Che mittoga
JF-Expert Member
- Mar 28, 2017
- 14,365
- 18,152
Usijali Mkuu.Uko vzr mkuu umeeleza vzr sana..
Mungu huwa haelezeki kwa Fikra za Kibinadamu.
Hadi Yeye ajitambulishe kwetu La sivyo asingejitambulisha tusingemwelewa kabisa.
Kila tunachoweza kukijua Kinamtii Mungu, kiwe Hai au bila Uhai.
Ona jinsi Yesu Kristo alivyouamrisha Upepo nao Ukamtii,
alivyoamrisha Dhoruba nayo Ikamtii,
alivyoulaani Mtini nao Ukaogopa na Kukauka Kabisa na Kufa.
Alivyoyaamrisha Maji Yambebe na Akatemea juu yake (hayo maji)
Alivyo iamrisha Nguvu ya Gravity imnyanyue hadi juu Mawinguni Ikamtii na Kumpaisha Akiwa katika Hali ya Uzito wa Mwili.
Nakadhalika na kadhalika.
Swali hilo lililoulizwa, kuhoji Uweza wa Mungu huwa Linajengwa sana na Shetani Lucifer.
Lengo la Lucifer kuuliza swali hilo ni kuwafanya watu wawe na mashaka na uweza wa Mungu wakati yeye pia naye hajui Uweza wote wa Mungu Aliyemuumba,
na ndicho kilichomfanya Lucifer awe na Kiburi na kutaka naye aabudiwe kama Mungu.
Laiti angejua mwanzo Uweza wa Mungu angelikuwa mpole na mtiifu kwake.
Maswali kama haya pia huwa wanaulizwa watu wanaojiunga na Jamii za Siri za Kishetani ili wasimwogope Mungu.
Kama umesikia Secret Societies, Illuminant, Skull of Bones nk.
Kila kitu kinamtii Mungu.Nadhani Umenielewa kwanini nimekwambia hivyo.