliamua kuretire na kula maisha na wake zake na watoto.Hiyo nyumba walishaifanyia mazoezi kwasababu walikuwa na ramani yake.Na walijua ni wapi atakuwa located kutokana na ghrofa yake anayoishi ambayo ni ya tatu na ya mwisho kuwa na kuta ndefu zaidi na hivyo kuonekana wazi ni kwa ajili yake.Kuta futi saba.
 
5 May, 2011, 08.44AM IST,Agencies

Osama captured alive and executed, claims 12-yr-old daughter

ISLAMABAD: Osama bin Laden was unarmed at the time of his killing and his 12-year-old daughter saw her father being shot dead, it was revealed on Wednesday, even as the exact circumstances of the al-Qaida chief's death remained unclear and the White House changed versions.

An Arabic TV station claimed the child had, in fact, said her father was taken prisoner and then shot, in an execution of sorts.

The girl is now in custody with a Yemeni wife of Osama's, an Inter-Services Intelligence ( ISI) official said. Up to 12 women and children who survived the US raid on their villa were now in custody, he said.

The child, reported to be 12 years old, "was the one who confirmed to us that Osama was dead and shot and taken away", said the official.

An Arabic television station went further, saying, "a source in Pakistani security quoted the daughter of Osama bin Laden that the leader of al-Qaida was not killed inside his house, but had been arrested and was killed later".

Four bodies were retrieved from the daring covert attack, including one of bin Laden's sons, said the official, speaking on condition of anonymity.

Up to three women and nine children, including the young Yemeni woman who was shot in the leg and a daughter of the Saudi-born mastermind, were in detention, he said.

"There are a lot of questions we want to ask them," another intelligence official said.
Source:http://economictimes.indiatimes.com...ms-12-yr-old-daughter/articleshow/8165559.cms
 
MAKACHERO wa Marekani wamesema walivamia nyumbani kwa Osama bin Laden na kumuua baada ya kunasa mawasiliano ya simu yaliyokuwa yakifanywa baina ya mmoja wa wafanyakazi wa kiongozi huyo wa kundi la Al Qaeda na jamaa zake wa karibu.Makachero hao walifichua siri hiyo Jumatatu na kueleza jinsi mawasiliano hayo yalivyowawezesha kumfuata mfanyakazi huyo hadi alikokuwa amejificha Osama.Kwa mujibu wa makachero hao, Osama hakumwamini mtu yeyote kwenye jengo hilo. Awe kamanda wa ngazi za juu au walinzi wake, lakini aliwaamini wafanyakazi wake wawili tu ambao aliwatumia kupeleka ujumbe nje ya makazi hayo.

"Kwenye jela ya kisiri ya CIA Ulaya Mashariki, kiongozi namba tatu wa Al Qaeda, Khalid Sheikh Mohammed, aliwataja wafanyakazi hao wa karibu wa bin Laden," mmoja wa makachero wanne wa zamani wa Marekani alisema.
Kwa mujibu wa kachero huyo, mtuhumiwa huyo wa ugaidi aliwaambia makachero hao kuwa iwapo wangempata mfanyakazi mmoja wa Osama, angewawezesha kumkamata Osama Bin Laden.

Mchakato wa kumpata Osama
Kwa mujibu wa kachero huyo wa zamani wa Marekani, iliwachukua makachero wa nchi hiyo miaka kadhaa kutambua jina la mfanyakazi huyo, ambalo hata baada ya mauaji ya Osama bado halijajulikana.
Alisema ilikuwa ni amri ya bin Laden kuwataka wafanyakazi wake hao kutotumia simu au kompyuta wakiwa karibu naye.

"Lakini katikati ya mwaka jana, mfanyakazi huyo alikuwa na mazungumzo ya simu na mtu ambaye alikuwa akifuatiliwa kwa karibu na majasusi wa Marekani," alisema ofisa mwingine wa makachero wa Marekani ambaye hakutaka kutajwa.

Alisema makachero hao walianza kumfuatilia mfanyakazi huyo hadi maficho ya Osama.
Agosti mwaka jana 2010, mfanyakazi huyo bila kujua alielekeza makachero hadi makazi katika jiji la Abbotabad, Kaskazini Mashariki mwa Pakistan na ambapo walibaini kuwa nyumba ya Osama ilikuwa imezungukwa ukuta wenye urefu wa futi 18 na kuwekwa seng'enge juu yake.

Kwa mujibu wa habari hizo, tangu wakati huo makachero wa Marekani waliogopa kuvamia jumba hilo kwa hisia kwamba, Osama angekuwa amelindwa na walinzi wenye silaha kali. Katika uchunguzi wao walibaini kuwa hakukuwa na mtu aliyekuwa akiingia wala kutoka ndani na kwamba hakukuwa na nyaya za simu wala intaneti zilizoonekana kutoka nje ya makazi hayo.

Habari hizo zinaendelea kudai kuwa CIA baadaye iliamini Osama aliishi katika makazi wazi, kwenye jengo lililojengwa kwa namna ambayo ni vigumu kumtambua kwa kuwa hakuna yeyote anaweza kuingia ndani bila kupitia lango kuu lenye ulinzi mkali.

Makazi ya Osama
Ilipofika katikati ya Februari mwaka huu, makachero hao wa Marekani walijiridhisha kwamba Osama yumo ndani ya jengo hilo na hivyo kumjulisha Rais Barack Obama ili aweze kuchukua hatua zaidi.
Kwa mujibu wa sheria za Marekani, ni rais pekee anayeweza kuidhinisha majeshi ya nchi hiyo kufanya uvamizi katika eneo lolote baada ya kushaurina na wakuu wa masuala ya usalama.

Lakini kutokana na nyumba hiyo kuwa kwenye makazi ya watu Obama alisita kutoa amri ya kuvamia haraka kwani aliamini kuwa kufanya hivyo halafu usimkute Osama, kungeibua mzozo wa kidiplomasia.

Hata hivyo, Jumapili wiki hii baada ya kujiridhisha kwamba wanaweza kufanya uvamizi huo bila athari kwa raia, Rais Obama aliamuru helikopta mbili zitoke Jalalabad, Mashariki mwa Afghanistan na kuingia kwenye anga la Pakistan kwa kutumia teknolojia ya kisasa ili Pakistan isizitambue.Helikopta hizo ziliwaingiza makachero hao kwenye makazi hayo ya Osama, lakini moja ikaanguka.

Mtandao wa WikiLeaks
Mtandao huo nao umeeleza kuwa aliyewezesha Marekani kujua alikojificha Osama, ni mmoja wa wahudumu wake ambaye alipata mafunzo ya kigaidi ili kutekeleza tukio la mashambulizi ya Septemba 11, 2001 nchini Marekani.
Abu Faraji al Libi ambaye aliwahi kufanya kazi karibu na Osama, anadaiwa kutoa taarifa muhimu kwa Shirika la Kijasusi la Kimataifa la Marekani (CIA) zinazomhusu mtuhumiwa huyo wa kigaidi duniani ambaye aliisumbua Marekani kwa zaidi ya miaka 10.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, CIA iliweza kumfahamu Abu baada ya kupata taarifa zake kupitia mtuhumiwa mwingine wa kigaidi ambaye alikuwa katika gereza la Guatanamo, Khalid Sheikh Mohammed.
Mahabusu mwingine wa Guantanamo, Muhammad Mani al-Qahtani aliiambia CIA kuwa Abu ndiye aliyempa mafunzo ya kompyuta katika mpango wa kutekeleza shambulio la kigaidi la Septemba 11, 2001.

Baada ya upelelezi huo, inadaiwa kuwa Abu aliorodheshwa kwenye kundi la watu muhimu mwenye kujua mambo yahusuyo matukio ya kigaidi ya kulipua ili kusababisha mauaji.

Mtanzania mpishi wa Osama
Mtanzania Ahmed Khalfan Ghailan mwenye asili ya Zanzibar, ndiye aliyekuwa mpishi wa aliyekuwa kiongozi kundi la Al-Qaeda, Osama Bin Laden.Ghailan ambaye sasa anatumikia kifungo cha maisha katika gereza la Marekani la Guantanamo lililopo nchini Cuba, kutokana na kuhusika katika kulipua ubalozi wa Marekani nchini Kenya na Tanzania na kusababisha vifo vya watu 257 na kuacha majeruhi 4000, alizaliwa mwaka 1974 visiwani Zanzibar.

Ghailan alikatisha masomo yake mwaka 1996 na kwenda jijini Dar es Salaam kuuza mitumba kabla ya kuanza kujihusisha na masuala ya ugaidi. Alikuwa akisafirisha foronya za magodoro kutoka Dar es Salaam kwenda Mombasa, nchini Kenya.

Alikuwa akifanya biashara na mwezake aliyefahamika kwa jina la Suleimani Abdallah ambaye alikuwa rafiki yake wa karibu. Baadaye aliamua kusafiri kwenda nchini Somalia, Dubai na Uarabuni kufanya biashara ya kuuza samaki.

Lakini baada ya biashara hiyo kuwa ngumu kutokana na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha, marafiki hao waliamua kurudi Mombasa, Kenya ambapo mwaka 1997 na mwanzoni mwa 1998 marafiki hao waliachana ambapo Ghailani alianza kufanya biashara ya sabuni akitokea Arusha na kuzipeleka Dar es Salaam.

Siku moja akiwa Arusha akipakiza sabuni kutoka kwenye duka la Hussein Abbe, uligundulika kuwa mzigo aliopakia haukuwa wa kawaida. Alikuwa anafanya safari zake mara kwa mara, lakini, siku hiyo aligundua kuwa alichokuwa amebeba siku ile haikuwa sabuni, bali ni malighafi yaliyotumika katika ulipuaji wa mabomu, katika balozi za Marekani.

1998 alielekea nchini Kenya na baadaye kwenda Pakistan na Afghanistan ambako alifanya mazoezi ya ugaidi aliyoyatumia kuulipua ubalozi wa Marekani mjini Nairobi, Kenya na Dar es Salaam.
Mwaka 1998 na 1999 Ghailani alifundishwa kwa miezi mitano masuala ya ugaidi na mwalimu wake Abdi Al Hakam Al Yamani. Pia alifundishwa lugha ya Kiarabu na akakijua vizuri kwani awali alikuwa akifahamu kuzungumza Kiingereza.

Baada ya kumaliza mafunzo hayo, Ghailan alienda Kandahar kati ya mwaka 1999 na 2001 baada ya kughushi hati ya kusafiria akionyesha kuwa ni Mujahideen na familia yake wanarudi nyumbani kwao Kandahar na baadaye alirudi tena nchini Kenya.

Taaluma ya kughushi
Baada ya kufanikisha azma yake ya ulipuaji wa bomu alitoka Kenya kuelekea nchini Afghaniastan kwa ajili ya mafunzo katika kambi ya Al Faruq. Kati ya 1999 na 2001 alikuwa mpishi wa kundi la Osama Bin Laden na baadaye alighushi vyeti na barua akawa anafanya kazi na Khalid Bin Attash na Ammar Al Baluchi.

Ahmed Abdul Aziz alimtambulisha kama mlinzi wake, alikuwa anawahudumia wenzake akiwa kama mwanafunzi, lakini baadaye alikataa kufanya kazi ya ulinzi kwa sababu walinzi walitumia muda wao mwingi kufanya kazi, huku wakikosa uhuru wa kufanya mambo mengine.

Wakati akiendelea na kazi yake hiyo ya upishi wa chakula katikati ya mwaka 2001 na wakati huo huo akitambulika kama mlinzi alipata mafunzo ya kughushi nyaraka.Alijifunza kughushi nyaraka kuanzia mwaka 2001 kutoka kwa mwalimu wake aliyefahamika kwa jina la Abu Yahya wa Afghanistan. Ujuzi huo aliutumia kughusshi nyaraka ambazo alizitumia kusafiri kutoka nchi moja kwenda nyingine akiutumikia mtandao wa Al Qaeda.

Anasema alifundishwa na mwalimu wake huyo namna ya kupiga picha na kuweka katika hati ya kusafiria, stempu, namna ya kutengeneza kitambulisho, leseni ya udereva, na namna ya kutumia Adobe Photoshop.
Ghailan aliendelea kuwa mwanachama wa Al Qaeda kwa sababu alikuwa yeye ndiye mtu aliyetumika kufoji nyaraka mbalimbali za kundi hilo.

Wakati bado yupo nchini Pakistani aliweza kuwasaidia wanachama wa kundi la Al Qaeda kuwagushia vyeti vya kuzaliwa na hati za kusafiria ambao wengi walikuwa wakisafiri na familia zao bila ya wasiwasi.

Osama alivyoishi na majirani
Katika hatua nyingine wakazi wa mji mdogo wa Abbottabad wanaoishi jirani na nyumba alimokuwa akiishi Osama bin Laden, wamesema katika nyumba hiyo kulikuwa na watu wazima 30 na watoto kadhaa.

Walisema watu hao walionyesha ustarabu mkubwa kwa majirani, lakini hawakupenda kuzoeleka.Miongoni mwa matendo waliyoonyesha kuwa ya kistaarabu yaliyofanywa na familia hiyo ya Osama ni kushiriki katika mazishi na kutoa msaada wa lifti kwa majirani waliokuwa wanaenda mjini kupata mahitaji.

Mmoja wa majirani aliyesema ana ufahamu mdogo kuhusu watu waliokuwa wakiishi kwenye nyumba hiyo, ingawa walikuwa majirani. Alisema ni wanaume wawili tu waliokuwa wanatoka kwenye nyumba hiyo na kuwakaribisha majirani.

Wanaume hao walijitambulisha kwao kuwa ni Tariq na Arshad Khan na walijieleza kuwa ni wenyeji wa eneo la Kaskazini Mashariki mwa Pakistani.Arshad alijitambulisha kuwa ndiye mwenye umri mkubwa kwenye familia hizo na alikuwa akizungumza lugha mchanganyiko zikiwapo za Kipashto na Kiurdu, ambazo zimezoeleka kwenye eneo hilo la Kaskazini Magharibi mwa Pakistani.

Khurshid Bibi (70), ambaye ni mkazi wa muda mrefu katika eneo hilo alisema kuwa ni nadra kuwaona wakazi wa nyumba hiyo mitaani.Lakini alisema anakumbuka kuwa mmoja wa wanaume waliokuwa wanaishi kwenye nyumba hiyo, aliwahi kumpa lifti wakati anaenda sokoni wakati mvua ikiwa inanyesha.

Jirani mwingine alieleza kwamba aliwahi kuona wanaume wawili kutoka nyumba alimoishi Osama wakishiriki kwenye msiba uliotokea eneo hilo.Walibaini pia kuwa kwenye nyumba hiyo ziliishi familia nyingi na hata wakati maofisa wa afya walipokuwa wanatoa chanjo ya polio kwa watoto, walishiriki.

Walisema siku hiyo ya chanjo ya polio ndiyo mtu nje ya familia hizo, aliruhusiwa kuingia kwenye jengo hilo.
Inaelezwa kuwa ofisa afya alipofika katika eneo hilo akitoa chanjo nyumba kwa nyumba, aliruhusiwa kuingia na kutoa huduma kwa watoto kwenye nyumba hiyo baada ya kueleza umuhimu wa huduma hiyo.
Inaelezwa kuwa wanaume waliokuwa ndani ya wigo walimruhusu ofisa huyo na alipoingia alitoa chanjo kwa watoto 23.
 
Du, magaidi ni hatari, wanaweza kujigeuza kama mama yako mzazi hadi sauti
 
KUNDI la Al Qaeda, huenda likamteua Ayman al Zawahiri, ambaye ni mzaliwa wa Misri, kuwa kiongozi wake, baada ya kuuawa kwa muuasisi wake, Osama Bin Laden, mapema wiki hii.

Maofisa wa usalama wa ngazi za juu nchini Marekani wamesema ingawa hakuna mambo mengi yanayojulikana kuhusu Zawahiri, lakini ndiye mtu aliyekuwa wa karibu na bin Laden.

Imeelezwa kuwa mtu huyo ndiye aliyekuwa akipanga mashambulizi kadhaa dhidi ya Marekani.Kutajwa kwa Zawahiri katika kumrithiri bin Ladeni, kumetokana na watu kumwelezea kuwa ni mtu jasiri na anayeweza kutetea kile anachokiamini kuwa ni haki.

Lakini wanamtandao wengi wa Al-Qaeda, hawamwamini kutokana na tabia yake ya kuamini kuwa anachofanya yeye ndicho sahihi zaidi na kusimamia imani hiyo bila kukubali kubadilika.

Zawahiri ndiye aliyekuwa anaongoza Kundi la Al-Qaeda, katika kuishambulia Marekani kwa akitumia silaha nzito za maangamizi.Makachero sita wanaopambana na ugaidi na baadhi ya watu wanaomfahamu Zawahiri, walikiambia Kituo cha Televisheni cha Al Jazeera kuwa kwa miaka mitatu sasa, Zawahiri amekuwa kimya, akiendesha operesheni za chini kwa chini.

"Sasa amekuwa kimya akiendesha operesheni za Mtandao wa Al Qaeda kisayansi na kwa kutumia utalaamu wa hali ya juu," mmoja wa maafisa hao alisema.Mwaka 2008, Zawahiri aliandika kitabu kilichokuwa kinaelezea historia na umahiri wake katika kutumia sila nzito za mabomu aina ya nuclear na mtazamo wenye misingi ya dini wa Mtandao wa Al-Qaeda, kuhusu kuua watu wengi kadiri iwezekanavyo.

Kitabu hicho pia, kinaonyesha jinsi Zawahiri alivyoandaa mpango wa kulipua majengo ya Marekani Septemba 11 mwaka 2001. Hali kadhalika, kinaonyesha namna Zawahiri alivyotekeleza mapango huo akishirikiana na mshirika wake wa karibu bin Laden.

Rolf Mowatt-Larssen, kiongozi wa zamani wa makachero wa Marekani wanaopambana na ugaidi wa silaha nzito, ni mmoja wa watu waliozungumzia uwezekano wa Zawahiri, kuongoza Kundi la Al-Qaeda, baada ya kifo cha bin Laden.
"Zawahiri yuko makini kuliko Osama na tunaamini kuwa ndiye atakayeongoza kundi hilo katika mapambano ya baadaye," alisema," Mowatt-Larrsen mmoja wa maafisa katika Chuo Kikuu cha Harvard.

Hata hivyo Michael Scheur, ambaye aliongoza makachero wa Kikundi cha Al-Qaeda mwaka 1996 hadi 1999 na ambaye pia ni mtunzi wa kitabu kipya cha Bin Laden, amesema Zawahiri ataligawa Kundi la Al-Qaeda, kama atachaguliwa kuliongoza.

"Siamini kuwa Zawahiri anaweza kuongoza kundi hilo kwa muda mrefu. Ni mtu anayetabirika, mkali na ni mtu anayependa kujitambulisha zaidi kuwa ni Mmisri. Tabia hizi zitafanya ashindwe kuwa kiongozi mzuri," alisema Scheuer.

Mwanasheria wa Misri Montasser el-Zayat, ambaye Zawahiri aliwahi kuwa mteja wake, alisema mwanaharakati huyo ni miongoni mwa watu waliokamatwa na kuteswa kati ya mwaka 1980 na mwaka 1990 chini ya uongozi wa Rais Hosni Mubarack, aliyelazimishwa kujiuzulu mwezi uliopita.El-Zayat alimwandikia kitabu mwanaharakati huyo kinachosomeka

"Amyan al-Zawahiri as I Knew Him, ikiamaanisha jinsi ninavyomfanya Amyan al-Zawahiri.Katika mazungumzo yake ya hivi karibuni nchini Misri, el-Zayat alisema "Zawahiri ni mtu mkorofi. Siku zote anafikiri kuwa yeye pekee ndiye anaweza kuwa sahihi na huu ndio udhaifu wake."

Kati ya miaka ya 1980 na mwaka 1990, Zawahiri alikuwa akitafutwa na utawala wa Mubarak kwa tuhuma za kuandaa matukio ya ugaidi yenye lengo la kuvuruga sekta ya utalii nchini humo.Lakini kuanzia mwaka 1993, Zawahiri alianza kujiunga na kundi la bin Laden nchini Sudan wakati kiongozi huyo alipowataka Waislamu duniani, kuungana na kutetea maslahi yao dhidi ya Marekani.

Bin Laden aliita namna hiyo ya kudai haki kuwa vita ya jihadi au vita vitakatifu dhidi ya Marekani.
 
MSIMAMO wa Rais Barack Obama wa Marekani, kuzuia kuonyeshwa hadharani kwa picha za mwili wa Kiongozi wa Al Qaeda, Osama bin Laden, aliyeuawa mapema wiki hii nchini Paskatani, umesukumwa na sababu nane, imeelezwa.

Jana, Gazeti la The Monitor la Uingereza, liliorodhesha sababu hizo zilizoelezwa kuwa zimetokana na uchunguzi wa timu ya waandishi wake wa habari.

Uchunguzi huo unafautia msimamo wa Obama wa kutorohusu picha hizo, kuonyeshwa hadharani kama inavyoshinikizwa na watu wengi duniani .
Kwa mujibu wa gazati hilo, sababu hizo pamoja na kuhofia kuchochea hasira za waumini wa dini ya Kiislamu duniani, kuwachukia Wamarekani, kwa sababu hawako radhi kuona sura ya maiti.

Sababu nyingine ni sheria za adhabu za vifo nchini Marekani, inakataza uonyeshaji wa picha za watu waliouawa katika kutekeleza adhabu.

Pia imeelezwa kuwa jaribio lolote la kuonyesha picha hizo hadharani, litachochea zaidi vitendo vya ugaidi na baada ya kuonyesha kwa vitendo vya kikatili wanavyowafanyiwa mateka wa mtandao wa kigaidi.

Kulingana na gazeti hilo la Uingereza, sababu nyingine ya Marekani kukataa kuonyesha picha ni wafuasi wengi wa mtandao wa Al Qaeda, kukataa kuambiwa ukweli kuwa bin Laden amekufa.

Lakini pia uonyeshaji wa picha ya mtu aliyeuawa, unakiuka maadili yanayokataza watoto kuonyeshwa picha za aina hiyo.

The Monitor ilitaja sababu nyingine kuwa mwili wa Osama hauwezi kufananishwa na bidhaa ama kitu muhimu cha maonyesho. Jambo la msingi katika tukio hilo ni tabia yake mbaya ambayo ilikuwa ni ya kuua watu wasio na hatia ili kuridhisha nafsi ya chuki zake dhidi ya watu wengine.

Sababu ya saba, imeleezwa kuwa ni Marekanikuweka nguvu zaidi katika malengo ya kuudhofisha watu wengine wenye mikakati kama ya Osama.

Hali kadhalika Wamarekani kuamini kuwa kuna kasi kubwa ya watu katika nchi za Kiarabu, kumchukia bin Laden kutokana na tabia yake na kwa hiyo hakuna sababu ya kuendelea kuwaonyesha picha yake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom