Old school days - Mko wapi?

aaah shemeji huyo kwenye red usingemtaja umenitonesha (alikuwa mkufunzi wangu)

afu kumbe nilichelewa kidogo tu we shem ningecheza 'disko' la welcome fomu wani na wewe.....

Shem, mie nilikuwa siku nyingi sana hapo Mazengo. Mkoba wakati anakuja Mazengo amenikuta. Enzi hizo ilikuwa shule ya WANAUME tu. Baadaye nikaja sikia imekuwa mchanganyiko. Pia siyo siri kuwa enzi hizo nilikuwa MSHAMBA wa kutupwa. Nilikulia Dar hadi nilipoanza kuzidisha utundu. Nikarushwa kijijini na sikuona wala Tabora mjini hadi nilipofika darasa la saba. Effect yake ilikuwa kubwa sana. Nilipofika Disco nilikuwa nashangaa tu. Enzi hizo pale Mazengo Disco linapigwa na wale watoto wa yule Mzee Wa Kinyamwezi mwenye kituo kinaitwa KAGUNILA Radio Service wale uwanja ya Jamhuri. Mzee alikuwa na Spika yule si kawaida. Mara ya kwanza niliona Spika ikitoa BASS peke yake. Ni baada ya miaka mingi sana nikaja kufahamu kuwa inaitwa SUBWOOFER. Hii ilikuwa mwanzo wa miaka ya 80. Baadaye akaja Mwalimu mmoja wa Kihaya na yeye akawa anatupigia Disco pale alikuwa akiitwa MGANYIZI. Mganyizi alitumika hata kwenye kukariri Periodic Table yaani "Lile Beda bovu Chonya Nipe Orange Fanya Nende, Na Mganyizi alivuta Sigara Paketi Sita Arusha..." Ahh Na-Sodium, Mganyizi-Magnesium......

Kuna mwalimu mmoja wa Kigogo alikuwa akifundisha Kiwahili, yeye alikuwa akiongelea ngono tu. Alinifanya nianze tabia ya kuangalia miguu ya wanawake. Unakuta linasema "Look her, from behind, her leg ........ hahahahaaa siyo chenzo bwana!!!!" Alikuwa akijisifu jinsi anavyofaulisha wanafunzi kwenye mitihani. Imekaribia mitihani tukagundua hatuelewi kitu. Ikabidi watu tukimbilie Mama mmoja wa Kipare akiishi Kikuyu Flats akiitwa Mwalimy Kasira kama sikosei. Tukamuomba notes zake na tukasoma tukitumia na yale aliyotufundisha zamani. Wagogo kweli ni WASANII.

Sasa Shem, kama ulifundishwa na Paramagamba sijui, na wewe alikuweka Ile alama ya 50 cent usoni? Maana Wagogo hawachelewi. Nilivyoona mara ya kwanza nikafikiri labda walipoona Train locomotive ila taa yake, wakaionea wivu na wao wakaamua WAWEKE ZAO usoni. Wagogo BANA!!!!
 
Nimepita A Level 2003-2005 but nimezaliwa na kuishi maeneo karibu na Moshi Tech, nakumbuka kulitokea vurugu mwaka 1994 ,wanafunzi walivunja duka wakanywa soda ,wakamwaga unga.Kulikuwa na dogo tunasoma nae primary baba yake alikuwa ticha Mwl Mrema wanafunzi walimkimbiza kwenye mahindi but Mzee alikuwa na speed kinoma .Walimu karibia wote hawakulala kwenye nyumba zao usiku walikuja FFU kutoa dozi,ukikatiza eneo la shule kipigo then unaingia kwenye karandinga
 
Elnino,

Peter Malembeka, baba yake walisoma na huyo Munuo sijui? Basi Peter alikuwa akilalamika kuwa jamaa alikuwa akiriport kila siku kwa baba yake. Hata Pesa akawa anakatwa kwa sababu Munuo alimwambia baba yake kuwa vijana hawahitaji pesa nyingi. Jamaa akakatiwa pesa. Ila kijamaa kilikuwa kihangaikaji sana aisee. Kilikuwa kikija Arusha na kusaka pesa kwa udi na uvumba. Ukipata contact zake basi nirushie.
 
Shem, mie nilikuwa siku nyingi sana hapo Mazengo. Mkoba wakati anakuja Mazengo amenikuta. Enzi hizo ilikuwa shule ya WANAUME tu. Baadaye nikaja sikia imekuwa mchanganyiko. Pia siyo siri kuwa enzi hizo nilikuwa MSHAMBA wa kutupwa. Nilikulia Dar hadi nilipoanza kuzidisha utundu. Nikarushwa kijijini na sikuona wala Tabora mjini hadi nilipofika darasa la saba. Effect yake ilikuwa kubwa sana. Nilipofika Disco nilikuwa nashangaa tu. Enzi hizo pale Mazengo Disco linapigwa na wale watoto wa yule Mzee Wa Kinyamwezi mwenye kituo kinaitwa KAGUNILA Radio Service wale uwanja ya Jamhuri. Mzee alikuwa na Spika yule si kawaida. Mara ya kwanza niliona Spika ikitoa BASS peke yake. Ni baada ya miaka mingi sana nikaja kufahamu kuwa inaitwa SUBWOOFER. Hii ilikuwa mwanzo wa miaka ya 80. Baadaye akaja Mwalimu mmoja wa Kihaya na yeye akawa anatupigia Disco pale alikuwa akiitwa MGANYIZI. Mganyizi alitumika hata kwenye kukariri Periodic Table yaani "Lile Beda bovu Chonya Nipe Orange Fanya Nende, Na Mganyizi alivuta Sigara Paketi Sita Arusha..." Ahh Na-Sodium, Mganyizi-Magnesium......

Kuna mwalimu mmoja wa Kigogo alikuwa akifundisha Kiwahili, yeye alikuwa akiongelea ngono tu. Alinifanya nianze tabia ya kuangalia miguu ya wanawake. Unakuta linasema "Look her, from behind, her leg ........ hahahahaaa siyo chenzo bwana!!!!" Alikuwa akijisifu jinsi anavyofaulisha wanafunzi kwenye mitihani. Imekaribia mitihani tukagundua hatuelewi kitu. Ikabidi watu tukimbilie Mama mmoja wa Kipare akiishi Kikuyu Flats akiitwa Mwalimy Kasira kama sikosei. Tukamuomba notes zake na tukasoma tukitumia na yale aliyotufundisha zamani. Wagogo kweli ni WASANII.

Sasa Shem, kama ulifundishwa na Paramagamba sijui, na wewe alikuweka Ile alama ya 50 cent usoni? Maana Wagogo hawachelewi. Nilivyoona mara ya kwanza nikafikiri labda walipoona Train locomotive ila taa yake, wakaionea wivu na wao wakaamua WAWEKE ZAO usoni. Wagogo BANA!!!!

hahaa shem hizo stori zinanichekesha sasa...am just imagining ulivokuwa mshamba lol!!

anyway hiyo ilikuwa longi sana bana mi sikuwepo huko, ningewahi tungegongana maana msalato na mazengo walikuwa partners wakudumu....bihawana ni supliments tu!!

Huyo Prof Kabudi kumbe ni 'msanii' na ile kitu kumbe ni ndonya??

nilimtolea uvivu siku moja alinishushua class kisa sijasoma novel ambayo yeye aliinunua 'amsterdam' airport!!! aliipa maneno ya ufedhuli sana na mi nikamtolea uvivu!!!
 
Nimepita A Level 2003-2005 but nimezaliwa na kuishi maeneo karibu na Moshi Tech, nakumbuka kulitokea vurugu mwaka 1994 ,wanafunzi walivunja duka wakanywa soda ,wakamwaga unga.Kulikuwa na dogo tunasoma nae primary baba yake alikuwa ticha Mwl Mrema wanafunzi walimkimbiza kwenye mahindi but Mzee alikuwa na speed kinoma .Walimu karibia wote hawakulala kwenye nyumba zao usiku walikuja FFU kutoa dozi,ukikatiza eneo la shule kipigo then unaingia kwenye karandinga

Yeah sisi tulivyoondoka kulikuwa hakuna A level, nafikiri itakuwa PCM - wakati tunasoma hap wewe ulikuwa primary - shule ilikuwa nzuri sana, Kulikuwa na kambi ya DANIDA - pale pale shuleni so maintanance ilifanyika kila mara kwa uangalifu.

Sidhani kama kipindi chenu mmekuta Jangos laws, bisi nk
 
Shem, mie nilikuwa siku nyingi sana hapo Mazengo. Mkoba wakati anakuja Mazengo amenikuta. Enzi hizo ilikuwa shule ya WANAUME tu. Baadaye nikaja sikia imekuwa mchanganyiko. Pia siyo siri kuwa enzi hizo nilikuwa MSHAMBA wa kutupwa. Nilikulia Dar hadi nilipoanza kuzidisha utundu. Nikarushwa kijijini na sikuona wala Tabora mjini hadi nilipofika darasa la saba. Effect yake ilikuwa kubwa sana. Nilipofika Disco nilikuwa nashangaa tu. Enzi hizo pale Mazengo Disco linapigwa na wale watoto wa yule Mzee Wa Kinyamwezi mwenye kituo kinaitwa KAGUNILA Radio Service wale uwanja ya Jamhuri. Mzee alikuwa na Spika yule si kawaida. Mara ya kwanza niliona Spika ikitoa BASS peke yake. Ni baada ya miaka mingi sana nikaja kufahamu kuwa inaitwa SUBWOOFER. Hii ilikuwa mwanzo wa miaka ya 80. Baadaye akaja Mwalimu mmoja wa Kihaya na yeye akawa anatupigia Disco pale alikuwa akiitwa MGANYIZI. Mganyizi alitumika hata kwenye kukariri Periodic Table yaani "Lile Beda bovu Chonya Nipe Orange Fanya Nende, Na Mganyizi alivuta Sigara Paketi Sita Arusha..." Ahh Na-Sodium, Mganyizi-Magnesium......

Kuna mwalimu mmoja wa Kigogo alikuwa akifundisha Kiwahili, yeye alikuwa ya waakiongelea ngono tu. Alinifanya nianze tabia ya kuangalia miguu ya wanawake. Unakuta linasema "Look her, from behind, her leg ........ hahahahaaa siyo chenzo bwana!!!!" Alikuwa akijisifu jinsi anavyofaulisha wanafunzi kwenye mitihani. Imekaribia mitihani tukagundua hatuelewi kitu. Ikabidi watu tukimbilie Mama mmoja wa Kipare akiishi Kikuyu Flats akiitwa Mwalimy Kasira kama sikosei. Tukamuomba notes zake na tukasoma tukitumia na yale aliyotufundisha zamani. Wagogo kweli ni WASANII.

Sasa Shem, kama ulifundishwa na Paramagamba sijui, na wewe alikuweka Ile alama ya 50 cent usoni? Maana Wagogo hawachelewi. Nilivyoona mara ya kwanza nikafikiri labda walipoona Train locomotive ila taa yake, wakaionea wivu na wao wakaamua WAWEKE ZAO usoni. Wagogo BANA!!!!

Sikonge, hizo sehemu za blue zimenifurahisha sana, kaka bora wewe umezaliwa mjini ukakulia sweka - mimi kuiona dar ilikuwa wakati napita kwenda moshi Tech kuanza form one, tupo wengi tu humu tuliolivamia jiji kama wanavyotuambia.

Kijijini mkuu enzi za primary kulikuwa na madisco hasa siku za xmas, Mwaka mpya na Pasaka - tatizo lake ilikuwa ni vumbi - ukumbi lazima umwagiwe maji kwanza mida ya saa tisa tisa - wengi walicheza Peku - sasa wachache wenye viatu akikukanyaga lazima urushe ngumi. ulinzi ulikuwa mdogo kwa hiyo kulikuwa na personal defence - mimi na manati yangu pembeni aniguse mtu naachia...

Pikiniki yangu darasa la saba ilikuwa safi sana - pilau la kijiji kijiji tukalipika - disko lilianza saa tisa mchana hadi saa 3 usiku - saa Moja mwalimu mkuu wetu akatufungua rasmi na Mwalimu wetu wa darasa wa kike ( by then alikuwa katoka chuo butimba mdogo tu) tulipenda kumtania sana ukizingatia wakati huo ndo wa ukuaji yaani kupevuka.

Mwalimu Mkuu ( Jamaa alikuwa fataki) akan'gan'gania mzigo wa ticha wetu wakati wa kufungua mziki wimbo naukumbuka hadi sasa ni ule " Shauri yako" wa Super Mazembe -http://www.youtube.com/watch?v=wzCvxIWVs7E Mimi nikaanza kutoa chozi la wivu - marafiki zangu wakaja kunifariji tukataka kumfanyizia mwalimu mkuu, Ticha wetu akamwachia Mkuu akaja kunipoza pale akaniambia nisiwe na wasiwasi nikianza kazi nitapata wanawake wengi hadi weingine nitakuwa nawakataa mi nikanyamaza kwa shingo upande - lakini leo naamini maneno ya ticha wangu.
 
Mkuu ELNINO,

Nakushukuru kwa hii "flashback"!

Vipi, yule teacher wa Biology (Mrs Futa) bado yupo? Alinifanya nikafurahia sana somo la "Biology"!

Mi nilimpenda huyu mwalimu alipokuwa anafundisha REPRODUCTION SYSTEM!
Kila alipouliza mmeelewa darasa zima linaitikia bado.....
Soma katikati ya mistari hapo!
 
Wakuu tutafutane tukumbushie yale mambo yetu ya zamani - zamani raha bwana siku hizi shida tupu.

Wale wa Masama, Kiraeni, Kbosho, Weruweru girls schools mpo? mnakumbuka zile nyimbo za slow slow yaani blues? duh zilikuwa zikipigwa zile ni hatari tupu hapo njia ya kupunguza msongo wa mawazo. naongelea 1986 to 95 hivi.
 
kwa wale tuliesomea mwanza kuna mashindano yalikuwa yanaitwa rottery asee ilikuwa sio mchezo, ilikuwa ni sehemu ya kuonyeshea nani mjanja, nani anjua kuvaa vizuri, nani mbabe na mambo kibao, shule kama lake secondary, bwiru boys, nsumba aka washamba wa pori na buswelu ilikuwa nom, mji mzima ulikuwa patashika ikifika kipindi cha rottery, pamba sec walikuwa wakali sna wa netball...miss those dem days
 
Ee bwanae umenigusa mahali pake,Memberswa JF walosoma umbwe (mtisafi) -(captain babile) miaka ya 85-88 mnakumbuka tulivyoaliwa na Kiraeni Girls katika graduation ya form yao ya kwanza kipindi cha masika mvua mtindo mmoja wenye mabasi wakagoma kutupeleka? Ilibidi Headmaster(Mtui) akatoa mkoko(lori) litupeleke likawekwa kipande cha turubali.Kufika kiraeni watu wako nyambunyambu tope tukaingizwa bafu watu wakaoga wakatia viwalo -wakati huo dont touch my schoes na raba za morogoro canvas.Mnakumbuka tulipewa vitochi vya mbege wakaja kilimanjaro boys kuzamia? du mbali sana
 
aisee mimi nakumbuka miaka ya 80/81 nilikuwa kule Iringa girls sec school, basi graduation moja tulialiikwa na kina kaka wa Mazengo high school, wakatuletea basi safari hadi Dodoma, tukafika mchana mchana hivi, tukapewa maakuli na dorm kupumzika kusubiri disco usiku, jioni tukajisafi na kufika ukumbuni, nakumbuka vile giza lilikuwa limeshaingia ilikuwa ni kusindikizwa na kikosi maalum cha wanafunzi na waalimu kutembea (umbali kiasi hivi) kutoka bwenini hadi ukumbini, ilikuwa tunapigwa hesabu za harakaharaka kila wakati, binti hata mmoja asije akapotea kwenye vichaka LOL maana njemba wa lower sec walikuwa wanatumezea mate ile mbaya, kwani hata disco lenyewe hawakuwa na cards za kuingia. Basi kudura ya mwenyezi mungu wasichana wote tukafika salama ukumbini, disco likachezwa hadi karibu na alfajiri hivi, tukawa tena tunajiandaa kutoka ukumbuni kurudi tena kuchuka mizigo yetu bwenini na kupanda basi kurudi Iringa, ile tunatoka nje (bado giza giza), usalama wetu ulikuwa bado matatani, na kwa bahati mbaya sana, binti mmoja akapotea kwenye miti na vichaka and she was sexually abused, ilisikitisha sana na ikawa kesi kubwa (ilibidi abaki Dom). Hii thread imenikumbusha hili tukio. Baada ya hili tukio headmistress wetu akawa mgumu sana kuturuhusu kwenda kwenye mialiko ya disco ya boys school.
 
Nakumbuka sie korogwe girls wavulana wetu walikuwa watu wa Tanga School,nao walikuwa mafundi na mikono yao migumu!,tulikuwa tunaazima anzia gauni mkpaka viatu toka kwa watoto wa walikuwa nazo!
 
Aisee!!! Mmenikumbusha mbali sana!!! lakini mimi naanzia nyuma kidogo!!! Mission Boarding school Tosamaganga kwa Sister Forosina, Kibasa na Padri Chengula!!! Enzi za Balaga Benito na Elton!!! ilikuwa ni kula Buluga kwa kwenda Mbele bila kusahau kwenda Lupalama kuogelea!!! nakumbuka pia wakati ule tulikuwa tunagombea kutumikia kanisani bila kujali huyu ni muisilamu mluteri au mroma!! life was very fun!!!
 
Bush people can't tell me nothing...

Nyani Nguruwe;
By the way; what is mjini? What is kijijini? Who is more advantaged kati ya aliyezaliwa bongo na ana uwezo wa kuishi bongo na ulaya, au aliyezaliwa ulaya na ana uwezo wa kuishi ulaya peke yake? Yupi ni mjanja kati ya hawa wawili? Wewe dogo kila siku huwa nakwambia bongo yako shule yake itakuwa ina mgogoro sana. Watu unawaharibia mada kwa kubadilisha focus ya mada! na kwa taarifa yako mimi siyo bushman, mimi ni Hotentont, jamii ya Bushmen ambao wao wanakuwa even more primitive!
 
Kulikuwa na wazamiaji wakuu hasa kutoka Kolila sec na Old moshi - hii mijemba ilikuwa inanusa disko hata likiwa wapi then inazamia - walinichekesha tu pale walipopitia maliwato ya kike kuzamia disko kule Kibosho ambalo moshi Tech tulikuwa tumealikwa. - disco likafungwa mlinzi alipigwa kwa sababu ya unoko wake.

.


Duhh kwenye red hapo umenigusa kabisa, ile shule ilikua na vitimbi mijamaa mingi iliyosoma pale sasa ni wanajeshi walipenda sana kubeba chuma na ni moja ya michezo ya shule, nusu ya wanafunzi walikua wanapuliza lile jani, ilikua ni ubabeubabe tu.
 
Tuandae dinner date tukutane - tumwalike DJ too short au Mr. Mtaa wa Mangoma - atupe ile miziki yetu ya wakati ule - mnaonaje?
tukutane na wale watoto wa enzi zile....
 
Mi nilimpenda huyu mwalimu alipokuwa anafundisha REPRODUCTION SYSTEM!
Kila alipouliza mmeelewa darasa zima linaitikia bado.....
Soma katikati ya mistari hapo!
Ha ha ha; kijana kumbe ulianza siku nyingi
 
Back
Top Bottom