Uko sahihi kaka. Ccm walishindwa kusoma game na alama za nyakati mapema. Wakafikiri ni zile enzi za Mwinyi, Mkapa Jk pengine na Magufuli kuwa tutaburuza tu kama siku zote, kumbe muda ushawatupa mkono.
Wakashindwa kujari mambo ya watu watu wanatekwa kisiasa mnawajibu pumba, watu wanaenda mahakamani sehemu muhimu ya kuipata haki wanapigwa na kuvunjwa miguu. Wanafungia makanisa zaidi ya 2,000 mara anavamiwa na anapigwa katibu wa TEC raia hasira zinajaa balaha.
Unafungia chama cha siasa tena kikuu cha upinzani kisifanye siasa na mwenyekiti wake unamtia ndani, machungu unawajengea hawa wananchi je wayaelezee wapi machungu yao?.
Alafu anatoka mtu eti watu walilipwa nani atalipa mamilioni hayo yote ya watu Ili waandamane?.
Najiuliza chadema Ile kauli mbiu yao ya NRNE ingeendelea nchi nzima ingelikuwaje kama tu hiyo Kidogo imetikisa hivyo.
Ushauri tu kwa ccm hii nchi ni kubwa na raia wameongezeka, hamuwezi kutawala peke yenu tena kwa sera za miaka ya 1970s is big no.
Watu million 61 wote hawawezi kuwa na fikra za ujamaa tuu wakati ambapo tunatawaliwa na ubepari ulimwengu karibia wote. Acheni kiburi raia hawapo upande wenu tena namna nzuri ya kusababisha raia wawe upande wenu balancini uwanja wa kisiasa.