On Ndulu: The "Guardian" must be kidding me!

Swala hapa isiwe kwa nini. Serikali ina jukumu la kuwajengea makazi bora raia wake wawe wafanyakazi wa benki, makarani au wakulima etc. Makazi bora kwa wananchi wote, hili ni jukumu ambalo lilianza tulipopata uhuru kama unakumbuka NHC ndio walipewa jukumu la kujenga nyumba na idara yoyote ya serikali ikihitaji nyumba wanakwenda kwa wataalamu wao ambao wamepewa hilo jukumu.

Si jukumu la serikali kuwajengea raia wake makazi bora. Jukumu la serikali ni kuweka mazingira ambayo yatawawezesha raia wake kupata( Kujenga au kupanga) makazi bora. Dhana ya kuwapatia wafanyakazi au raia wake makazi ndiyo iliyotufikisha hapa.

Amandla.......
 
Pasco mara nyingi nakubaliana sana na insights zako,lakini pia huwa unanichanganya sana mara nyingi,Sasa haufagilii lavish spending lakini hapo hapo unataka tuwe na the best money can buy?
Sehemu zote posting imetulia kasoro hapo tu....Na ndio maana nimetoa sanks lakini nikiwa critical kwenye red highlights.
.
jmushi, asante sana kwa maoni yako, ninaposema sifagilii lavish spending, ninamaanisha kuna matumizi ya mabilioni na mabiliona yanakuwa spent na serikali yetu for nothing, or not accounted for. Hii ndio naita lavish spending.

Nimesema we deserve the best money can buy not the luxury. Mimi ni mtu wa Nyerere time, ile miezi 18 ya kujifunga mikanda ndio nilikuwa primary na foleni nimepanga mpaka zile za kupanga mawe nimeshiriki kupata kilo ya unga wa yanga!. Uniform tumevaa 'madurufu'. Kipindi hicho Nyerere alituaminisha personal car ni laxury, tv ni luxury etc. Nyerere ndie alitembelea benzi, mawaziri peogeot 504. Hivyo hata gari la kutembelea na tv kwa wakati huo ilikuwa lavish spending.

Leo gari tv, dish ni ordinary emenities sio laxury tena. Hivyo hiyo nyumba ya gavana, japo kwa sasa itaonekana lavish na laxury, imejengwa idumu miaka 100. Ile swimming pool ambayo leo inaonekana ni laxury, kwa wengine ni exericise ground for tension releave na relaxation, labda Balali angekuwa na swimming pool home na gym, asingekufa mapema vile, angekuwako on the dock na kutegua vitendawili kibao kikiwepo cha Kagoda.

Kwa vile hatuna detailed value for money ya hiyo nyumba na ina nini, then to me spending 1.4 billion kwa nyumba ya hadhi ya gavana itakayoishi for 100 years is not a big deal despite all our povert stinking nation kama hiyo ni fedha ya kununua only a single mobile phone ya Goldvish "Le million".

Rev. Kishoka amekuwa objective kuhoji hivi hiyo nyumba ina nini?. ukishajua what it takes to swallow hiyo bilioni, then tunajustify lawama. J.Mushi huwezi amini, taasisi kama TACAIDS inatumia mara kumi ya kiwango kama hicho kwenye warsha, semina na makongamano kuhusu Ukimwi, huku waathirika wakiuliwa na retroviral kufuatia mlo mmoja kwa siku!.

Bilioni 1.4 is a lot of money in a small picture, but in a bigger picture, its nothing!. We are spending like hell for nothing, tunahaki ya kupiga kelele, ila pia sometime kelele zinazidi hata kama we are spending for something.
 
Usimuonee yeye ameandika kama alivyoona na sio mtaalam. Ameona granite tiles zimetumika, akaambiwa madirisha ni bullet proof na vikolombwezo kibao alipouliza wakamwambia hiyo ndio Japanese technology etc etc. Ujumbe umefika.
 
Japo siungi mkono hiyo PR Capaign ya Guardian, lakini niko curious kujua what a big deal ya hiyo nyumba ya 1.4 Bil. Baada ya kina Mramba, Yona na Mgonja kutiwa ndani, Ndugu jamaa na marafiki wa Mgonja na Mramba, walichangishana kupata thamana. Yona alijidhamini mwenyewe na miongoni mwa dhamana zake ni nyumba yake ya Makongo Juu, 1.2 Bilion. What's so big deal kuhusu hii ya 1.4 kabla hatujapata what are reasons behind justifying it.

Tatizo sio nyumba kugharimu kiasi hicho. Tatizo ni kutumia pesa za umma kujenga nyumba ya gharama hiyo. Kama ingekuwa kajijengea binafsi wengi tusingemchachamalia. kama Yona ana uwezo wa kujijengea nyumba ya mabilioni, hilo si shauri letu ili mradi akituhakikishia kuwa pesa zilizotumika hazikutoka serikalini. Pasco kuwa na simu ya $milioni moja haituhusu. Ni pale Pasco atakaponunuliwa na shirika la serikali simu ya $milioni ndipo panapotokea tatizo. Upuuzi fanyia pesa yako mwenyewe lakini si ya umma! Hakuna justification kwenye hilo.

Amandla........
 
Si jukumu la serikali kuwajengea raia wake makazi bora. Jukumu la serikali ni kuweka mazingira ambayo yatawawezesha raia wake kupata( Kujenga au kupanga) makazi bora. Dhana ya kuwapatia wafanyakazi au raia wake makazi ndiyo iliyotufikisha hapa.

Amandla.......

Kuweka mazingira na kujenga kuna tofauti gani? Au unaongelea mazingira ya rushwa?
 
Usimuonee yeye ameandika kama alivyoona na sio mtaalam. Ameona granite tiles zimetumika, akaambiwa madirisha ni bullet proof na vikolombwezo kibao alipouliza wakamwambia hiyo ndio Japanese technology etc etc. Ujumbe umefika.

Hapana, simuonei. Hii inaweza kuwa walikuwa wanajaribu kuona kama wataweza kutumia upuuzi huo ku-justify matumizi yao ya ovyo! Si unaona wanavyotapa tapa kwenye haka kajumba? Watu hawana aibu hawa.

Amandla......
 
.

Mzee Mwanakijiji, nyumba ya 1.4 Biliion ni nyumba ya Gavana, siyo nyumba ya Ndulu. Kila kitu kilipangwa kabla ya ujio wake.

Nyumba anayokaa ni nyumba ya Benno Ndulu siyo ya gavana, sasa maadam imetokea gavana ndie Benno Ndulu, mwache akae nyumba ya stahiki yake.

Kwa walio dar, si mnapajua pale kwa JK, piteni muune, nini bilioni 1.4!, majirani wamehamishwa hekalu linateremka, si JK yule yule aliyeishi hapo miaka yote?, why now?.

Kama kuna nyumba za mpaka bilioni 10 ila kwa vile ni za wahindi, hao hao wanaoendesha serikali kwa remote, hizo ni hizo hizo top up za rada, gulf stream etc, hatusemi, lakini akijengewa mwenzetu!.

Mtu wa kwanza kuendesha Ferari bongo Bongo ni mhindi, wa pili mwarabu, mswahili bado sijaona na akitokea ataitwa fisadi.

Nasisitiza siungi mkono matumizi yoyote mabaya ya fedha za umma, bali siungi mkono shutuma kwa matumizi yanayoonekana, japo mabaya, huku tuko kimya kwa mabilioni na mabilioni yanatumiwa kwa vitu visivyoonekana.

Pale kwa gavana, si angalau jengo lipo, nimewaambia kila safari moja ya mkulu, zinatumika zaidi ya hizo, kipi kinaonekana?.

Tumemlipa Prof. De Sotto, consultancy ya Dola, 1,000,000 kwa siku moja iliyokuja nchini, tunawalipa wangapi kwa huduma kama hiza and what do we get there after? Si afadhali hapo jengo la hadhi ya gavana lipo?.



Very true, tatizo hapa naona jazba ndio zinatawala. Nyumba ni kweli inaweza kugharimu bilioni 1.4 kutegemea na material yalitumika, security systems nk.

Ningekuwa mimi ningeuliza mchanganuo wa gharama kwanza kabla sijaita watu wajinga( MMK anasema Guardian are stupid).

Pia umefafanua vizuri kuwa ni nyumba ya Gavana wa benki kuu sio ya Beno Ndulu.

MMK sometimes naona kama sifa zimezidi na kudhani wate ambao hawafikiri kama yeye ni wajinga. NA mara nyinyine anapinga kila kitu.

Hasa siku hizi unaonyesha kama umeshuka kidog.. u complain on everything , ooh sijui Haiti hutujasaidia yani sijui vipi .. unaboa at times ile mbaya.
 
Kuweka mazingira na kujenga kuna tofauti gani? Au unaongelea mazingira ya rushwa?

Mazingira ni pamoja na kumwezesha mwananchi kupata mahali pa kujengea, kuweza kupata pesa ( kipato kizuri au uwezo wa kukopa) au malighafi ya kujenga kama anataka. Ni mwananchi ndiye anayejenga sio serikali. Unaposema jukumu la serikali ni kujenga ina maana serikali inajenga na kumkabidhi nyumba mwananchi! Na kuwa na makazi mazuri si lazima yawe yako. Panatakiwa pawe na makazi mazuri yanayoweza kupangwa kwa bei inayomudika.

Si kila kitu ni rushwa.

Amandla........
 
Pasco. Nenda taratibu, mbona unataka kutufanya wote limbukeni?

Hauwezi kutumia titanium kama nondo. Hata huko japan hawatumii. Titanium quality zake hazikidhi mahitaji. Titanium inatumika zaidi katika kufunika jengo na sio kwenye zege.

Hakuna kitu kama Japanese technology ya kujengea skyscraper. Ujuzi ni ule ule. Hesabu za structure ni zile zile. Ubunifu ni kwa watu binafsi na sio kwa taifa, Kwanza skyscrapers nyingi hazijengwi kwa zege. Ni chuma mtindo mmoja.

Light wood ndio nini? Kupunguza uzito kwenye nini? Unaweka sakafu na kuta za granite halafu unaogopa uzito!

Bullet proof windows za nini? Hivi wao wasiwasi wao ni watu kupigwa risasi au jengo kulipuliwa? Hizi ndiyo specification za kipuuzi.

Naona aliyekutembeza amekuingiza mkenge. Ukweli ni kuwa kwenye lile jengo hakuna value for money ya aina yeyote.

Amandla.......

Asante Fundi Mchundo,
Nilitembezwa katika hili hili la kutaka kujua, masikini mimi, sina hili wala lile, nilidanganywa kama walivyodanganywa wenye jengo, limejengwa kama oval office, eti safe and secure.

Tena ili kuwalinda watumishi wa BOT eti nao wanakinga ya kutoshitakiwa popote kutokana na utekelezaji wa maukumu yao, kama ile ya rais!.

Nakubaliana na wewe, kama ni mtu hujua titanium ni nini, utakubali unachoambiwa. Tena electical ya jengo line ni supper conductors!. Inawezekana wameyasema yote hayo ili kuhalalisha ulaji tuu, justification inapatikana kwenu wenye uzoefu wa nini haswa kimefanyika, kimegharimu nini na tunaambiwa nini sie tusiojua.
Thanks.
 
Very true, tatizo hapa naona jazba ndio zinatawala. Nyumba ni kweli inaweza kugharimu bilioni 1.4 kutegemea na material yalitumika, security systems nk.

Ningekuwa mimi ningeuliza mchanganuo wa gharama kwanza kabla sijaita watu wajinga( MMK anasema Guardian are stupid).

Pia umefafanua vizuri kuwa ni nyumba ya Gavana wa benki kuu sio ya Beno Ndulu.

MMK sometimes naona kama sifa zimezidi na kudhani wate ambao hawafikiri kama yeye ni wajinga. NA mara nyinyine anapinga kila kitu.

Hasa siku hizi unaonyesha kama umeshuka kidog.. u complain on everything , ooh sijui Haiti hutujasaidia yani sijui vipi .. unaboa at times ile mbaya.


Kabla ya kutoa shutuma na kuleta Jazba kama ulivyosema, thamani ya nyumba iliyojengwa haizidi 500 million kuna jamaa walileta data kwenye thread ya ile nyumba.

Vile vile kuna consultants ambao wametoa vidokezo na ushahidi kusema haiwezekani pesa nyingi kiasi kile kwa kale kajumba. Sasa wewe kama una Bill of quantity ya hiyo nyumba iweke hapa ili tuweze kuchambua mchele na pumba.
 
We say the said expenditure was a pretext because available evidence indicates that, based on the annual rent of 113 million/- BoT had been paying for the governor’s accommodation in rented premises

Hiyo nyumba walipanga kutoka kwa nani? Na ilikuwa wapi? Na ikoje?

Amandla........
 
Mazingira ni pamoja na kumwezesha mwananchi kupata mahali pa kujengea, kuweza kupata pesa ( kipato kizuri au uwezo wa kukopa) au malighafi ya kujenga kama anataka. Ni mwananchi ndiye anayejenga sio serikali. Unaposema jukumu la serikali ni kujenga ina maana serikali inajenga na kumkabidhi nyumba mwananchi! Na kuwa na makazi mazuri si lazima yawe yako. Panatakiwa pawe na makazi mazuri yanayoweza kupangwa kwa bei inayomudika.

Si kila kitu ni rushwa.

Amandla........


Nikupe mfano wa UK. Serikali ina jukumu la kuwapatia makazi raia wake. Kama hawana nyumba inawapatia mahali pa kuishi na kuna system ya kuweza kuona uwezo wa kila raia wake. Ukiweza kulipa kodi kwa miaka kadhaa wanakuuzia kwa bei poa nk. Na hii ni kwa sababu ya kukusanya kodi na kuweka vitu muhimu kama makazi nk.

Unachosema wewe ni kwamba wale waliopata ndio basi wengine walie tu. Yaani waliowahi kuingia NHC warithishane hadi kiama. Je kulikuwa na muongozo gani hadi hawa wakodishwe na wengine wasiweze kukodishwa kwenye nyumba za NHC?

Je katiba ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema nini kuhusu hili?

Ukipitia yote hayo utarudi hapa na kuniambia jukumu ni la serikali na hapo ndipo utakata mzizi wa Wizi ambao umekubuhu na hauna tija kwa taifa. Pesa ambazo serikali inakusanya kwenye kodi nk ni tosha kabisa kufanya mambo makubwa ambayo wengine wanaona ni miujiza.
 
It’s such a shame, it’s such a shame, (Ndulu)
Don’t walk away, don’t walk away(Ndulu)

yana mwisho haya.
 
Tatizo sio nyumba kugharimu kiasi hicho. Tatizo ni kutumia pesa za umma kujenga nyumba ya gharama hiyo. Kama ingekuwa kajijengea binafsi wengi tusingemchachamalia. kama Yona ana uwezo wa kujijengea nyumba ya mabilioni, hilo si shauri letu ili mradi akituhakikishia kuwa pesa zilizotumika hazikutoka serikalini. Pasco kuwa na simu ya $milioni moja haituhusu. Ni pale Pasco atakaponunuliwa na shirika la serikali simu ya $milioni ndipo panapotokea tatizo. Upuuzi fanyia pesa yako mwenyewe lakini si ya umma! Hakuna justification kwenye hilo.

Amandla........

This is what is referred as "the crux of the matter". Watu wanafikiria tunagombana kuwa Gavana anaishi kwenye nyumba iliyogharimu bilioni 1.4.. kama ingekuwa ni ya kwake na kutokana na mapato yake halali hakuna ambaye angehoji.. sisi ni mabepari bwana! Kwani kuna mtu kalalamikia nyumba anayoishi Rostam au Mengi?
 
Hivi hadhi ya Ndullu ni kubwa kuliko Wakazi wa Kagera ambao hawana reliable airport? au Lindi Au Tabora au Sumbawanga etc etc? na kati ya Nyumba ya Ndullu na maendeleo mengine mfano kuwa na Scanner Hospitali ya Bombo etc lipi linalo faa ?
 
Hiyo nyumba si itatumiwa na Ndulu, na Gavana wa BOT atakayefuata baada ya Ndulu?
 
Very true, tatizo hapa naona jazba ndio zinatawala. Nyumba ni kweli inaweza kugharimu bilioni 1.4 kutegemea na material yalitumika, security systems nk.

Ningekuwa mimi ningeuliza mchanganuo wa gharama kwanza kabla sijaita watu wajinga( MMK anasema Guardian are stupid).

Pia umefafanua vizuri kuwa ni nyumba ya Gavana wa benki kuu sio ya Beno Ndulu.

MMK sometimes naona kama sifa zimezidi na kudhani wate ambao hawafikiri kama yeye ni wajinga. NA mara nyinyine anapinga kila kitu.

Hasa siku hizi unaonyesha kama umeshuka kidog.. u complain on everything , ooh sijui Haiti hutujasaidia yani sijui vipi .. unaboa at times ile mbaya.

I choose my words very careful; and I mean them!

kusema kuwa "nyumba ni ya Gavana na siyo ya Ndulu" ni kuchezea maneno!
 
Hiyo nyumba si itatumiwa na Ndulu, na Gavana wa BOT atakayefuata baada ya Ndulu?

Hivi unakumbuka Nyumba ya NHC aliyokuwa anakaa BWM ilikarabatiwa kiroho mbaya wakati yeye ni rais na baadaye aliuziwa kwa bei ya peremende.

Ndulu naye atapewa mkono wakati anastaafu kwa bei ile ile ya pipi. Hiyo ndio Tanzania ya leo, ile katiba inasema makazi bora kwa .... .... lakini Serikali ya Chama Cha Majambazi inaigeuza kama kinyonga.
 
Back
Top Bottom