Ogopa hizi shuhuda

Ogopa hizi shuhuda

Kuna siku nilikua zangu nyumbani likizo fupi.basi nikiwa sina hili wala lile nilishangaa meseji inaingia kwenye simu yangu frm mamdogo wangu yupo Arusha.Akaniambia amepata matatizo nimsaidie elf 50 kwa mpesa atanirudishia akijisort.nikaamua kumpigia ajabu akawa hapokei.nikapiga kama mara nne nilitaka kumuuliza kama kuna tigopesa maana mimi mpesa yangu nilikua na 2000 tu.wapi?hapokei.

Basi nikamtumia hivyo hivyo atajijua mwenyewe maana simu hapokei.kama nusu saa hivi dadaangu nae ananipigia kuniambia kama mamdogo amekwama lakini nimemsort.nikamwambia basi tumemtumia kwa wakati mmoja.sio kesi.sijakaa sawa mama ananiambia hebu mpigieni mama yenu mdogo mimi nikimpigia hapokei kasema kuna tatizo anaomba hela.apo alarm ikalia.

Nikampigia mume wake.eti mamdogo yuko wapi?akasema sijui maana kanitumia meseji eti amepata shida nirushie elf 50 sasa nikipiga hapatikani.na akipatikana hapokei.tukahisi tumeliwa.muda huo huo na mamdogo akampigia mumewe kumwambia kama kaibiwa simu na anarudi nyumbani.daah heka heka iliopita hapo si mchezo.mbio mpaka kwa

wakala.yangu ilifanikiwa kurudishwa ila zingine zilienda maana alikua anatumia tigo na mimi nilituma tigopesa kwa hiyo ikashindwa kutolewa.ile zile laki moja mpesa za dada na mama zikaliwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa mganga fulani ni kiboko. Kuna madalali mpaka kwenye ulozi.

Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa kapiga pesa ndefu kwenye kamari. Huyu kaumizwa naye anataka akuumize.

Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa biashara GLND, FOREVER LIVING nk zinalipa sana. Huyu keshapigwa na ana mzigo mkubwa wa bidhaa na hana wa kumuuzia, Ukikubali unalo lake.

Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa biashara fulani inalipa na faida yake ni chap chap. Huyu hajui ni mropokaji tu naye kasimuliwa.

Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa fulani kafanikiwa kupitia njia fulani lakini yeye yuko hapo hapo akiwa hohehahe hana mbele wala nyuma. Hizi ni story za vijiweni,

Hii dunia haina shortcut, hakuna pesa za bure. Kila sent lazima uitolee jasho.

Marafiki wa mitandaoni wanaojifanya wako njema na wanataka mshirikiane kufanya ishu ya pesa. Hawa ni matapeli tu, wezi waganga njaa kama wengine tu.

Mtu anayekushuhudia fursa kwa bashasha na lugha za kuvutia jua ya kwamba tayari aneshakuona wewe ni fursa..

Bahati mbaya sana hata baada ya kusoma hii post bado kuna watu watapigwa na watakuja hapa kulalama.. Na wengine watapigwa hapa hapa na wana JF wenzao

Ishu za madini
Ishu za mali ya Mjerumani
Ishu za pesa za majini
Ishu za Freemason
Ishu za utajiri wa kafara
Ishu ya dola za kusafisha
Ishu za madawa, vipuri, vivyago, magari, vyakula na zabuni mbalimbali kupitia UN kwenda kambi za wakimbizi zote hizi ni wizi na utapeli

MAKINIKA, MAKINIKENI, WAJINGA HAWAISHI ILA KUKUMBUSHANA NI ADA.

Jr
you're genius

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niko Kyela huku kuna mahali panaitwa Ipyana darajani karibu na Kambi ya jeshi la JWTZ kuna jamaa anaitwa Chaurembo mkinga mmoja kapigwa 2 million kwa kuamini uganga uganga na jamaa anaduka lenye vitu full, siku nne hajafungua duka stress za kupigwa...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niko Kyela huku kuna mahali panaitwa Ipyana darajani karibu na Kambi ya jeshi la JWTZ kuna jamaa anaitwa Chaurembo mkinga mmoja kapigwa 2 million kwa kuamini uganga uganga na jamaa anaduka lenye vitu full, siku nne hajafungua duka stress za kupigwa...

Sent using Jamii Forums mobile app
nilikaa sana hapo darajani...njia kuu ya kuelekea NGONGA BEACH..hv bdo ipo ile?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bro mmoja kariakoo alipigwa 124m
Aiseee walimpeleka LINDI PANGONI ETI AKASHIKE MKONO WA MALAIKA WA ULINZ WA PESA.ANASEMA WA BARIDI
HALAFU WALIMPELEKEA SANDUKU TATU ZA DOLA ETI AWEKE NA HELA ZAKE ZA KIBONGO.AISEEEEE
Naomba story zaid please,,,,,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa mganga fulani ni kiboko. Kuna madalali mpaka kwenye ulozi.

Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa kapiga pesa ndefu kwenye kamari. Huyu kaumizwa naye anataka akuumize.

Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa biashara GLND, FOREVER LIVING nk zinalipa sana. Huyu keshapigwa na ana mzigo mkubwa wa bidhaa na hana wa kumuuzia, Ukikubali unalo lake.

Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa biashara fulani inalipa na faida yake ni chap chap. Huyu hajui ni mropokaji tu naye kasimuliwa.

Mtu anayekushuhudia kwa hakika kuwa fulani kafanikiwa kupitia njia fulani lakini yeye yuko hapo hapo akiwa hohehahe hana mbele wala nyuma. Hizi ni story za vijiweni,

Hii dunia haina shortcut, hakuna pesa za bure. Kila sent lazima uitolee jasho.

Marafiki wa mitandaoni wanaojifanya wako njema na wanataka mshirikiane kufanya ishu ya pesa. Hawa ni matapeli tu, wezi waganga njaa kama wengine tu.

Mtu anayekushuhudia fursa kwa bashasha na lugha za kuvutia jua ya kwamba tayari aneshakuona wewe ni fursa..

Bahati mbaya sana hata baada ya kusoma hii post bado kuna watu watapigwa na watakuja hapa kulalama.. Na wengine watapigwa hapa hapa na wana JF wenzao

Ishu za madini
Ishu za mali ya Mjerumani
Ishu za pesa za majini
Ishu za Freemason
Ishu za utajiri wa kafara
Ishu ya dola za kusafisha
Ishu za madawa, vipuri, vivyago, magari, vyakula na zabuni mbalimbali kupitia UN kwenda kambi za wakimbizi zote hizi ni wizi na utapeli

MAKINIKA, MAKINIKENI, WAJINGA HAWAISHI ILA KUKUMBUSHANA NI ADA.

Jr™️
Hao wa kushuhudia biashara fulani inalipa ni wengi sana,hao ni wahujumu uchumi wa vijana wenye uchungu wa maisha.Maana wengine ni wazee wanaoonekana kuwa na hekima kumbe maboya tu na wanaishia kuumiza watu wanaowaamini
 
Back
Top Bottom