Omnipotence paradox na ukomo wa nguvu za Mungu

Walikuwepo watu wakubwa, wenye nyadhifa, wenye kiburi na makufuru zaidi yako.

Lakini siku ya mwisho wakaja kumkili Mungu. Na wengine walienda na dhambi zao na sasa wanapata haki yao huko ahera.

Na wewe ipo siku utauona uwepo wa Mungu, uwe hai au umekufa.
Riwaya
 
4574173.jpg


Omnipotence

Limetokana na maneno mawili ya kigiriki "omni na potens " ambayo yaana maanisha mwenye nguvu zote

Moja kati ya maswali ambayo ukimuuliza muumini wa dini yeyote ile mkristo au muislamu kuwa "Je, nguvu za Mungu wako zina ukomo?".

Jibu ambalo atakujibu ni hili, "Nguvu za Mungu wangu hazina ukomo".

Lakini fikiria hili; karne ya 12 mwanafalsafa maarufu wa wakati ule Averroes alisema haya kuhusu omnipotence;

"Can deity create a rock so heavy that even the deity itself cannot lift it? So then the rock is now unliftable limiting the deity power, but if not then the deity is not omnipotent because it cannot create that rock.

Hii ni sawa na kusema hivi "Je, katika sheria hizi hizi na Euclidean geometry, Mungu anaweza kutengeneza pembetatu ambayo jumla ya angle zake siyo 180?

Au Mungu anaweza kutengeneza gereza ambalo lina ulinzi mkali kiasi kwamba hata yeye mwenyewe hawezi kutoroka?
.....Tatizo siku hizi watu wanajifanya wanamjua sana Mungu wengine wanamuongezea na yao, wakati inatakiwa tumuonyeshe busara na kumuogopa lkn siku hizi wanamuongelea simple tu kama Shemeji tu
 
Mishaweza kudhibiti kifo ndio ntawasikiliza na kuwaheshi

Mungu ni kila kitu na hana kipimo chq nguvu wala limits
 
Kuna wakati nlikuwa natumia neno "omnipotence" nkajiona labda nakosea..kufanya utafiti nkakuta neno sahihi ni "Omnipresent." Sasa nimeliona tena kwenye kichwa cha uzi, sijui ndo mm nachanganya mafile..
 
Kuna wakati nlikuwa natumia neno "omnipotence" nkajiona labda nakosea..kufanya utafiti nkakuta neno sahihi ni "Omnipresent." Sasa nimeliona tena kwenye kichwa cha uzi, sijui ndo mm nachanganya mafile..
Omnipotence ni uwezo wa kufanya kila kitu au kuwa na nguvu zisizo na kipimo

Omnipresence ni uwezo wa kuwa kila sehemu.
 
Unaharibu, mungu hajaumba mauti, angalia tena chanzo chako
Mungu aliumba umauti kabla ya uhai...kwenye kuran mungu anasema amemuumba binadamu kutoka ufu hadi uhai..na pia chanzo kinasema mungu aliumba umauti kabla ya uhai kwa viumbe vyake.
 
.
Magagafu, hujajieleza vizuri. Na wanafalsafa wengi hawako upande wako. Hebu fuatilia hoja za hawa wawili:

A version of argument by William L. Rowe:
  1. There exist instances of intense suffering which an omnipotent, omniscient being could have prevented without thereby losing some greater good or permitting some evil equally bad or worse.
  2. An omniscient, wholly good being would prevent the occurrence of any intense suffering it could, unless it could not do so without thereby losing some greater good or permitting some evil equally bad or worse.
  3. (Therefore) There does not exist an omnipotent, omniscient, wholly good being.
[William L. Rowe (1979). "The Problem of Evil and Some Varieties of Atheism". American Philosophical Quarterly 16: 337].

Another argument by Paul Draper:
  1. Gratuitous evils exist.
  2. The hypothesis of indifference, i.e., that if there are supernatural beings they are indifferent to gratuitous evils, is a better explanation for this situataion than theism.
  3. Therefore, evidence prefers that no god, as commonly understood by theists, exists.
[Paul Draper (1989). "Pain and Pleasure: An Evidential Problem for Theists". Noûs (Nous, Vol. 23, No. 3) 23 (3): 331–350 doi:10.2307/2215486. JSTOR 2215486].

Umeziona hoja hizi? Hebu changamsha ubongo sasa. Usikubali kukaririshwa tu.....
Mbona wewe umekaririshwa na hawa jamaa....usimlazmishe mtu kufata kile unachokiamini....
Binafsi naamini uwepo wa Muumba wa mbingu na Ardhi na vilivyomo...na watu kama nyie nawaona ni Mashetani tu...na mbaya zaid u cant change that.
 
Mr einstein newton hebu muulize huyo muumini hili swali

JE, MUNGU WA KWENYE BIBLIA NI MKUU NA NI MJUAJI WA YOTE KWELI?

Mwanzo 6: 5-7

5 Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.

6 akajilaumu Bwana alivyofanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyoni wake.

7 Bwana akamwambia, Nitaharibu mtu niliyemwumba kutoka uso wa dunia; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana najilaumu ya kwamba nimewafanya.

Mwanzo 6: 11-13

11 Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa jeuri.

12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.

13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; maana dunia imejaa jeuri kwa njia yao; na tazama, mimi nitangamiza dunia yote

Hivyo sababu kubwa ya mungu kuleta gharika duniani ni kwa sababu binadamu walikuwa wabaya, rushwa na vurugu. Naye alitumia gharika kuondoa ubaya, rushwa, na watu jeuri.

Je, alifanikiwa? Je gharika duniani ililikomesha waovu, wala rushwa na vurugu?

HAPANA! Mungu alishindwa tena. unaweza kudhani Mungu anayejua yote kwamba anajua wakati ujao bila kujua gharika kuwa itashindwa kutimiza lengo kusudi lake (ili kuharibu nchi ya waovu, wala rushwa, na watu waliojaa jeuri), bado inaonekana hakufanya hivyo.

MPAKA NAONGEA HAYA, DUNIA IMEJAA UOVU KULIKO ULE WA KIPINDI CHA GHARIKA, SODOMA NA GOMORA.

MUNGU MKUU NA MUWEZA YOTE AMEFELI?


[HASHTAG]#Tujisahihishe[/HASHTAG]
[HASHTAG]#Tujikomboe[/HASHTAG] na Utumwa wa akili
[HASHTAG]#Sambaza[/HASHTAG] ujuzi
Na wazazi wako ushawasambazia huu upumbavu ?
 
Mbona wewe umekaririshwa na hawa jamaa....usimlazmishe mtu kufata kile unachokiamini.... Binafsi naamini uwepo wa Muumba wa mbingu na Ardhi na vilivyomo...na watu kama nyie nawaona ni Mashetani tu...na mbaya zaid u cant change that.
.
Kauli zako zinajenga ukuta badala ya daraja. Lakini, kumbuka, jamiiforums ni jukwaa la mijadala--only point counterpoint. Kwa ajili ya kukuonyesha jinsi watu makini wanavyobishana kisomi kwa kutumia utaratibu huo, na hasa kuhusu swali linalohusu "Ama kuwepo au kutokuwepo kwa Mungu," hebu angalia kitabu hiki ambacho nimeambatanisha hapa. Kinaitwa "A DEBATE BETWEEN A CHRISTIAN AND AN ATHEIST." Ukifanikiwa kuelewa 33% ya yaliyomo humu utakuwa umekombolewa. Hilo likishindikana mpelekee mchungaji/paroko wako akusaidie kutoa ufafanuzi.....
 

Attachments

  • God-A-Debate-between-a-Christian-and-an-Atheist--Craig-Sinnott-Armstrong.pdf
    816.2 KB · Views: 89
Hali na sifa za Mungu sio hizo peke yake kama wewe unamwamini Mungu....na kuruhusu mabaya sio kwamba sifa zake zimejipinga.....ila kwa uelewa wa kibinadamu utaona kajipinga ila vitabu vya dini vimeelezea vizuri embu visome tena kwa ufasaha na ukiamini Mungu yupo utaelewa
.
Nimekusoma. Lakini, hapa tunajenga hoja, sio ya kiteolojia, bali ya kifalsafa--natural theology. An argument against the existence of God from the existence of evils is a show-stopper my friend. Kwa ufahamu zaidi wa hoja hii, hebu pitia chapter 4 ya kitabu hiki halafu tuwasiliane: "A DEBATE BETWEEN A CHRISTIAN AND AN ATHEIST"--Nimeambatanisha hapa chini....
 

Attachments

  • God-A-Debate-between-a-Christian-and-an-Atheist--Craig-Sinnott-Armstrong.pdf
    816.2 KB · Views: 71
Mkuu kama una Thoedicy yoyote yenye mashiko njoo nayo!
.
Mkuu Eistein Newton,

Salaam. Uliomba theodicy yenye mashiko. Sikuwa nayo. Nimeagiza toka USA na imefika. Hii hapa: "A DEBATE BETWEEN A CHRISTIAN AND AN ATHEIST"--Naambatanisha. Ile hoja yetu, an argument against God's existence starting from the existence of evils in the world, inapatikana sura ya nne. Lakini soma kitabu chote kwanza ndio tuanze mjadala....
 

Attachments

  • God-A-Debate-between-a-Christian-and-an-Atheist--Craig-Sinnott-Armstrong.pdf
    816.2 KB · Views: 64
.
Kauli zako zinajenga ukuta badala ya daraja. Lakini, kumbuka, jamiiforums ni jukwaa la mijadala--only point counterpoint. Kwa ajili ya kukuonyesha jinsi watu makini wanavyobishana kisomi kwa kutumia utaratibu huo, na hasa kuhusu swali linalohusu "Ama kuwepo au kutokuwepo kwa Mungu," hebu angalia kitabu hiki ambacho nimeambatanisha hapa. Kinaitwa "A DEBATE BETWEEN A CHRISTIAN AND AN ATHEIST." Ukifanikiwa kuelewa 33% ya yaliyomo humu utakuwa umekombolewa. Hilo likishindikana mpelekee mchungaji/paroko wako akusaidie kutoa ufafanuzi.....
Still this book is just a piece of shit...I am Muslim and m sure 100% wahat I stand for. Achana na kina Einstein au Newton...jitambue wewe kama wewe.
 
Still this book is just a piece of shit...I am Muslim and m sure 100% wahat I stand for. Achana na kina Einstein au Newton...jitambue wewe kama wewe.
.
You sound extremely dogmatic. The book is philosophical per se. No christian arguments in it. Open up your mind.....
 
.
You sound extremely dogmatic. The book is philosophical per se. No christian arguments in it. Open up your mind.....
I said I know what I stand for...beyter this way...your way leads astray..My mind has been open looong looong time ago.
 
kuna ku run away ambako hutokea pale speed governor inapofyatuka. yaan kitu kinakuwa out of your control. hivi ndivyo alivyo shetani. ni sawa na kufuga chatu kisha likakugeuka!
so kila anachokipanga Mungu shetan hukibadili. Hata humu jf shetan hutumia sana baadhi yetu kupandikiza mawazo hasi juu ya Mungu wetu.
kumbuka Mungu ni roho. na shetani ni roho! so Yesu alimtumia bikira Maria lakin shetan hutumia makahaba!
so always sheyan yupo kinyume kbsa na Mungu.
 
Ukweli nikwamba swali halijibiki, ukijibu una muondolea mungu sifa ya kuwa muweza wayote.
 
Nimeuliza.

Kama mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote yupo, kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Kama aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani lakini hakutaka tu, ni kweli ana mapenzi yote?

Kama hakuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani licha ya kutaka kuuumba ulimwengu huo, ni kweli ana uwezo wote?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom