Osama bin Laden killed!

Osama bin Laden killed!

Status
Not open for further replies.
Lakini pia jamani hata kama ni kweli utata ni mkubwa kuliko ukweli wenyewe hiyo nyumba yenyewe imekaa tofauti na zote hiyo sehemu mtu anayeelezwa kuwa na akili na gaidi mkubwa kukaa kwenye nyumba kama hiyo ambayo iko visible na most likely kuwa suspected bila kujitengenezea kitu kama njia za chini kwa chini za kutorokea kuelekea hiyo milima ya Afganistani inawezekana kweli? Michoro ya nyumba ni mizuri kuliko nyumba yenyewe na wala sioni kuwa ni complex fulani na hizo features wanazoeleza kwa mtu gaidi ya std ya Osama sijui kama angeweza kukaa humo. Any way acha jogoo wa dunia wa wikie vitetea vyao si wengine twaishi ulimwengu wetu wenyewe na ufalme wetu si wa dunia yao.

Nafikiri mungu hawezi kutunyima vyote, hiki ndio kipaji pekee tulichonacho Watanzania. BISHANA MPAKA UFE. Usichokijuwa tu ni kwamba alikuwa anahifadhiwa na serikali ya Pakistan, kwa sababu ya upumbavu ule ule wa huyu ni mwislamu mwenzetu.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Shirikisha ubongo wako japo kidogo, Wamarekani wanacho kila kitu, ikiwemo live coverage video ya tukio zima la mauwaji ya huyu Shetani Osama, lakini wewe huwezi kuwapangia CIA ni muda gani wazitoe hizo solid evidence, kwa sababu kila wanachofanya wao wanaangalia maslahi ya Marekani kwanza, na sio kuwaridhisha nyinyi watu wa kwenye vijiwe vya ubishi wa kwenye kahawa.
Hata walipotaka kwenda kuvamia Iraq pia shetani bush na watu wake walitoa solid evidence, kuwa jamaa anamiliki siraha za maangamizi. Na kweli tuliziona, tena nyingi kweli kweli.
 
Nafikiri mungu hawezi kutunyima vyote, hiki ndio kipaji pekee tulichonacho Watanzania. BISHANA MPAKA UFE. Usichokijuwa tu ni kwamba alikuwa anahifadhiwa na serikali ya Pakistan, kwa sababu ya upumbavu ule ule wa huyu ni mwislamu mwenzetu.

Kama ndivyo basi siwangetengeneza nyumba tatu nne randomly zinazofanana kiaina ma hata status ili kupotezea? Vipi wampeleke kwenye sehemu ambayo hata mm nikiwa mgeni hapo ntajua huyo mtu anaumuhimu fulani huo mtaa na lazima nitapenda kuchimba historia yake? Yaani Osama asumbue dunia nzima miaka yote ashindwe kuwa na akili ya kutengeneza cover na escape roots zinazoeleweka? I should then doubt my common sense!
 
Hata walipotaka kwenda kuvamia Iraq pia shetani bush na watu wake walitoa solid evidence, kuwa jamaa anamiliki siraha za maangamizi. Na kweli tuliziona, tena nyingi kweli kweli.

Mtaongea sana mpaka povu liwatoke, lakini huyu gaidi muhimili wa uovu ameshauwawa PERIOD. ninachosikitika tu ni kwa nini hawakumchemsha supu? maana ningechelewa kutafuna nyama yake basi hata mchuzi tu nilikuwa nautaka nishushie na ndizi bukoba. na kuanzia sasa hautasikia tena misikiti ikitekwa.
 
After 10 yrs...thats a very long manhunt,but it bore fruit,america has killed an old man, was he in charge still???? maybe not, is al quaeda dead???? maybe not.so let us not be complacent. tukae chonjo!
 
Labda mkuu ungenisaidia mimi mbumbumbu kunijurisha ni kwa nini Pakistan inajieleza kwa Marekani kwamba haikuwa inajuwa kama Osama amejificha Pakistan? hivi haujuwi kwamba baadhi ya Intelijensi ya Pakistani ilikuwa inahusika kumpa hifadhi Osama? na je kama wewe unaishi Marekani haujasikia kwamba CONGRESS wanaishauri serikali yao kwamba, kama ikithibitika Pakistan ilikuwa inajuwa kwamba Osama yupo Pakistan basi Marekani ikate msaada wa mabillioni ya dollar kwa Pakistan? hivi mnatumia akili zenu kufikiri vizuri kweli?

Uko sawa mkuu
 
Hata walipotaka kwenda kuvamia Iraq pia shetani bush na watu wake walitoa solid evidence, kuwa jamaa anamiliki siraha za maangamizi. Na kweli tuliziona, tena nyingi kweli kweli.

Hebu niambie ni zipi hizo nyingi (Japo moja) unazosema walizitoa kama solid evidence (nasisitiza Solid evidence). Taja moja tuichambue kwa kina.
 
Kama ndivyo basi siwangetengeneza nyumba tatu nne randomly zinazofanana kiaina ma hata status ili kupotezea? Vipi wampeleke kwenye sehemu ambayo hata mm nikiwa mgeni hapo ntajua huyo mtu anaumuhimu fulani huo mtaa na lazima nitapenda kuchimba historia yake? Yaani Osama asumbue dunia nzima miaka yote ashindwe kuwa na akili ya kutengeneza cover na escape roots zinazoeleweka? I should then doubt my common sense!
Mkuu mbona sie Tanzania tulimuifadhi Laurent Kabila, Wamba Dia Wamba kweupe na hatukutengeneza nyumba mbili mbili na serikali ya Mobutu haikuwashika, kwa kifupi Pakistan wameachwa uchi kwenye hii issue hawana pa kutokea miaka yote Hamid Karzai alikuwa anasema Osama yuko Pakistan, lakini serikali ikawa inakana wee sasa amekutwa kajificha karibia na shule yao kubwa ya kijeshi.

Mkuu kusema hakuwa na escape route, angalia jinsi Carlos alivyoshikwa au Savimbi siku zako zikifika zinakuwa zimefika tu.
 
Hii issue inakokwenda kutamu, McDonough anasema kuwa watu waliokuwa ndani ya nyumba ya Osama wako mikononi mwa serikali ya Pakistan.
 
Hebu niambie ni zipi hizo nyingi (Japo moja) unazosema walizitoa kama solid evidence (nasisitiza Solid evidence). Taja moja tuichambue kwa kina.
Aaaaah Mkuu sasa mambo gani hayo tena, kwani wewe ukuona michoro iliyo onyeshwa baraza la usalama la umoja wa mataifa?

Hotuba za George Bush, Rumsfeld na wengine wakitangaza ilo jambo... au ukumbuki?
 
3D said:
Nimekuuliza swali katika post namba 1121 hujanijibu. Nimesubiri kwa zaidi ya nusu saa. Sasa naingia usingizini. Ila ushauri wangu kwako, weka hisia (emotions) pembeni, leta hoja.
Hizo Hisia (emotions) zinatoka wapi sasa...!

Sasa wewe na G.W.Bush nani mkweli?
 
Kuna hii hapa nyingine:



Walisema wakaaminiwa, waliopinga wakaonekana siasa kali Mujahidina.
 
Last edited by a moderator:
Aaaaah Mkuu sasa mambo gani hayo tena, kwani wewe ukuona michoro iliyo onyeshwa baraza la usalama la umoja wa mataifa?

Hotuba za George Bush, Rumsfeld na wengine wakitangaza ilo jambo... au ukumbuki?

Nakumbuka sana na ndiyo maana nimekuuliza ni ipi unayozungumzia. Hakuna hata moja ambayo ilikuwa ni nzito kiushahidi. Ngoja nikukumbushe:

  1. Kwanza kumbuka tuhuma ilikuwa ni Iraq kumiliki Weapons of Mass Destruction (WMD - Sialaha za maangamizi ya halaiki) hivyo shinikizo lilipokuwa kubwa wachunguzi chini ya Hans Blix walikwenda kuchunguza. Baada ya muda mrefu kukawa hakuna ushahidi wa wazi, kilichokuwa kinawapa visingizio (ushahidi dhaifu) ni suala la Saddam kuwazuia kuingia baadhi ya maeneo (Nadhani yeye Saddam alikuwa anachukulia ni siri za kawaida za Taifa hivyo huwezi kumwonesha mgeni kila kitu), hili lilimpoonza. Ilifikia kukawa na mashinikizo Makubwa.
  2. Kilichokuja kuonekana kwa haraka ni Makombora ya Alsamoud II ambayo yalidaiwa kuwa na masafa marefu zaidi ya ilivyopangiwa Iraq kwa mujibu wa vikwazo vya silaha. Saddam aliridhia yabomolewe (dismantling).
  3. Shinikizo lilizidi baada ya Marekani "kudai" kupata habari kuwa kuna wakati Abu Moussab Al-Zarqawi alikwenda kutibiwa Iraq. Huu ulikuwa ushahidi wa "taarifa" za kiintelijensia za CIA ambazo balozi wa Iraq UN alikuwa akizikanusha. Hivyo ilileta utata barazani UN wamsikilize nani.
  4. Nchi zingine zilikataa madai ya Marekani. Marekani ikashinikizwa kuleta ushahidi. Akapewa kazi ya kupresent Gen Collin Powell (Secretary of State).
  5. Collin akaja na picha za satellite na michoro (illustrations) za kuonesha possession ya mobile laboratories (Masemitrella (kiswahili!!)) yanayotumika kutengenezea kemikali za sumu (Niliitazama presentation live. Powell alipoanza kuongea aliwachekesha wajumbe kwa kusema hata yeye si mtaalamu ya kutafsiri picha za satellite, aliongea kama masihara. Nadhani resolution ya UN ambayo Iraq ilikuwa inadaiwa kuvunja ilikuwa ni 1444 (nadhani (muda umepita sana!)).
  6. Wajumbe hawakuridhika kabisa isipokuwa England na Hispania.
  7. Marrekani ikatangaza bado inaamini Iraq inamiliki WMDs hivyo ikaema itakwenda kupiga Iraq with or without allies. Blair akapambana kweli hadi akapata ruhusa England kusaidia.
  8. Kwa taarifa za dharura zilizoifikia Ikulu ya Marekani kuwa Saddam ana kikao katika moja ya majengo ya Serikali, Rais Bush akatoa ruhusa rasmi na kombora la kwanza lilikuwa ni Cruise Missile toka baharini, Saddam aliescape. Hapo vita ilkuwa imeanza.
  9. Waislam Tanzania waliitisha mkutano Jangwani, BBC iliwatangaza wakilia kwa sauti za juu. Uganda watu walidai kujitolea kuandaa "human shield" kumlinda Saddam, sijui waliishia wapi. Canada, Ujerumani, Arabuni maandamano yalifanyika kupinga vita. Marekani maandamo yalifanyika kupinga vita. Nakumbuka maneno ya mwanamuziki Sheryl Crow (ameimba nyimbo Soak up the sun na The first cut is the deepest) alisema, "Get the Hell outta here!!" akimponda bush.
  10. Kabla ya Hapa Papa Yohani Paulo II alipinga vita na aliongea na Blair na kumwambia hivyo. Hata Tareq Aziz (nadhani alikuwa mkristo huyu) sikumbuki cheo chake Iraq nadhani alikuwa Waziri Mkuu maana Al Sahaf alikuwa mambo ya nje kama sijasahau. Baada ya kama mwezi Saddam alkuwa kaondolewa madarakani.
Hayo ndo nayakumbuka kwa haraka haraka. Nachotaka kusema Marekani haikuwa na ushahidi mzito sana. Kabla, wakati na baada ya vita. Ila ilikuwa imeshaingia katika hasira ya kwamba Saddam lazima atoke. Hasira hii ndiyo itayomwondoa Gaddhafi. Kwani XPaster Gaddaffi kaoneshwa ushahidi upi mzito sana. Ushahidi ungekuwepo usingesikia lugha za "Kumzuia asiue raia wasio na hatia." Aidha usingesikia habari ya "No Fly Zone" angepigwa fasta maana Libya haiwezi kusimama kwa US hata kwa siku 30.

Ukweli ndiyo huo. Nalala sasa. Well naweza kuvumilia hadi saa nane and not more than that.
 
Hizo Hisia (emotions) zinatoka wapi sasa...!

Sasa wewe na G.W.Bush nani mkweli?

Well, nilikuwa sijaiona hii. Bush likely ni mkweli na mimi mkweli. Ukweli wa Bush ni kusema ukweli juu ya ukweli ambao ni "uongo" alioaminishwa kuwa ni ukweli. Yeye kama Rais aliongea yale aliyotaarifiwa. Suala la kumpotosha Rais lilichangia Ramsfeld, Collin na bosi wa CIA kuachia ngazi. Hata Paul Bremer aliachia ngazi. Hivyo Bush likely alikuwa mkweli kwa kuusema "uongo" alioaminishwa kuwa ni ukweli, yeye si mpelelezi. Mimi ni mkweli kwa kuwa nasema nachoamini ni ukweli, kama ni uongo sijui. Nobel Laureate Niels Bohr (we ni mwanasayansi unamfahamu) alisema, "Uongo hutenguliwa na ukweli na ukweli hutenguliwa na ukweli mkubwa zaidi."
 
Well, nilikuwa sijaiona hii. Bush likely ni mkweli na mimi mkweli. Ukweli wa Bush ni kusema ukweli juu ya ukweli ambao ni "uongo" alioaminishwa kuwa ni ukweli. Yeye kama Rais aliongea yale aliyotaarifiwa. Suala la kumpotosha Rais lilichangia Ramsfeld, Collin na bosi wa CIA kuachia ngazi. Hata Paul Bremer aliachia ngazi. Hivyo Bush likely alikuwa mkweli kwa kuusema "uongo" alioaminishwa kuwa ni ukweli, yeye si mpelelezi. Mimi ni mkweli kwa kuwa nasema nachoamini ni ukweli, kama ni uongo sijui. Nobel Laureate Niels Bohr (we ni mwanasayansi unamfahamu) alisema, "Uongo hutenguliwa na ukweli na ukweli hutenguliwa na ukweli mkubwa zaidi."
Ungenisoma vizuri tangia mwanzo, tena kwa kurudia rudia nilichokiandika ungekwisha nielewa mapema. Namaanisha nini!

Haya kaka usiku mwema.
 
White house wamesema watatoa picha watazionesha
Kuna picha nyingine (chini) inazungukua kwenye mitandao, ukiiangalia kwa haraka haraka unajua ni fake..
4044390osama.jpg
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom