Oneni utata jamani?

ndume

Member
Jan 10, 2011
53
2
Baraza la kiswahili lilitumi vigezo vipi kuita majina yafuatayo kama ifuatavyo:
mnyama mbwa badala ya kuita m'mbwa.
Mbu badala ya kuita m'mbu.
Nge badala ya kuita n'nge. Vilevile hata neno nje badala ya kuita n'nje.
Naomba msaada kuhusu hizi ni kwa nini waliita hivi?
 
acha tusubiri wataalam wakuje kumwaga elimu.

lakini kwanini na wewe unaitwa ndume na sio n'ndume?
 
Kiswahili kuandika na kutamka ni tofauti kama kilivyo kiIngereza. Ukitaka kutatuwa tatizo la kuandika na kutamka tumia herufi za kiarabu. Kiarabu kina vitamshi vinavyofanya kila neno ulisome kama linavyotamkwa hata kama ndio mara ya kwanza kulisoma hilo neno.

Kumbuka kuwa historically kiswahili kilikuwa kinaandikwa kwa herufi za kiarabu na si za kilatini kama tufanyavyo sasa. Kuna baadhi ya wazee wa kiSwahili mpaka leo hutumiana baruwa za kiswahili kwa maandishi ya kiarabu.
 
acha tusubiri wataalam wakuje kumwaga elimu.

lakini kwanini na wewe unaitwa ndume na sio n'ndume?
Khaaaaaaa.......mbona unalinganisha visivyo vya aina moja...??? Hayo maneno aliyoyaulizia yeye yanavyoandikwa na yanavyotamkwa ni tofauti kama ilivyo kwa maneno ya kiingereza
 
Kiswahili kuandika na kutamka ni tofauti kama kilivyo kiIngereza. Ukitaka kutatuwa tatizo la kuandika na kutamka tumia herufi za kiarabu. Kiarabu kina vitamshi vinavyofanya kila neno ulisome kama linavyotamkwa hata kama ndio mara ya kwanza kulisoma hilo neno.

Kumbuka kuwa historically kiswahili kilikuwa kinaandikwa kwa herufi za kiarabu na si za kilatini kama tufanyavyo sasa. Kuna baadhi ya wazee wa kiSwahili mpaka leo hutumiana baruwa za kiswahili kwa maandishi ya kiarabu.
We unakoelekea......mnh haya........
 
acha tusubiri wataalam wakuje kumwaga elimu.

lakini kwanini na wewe unaitwa ndume na sio n'ndume?

sikiliza wewe kwani mimi nimekwambia mimi naitwa n'ndume? Mimi bwana naitwa Ndume bwana swala zima naomba majibu kwa sababu neno linavyoandikwa sivyo linavyotamkika.
 
Hapa tatizo ni kuwa maneno uliyoyataja na mengine kama hayo (ndio=ndiyo, kukua=kukuwa, ingia=ingiya, n.k), yako vilevile kama yalivyoandikwa kwa mara ya kwanza katika karne ya 19 na Johnson, na bado mpaka leo wataalamu wetu hawakufikiria ama kuyabadilisha au kutoa maelezo ya kuridhisha kwa nini yabakie hivyo.

Nafikiri kwa kiasi kikubwa mambo mengi yamerekebishwa katika kamusi la kiswahili lililotolewa na Baraza la Kiswahili Zanzibar mwaka jana, lakini sina hakika kama maneno yote yenye utata yametatuliwa.
 
Jamani acheni siasa mpeni Ndume majibu na kama hamna basi muwe wazi.Ndume nami nasubiri jibu,ila hata miye sijui baraza la kiswahili lilitumia kigezo gani
 
Hapa tatizo ni kuwa maneno uliyoyataja na mengine kama hayo (ndio=ndiyo, kukua=kukuwa, ingia=ingiya, n.k), yako vilevile kama yalivyoandikwa kwa mara ya kwanza katika karne ya 19 na Johnson, na bado mpaka leo wataalamu wetu hawakufikiria ama kuyabadilisha au kutoa maelezo ya kuridhisha kwa nini yabakie hivyo.

Nafikiri kwa kiasi kikubwa mambo mengi yamerekebishwa katika kamusi la kiswahili lililotolewa na Baraza la Kiswahili Zanzibar mwaka jana, lakini sina hakika kama maneno yote yenye utata yametatuliwa.

mimi naona kama unanipigia hadithi sababu unakuwa unageuza mada hayo unayosema mimi sikuyauliza kwa kuwa yapo maneno mengine kama
Mfano:1.Amenionesha ili neno linatokana na kitenzi Ona.
2.Amenionyesha ili linatokana na kitenzi Onya.

Kwa kumalizia watu wengi hutumia maneno hayo kwa kuyachanganya kwa kuzani kuwa yana ujumbe mmoja, kumbe yana jumbe mbili tofauti.

Sasa mimi naomba majibu utata upo palepale ni kigezo kipi walichokitumia mpaka maneno hayo yawe tofauti jinsi ya kutamkika na kuandikika.
 
Kiswahili kuandika na kutamka ni tofauti kama kilivyo kiIngereza. Ukitaka kutatuwa tatizo la kuandika na kutamka tumia herufi za kiarabu. Kiarabu kina vitamshi vinavyofanya kila neno ulisome kama linavyotamkwa hata kama ndio mara ya kwanza kulisoma hilo neno.

Kumbuka kuwa historically kiswahili kilikuwa kinaandikwa kwa herufi za kiarabu na si za kilatini kama tufanyavyo sasa. Kuna baadhi ya wazee wa kiSwahili mpaka leo hutumiana baruwa za kiswahili kwa maandishi ya kiarabu.

mhhhh eti kiswahili kinaandikwa kwa kilatini. soma history ya kitu kwanza. hizi herufi tunazoumia ni za kirumi au kiroma.

hukuwiii kusema hata 1,2,3,4,5 ,6 ni kilatini

ukitaka kujua kilatini original gonga hapa Latin Alphabet
 
Kiswahili kuandika na kutamka ni tofauti kama kilivyo kiIngereza. Ukitaka kutatuwa tatizo la kuandika na kutamka tumia herufi za kiarabu. Kiarabu kina vitamshi vinavyofanya kila neno ulisome kama linavyotamkwa hata kama ndio mara ya kwanza kulisoma hilo neno.

Kumbuka kuwa historically kiswahili kilikuwa kinaandikwa kwa herufi za kiarabu na si za kilatini kama tufanyavyo sasa. Kuna baadhi ya wazee wa kiSwahili mpaka leo hutumiana baruwa za kiswahili kwa maandishi ya kiarabu.
Nakubaliana na wewe cku mmoja ililetwa barua ya Posa kijengoni kwetu lkn barua hiyo iliandikwa kwa kiarabu cha kiswahili,aisee nilipata tabu mpaka kuja kugundua kumbe hiki ni kiswahili ila kimeandikwa kwa herufi za kiarabu,mimi nilifikiri kilichoandikwa mule ni kiarabu ili niwatafsirie kwa kiswahili,basi ukawa ni mteremko tu nikawasomea posa yao na jamaa akaja kuchukua jike lake.
 
sautu za hayo maneno zipo katika matamshi na si maandishi............katika linguistic kuna process inaitwa ASSIMILATION dio iliyotu mika kuficha hizo sauti katika maandishi...
 
mimi naona kama unanipigia hadithi sababu unakuwa unageuza mada hayo unayosema mimi sikuyauliza kwa kuwa yapo maneno mengine kama
Mfano:1.Amenionesha ili neno linatokana na kitenzi Ona.
2.Amenionyesha ili linatokana na kitenzi Onya.

Kwa kumalizia watu wengi hutumia maneno hayo kwa kuyachanganya kwa kuzani kuwa yana ujumbe mmoja, kumbe yana jumbe mbili tofauti.

Sasa mimi naomba majibu utata upo palepale ni kigezo kipi walichokitumia mpaka maneno hayo yawe tofauti jinsi ya kutamkika na kuandikika.
Hapo kwenye bold ndo uwingi wa ujumbe?
 
mhhhh eti kiswahili kinaandikwa kwa kilatini. soma history ya kitu kwanza. hizi herufi tunazoumia ni za kirumi au kiroma.

hukuwiii kusema hata 1,2,3,4,5 ,6 ni kilatini

ukitaka kujua kilatini original gonga hapa Latin Alphabet
Hizi namba tunazo zitumia asili yake si kilatini, namba zina asili ya herufi za Kiarabu na Kihindi.

Arabic numerals or Hindu numerals or Hindu-Arabic numerals are the ten digits (0, 1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9). They are descended from the Hindu-Arabic numeral system developed by Indian mathematicians, in which a sequence of numerals such as "975" is read as a whole number. The Indian numerals were adopted by the Persian mathematicians in India, and passed on to the Arabs further west. They were transmitted to Europe in the Middle Ages. The use of Arabic numerals spread around the world through European trade, books and colonialism.....

Source:


Arabic numerals

Eastern Arabic numerals

Indian numerals
 
kaka swali lako limejikita sana kwenye ngeli za majina hasa katika misimamo yote miwili ule wa kisasa na wakimapokeo na yote hiyo inatoka kutokana na upatanishp wa kisarufi
 
Baraza la kiswahili lilitumi vigezo vipi kuita majina yafuatayo kama ifuatavyo:
mnyama mbwa badala ya kuita m'mbwa.
Mbu badala ya kuita m'mbu.
Nge badala ya kuita n'nge. Vilevile hata neno nje badala ya kuita n'nje.
Naomba msaada kuhusu hizi ni kwa nini waliita hivi?
kweli jf imevamiwa siku hiz haya mambo gani tenaaa hiv umepitia sekondari kweli wewe au mtaala ulikuta wameubadirisha
 
:rain: Maandishi ni alama mojawapo ya lugha inavyowakilishwa. Maneno mengi katika Lugha ya Kiswahili ni yale yaliyosanifiwa enzi hizoooo! kwa sasa tukisema funguwa, onesha, sikiya, panguwa, siyasa.... wenye mtazamo wa sarufi kongwe, tunawaingiza katika mgogoro.
Hivyo fonimu zinazo achwa katika maandishi, huu ni wakati muafaka kuyaandika maneno hayo na yale yafananayo yatendewe haki. Sasa funguweni masikiyo ili msikiye fonimu hizo zinavyo wachwa katika maandiko.
Itachukuwa muda wa kuwabadilisha watumiaji wa abjadi katika kuunda maneno kutokana na vitamkwa. Je, ni siku gani ya usanifishaji mpya ili tujiandaye kuu-o-ndowa utata? Hapa hapatoshi. Ni wakti ni huu kwa wanataaluma na wazuwoni kusemeya haya. Ama sivyo Ndume? :director:
 
Back
Top Bottom