Oneni utata jamani?

:rain: Maandishi ni alama mojawapo ya lugha inavyowakilishwa. Maneno mengi katika Lugha ya Kiswahili ni yale yaliyosanifiwa enzi hizoooo! kwa sasa tukisema funguwa, onesha, sikiya, panguwa, siyasa.... wenye mtazamo wa sarufi kongwe, tunawaingiza katika mgogoro.
Hivyo fonimu zinazo achwa katika maandishi, huu ni wakati muafaka kuyaandika maneno hayo na yale yafananayo yatendewe haki. Sasa funguweni masikiyo ili msikiye fonimu hizo zinavyo wachwa katika maandiko.
Itachukuwa muda wa kuwabadilisha watumiaji wa abjadi katika kuunda maneno kutokana na vitamkwa. Je, ni siku gani ya usanifishaji mpya ili tujiandaye kuu-o-ndowa utata? Hapa hapatoshi. Ni wakti ni huu kwa wanataaluma na wazuwoni kusemeya haya. Ama sivyo Ndume?

Hapo ndipo penyewe
 
Kiswahili si kama Kiingereza, na kinaondoa redundancy ya kurudia herufi kama m na n kama ilivyoandikwa hapo juu. Katika lugha kama kiingereza kuna kitu kinaitwa "silent letters", kwa mfano b haitamkwi inapofuatia m na kuwa mwisho wa neno, kama climb, dumb (as a rule). Sisi tuna reverse hilo kwa kuwa na repeated but invisible m and n kama ilivyoonyeshwa hapo juu.

Bottom line ni kwamba lugha zina rules na exceptions, na lugha si hesabu kwamba lazima zifuate kanuni fulani.

Most probably waandishi wa kwanza wa Kiswahili hawakuwa Waswahili na walipata challenge kuandika maneno fulani ambayo kutamkwa kwake hakufanani kabisa na lugha za kigeni, wakaandika tofauti na ikakubalika mpaka leo. Ndiyo maana mpaka leo tuna mji wa Bagamoyo badala ya Bwagamoyo.
 
Baraza la kiswahili lilitumi vigezo vipi kuita majina yafuatayo kama ifuatavyo:
mnyama mbwa badala ya kuita m'mbwa.
Mbu badala ya kuita m'mbu.
Nge badala ya kuita n'nge. Vilevile hata neno nje badala ya kuita n'nje.
Naomba msaada kuhusu hizi ni kwa nini waliita hivi?
Katika lugha herufi za mwanzo haziwezi zikawa mbili, mfano M'mbwa, m'mbu badala yake inatumika herufi moja mfano mbwa au mbu, au sio Ndume..
 
Back
Top Bottom