Nimefuatilia uzi wako
Naona una mapungufu fulani yanayokufanya uonekane kama tapeli japo yawezekana ukawa sio tapeli
labda nikukumbushe tu kwakuwa wewe ni mgeni humu jf hapo nyuma kulikuwa na mtu alikuja na staili kama yako alikuwa anaitwa
kevin isaya yeye alikuwa anachukua 10%ya hela yote then mzigo ukija unammalizia unachukua mzigo wako na alikuwa na ofisi dar na watu wachache wa kwanza walipata mizigo yao akajijengea uaminifu baada ya hapo walioorder raundi ya pili wote walipigwa na ofisi walikuta imefungwa
Ushauri wangu jaribu kutafuta mtaji ununue na kuleta mzigo kwa hela yako pia kama unashindwa jaribu kuweka dhamana ambapo mteja atakuwa na uhakika wa pesa yake kama hatatapeliwa
Usione watu wanalalamika sana wengi wamelizwa humu ndani