Ogopa hizi shuhuda

Ogopa hizi shuhuda

Una umri chini ya miaka 40... Anatokea mtu anakuambia mlima fulani kuna mashimo ama mapango yana mali za mjerumani.. Unaweka mashaka lakini anakuaminisha kabisa
Ukimwangalia ni kachala kachoka kabisa lakini anakwambia ukitafuta KIASI fulani cha pesa mkafanya kafara mtapata hiyo mali.. Na kwa ujuha wa kiwango cha juu mno unamuamini na kusahau kabisa kujiuliza haya
Hizo ni mali gani?
Zina thamani gani?
Utauza wapi?
Utamuuzia nani?
Nani kathibitisha uwepo wake? Kwanini yeye hakuchukua?
Ina maana walioweka ni wapumbavu kiasi cha kuacha kuja kuzifuatilia?
Ni nani hapendi utajiri? Ina maana hakuna watu wenye uwezo wa pesa walio tayari kuitafuta hiyo mali kwa njia zozote zile?

CC: Slim5

Jr
BRO Mshana Jr
Mm.mtu akianzaga hizo stori namuuliza huna ndugu yeyote mwenywe pesa mfanye naye biashara? Kweli nimewahi pigwa 100k kwa wale wauza odds WANASEMA fixed GAMES ODDS 123+ from my trustfull source...WAKENYA BWANA.
 
WEKA hapa mkuuu...huko utawachomeka chaji watu..mpaka aje wa kuwachomoa chaji washapeleka washapigwa sana
 
Hapo kwenye zabuni za UN kambi za wakimbizi inakuwaje huo utapeli

Sent using Jamii Forums mobile app
Unapigiwa simu na rafiki wa kitambo lakini usiyemkumbuka Ila yeye anakujua (kiuhalisia kakudukua tuu) yeye anakupa siri ya dili la kupeleka vitu huko na mlipaji ni UN kisha anakuunganisha na boss wake mzungu anayeongea kiingereza safi kabisa.. Utachanganyiwa habari mpaka utapigwa kama ukiwa na tamaa ya kupata haraka

Jr
 
me ubahili wangu ndo huwa unanisaidia jamani, we ongea yooooote shawishi uwezavyo, ila ikifikia sehemu ukataja nitoe hela hapo ndo kwa heri ya mimi na wewe, hela yangu ngumu mno kutoka yaaani saaana hv hv tu aisee Big No
 
Utapeli unaonitesa mimi siyo huo ulioainisha hapo,

Natapeliwa na rafiki, ndugu na wafanyakazi wenzangu kupitia mikopo, nakuwaga na huruma mtu akiwa na shida akiomba umkopeshe kiasi fulani unatoa lakini mpaka sasa nimepoteza marafiki na ndugu kibao kwani mkopo ukiiva hata kama unataka kumsalimia anahisi unadai pesa yako hivyo kuishia kukukwepa na kutopokea simu.

Kwa sasa naona kama nimeanza kuwa na roho mbaya kwa sababu ya maumivu ya kutapeliwa hadi rafiki zangu wa karibu naishia kusema kwa sasa niko vibaya mno hata kama niko vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Doooh! Rafiki yangu fulani alinihakikishia kuwa kilimo cha viazi ulaya kinalipa ile mbaya.Basi bwana, tukaandaa mpango mzima na nikamwaga million kadhaa. Kweli tulilima but mvua zimenyesha hadi kero, viazi full kuugua ugonjwa wa mnyauko.Mwisho wa siku mavuno yamekuwa negative na millions zimepotea hivi hivi.

Next time mtu asiniambie sijui upuuzi gani gani unalipa. Kama unalipa dump pesa zako mwenyewe kwenye huo upuuzi ili zikulipe.
 
I bet from time to time, I'm not doing it seriously like other folks and I have a few apps to guide me for that. I place say 5k in four different stakes and trust me, one or two of them MUST tick.

Maisha yenyewe haya ni kamari tupu, ona sasa Corona inataka kuanza kutumaliza, we bet in every step of our lives.

Sina objection na uliyoandika, ni ukweli mtupu.
 
Doooh! Rafiki yangu fulani alinihakikishia kuwa kilimo cha viazi ulaya kinalipa ile mbaya.Basi bwana, tukaandaa mpango mzima na nikamwaga million kadhaa. Kweli tulilima but mvua zimenyesha hadi kero, viazi full kuugua ugonjwa wa mnyauko.Mwisho wa siku mavuno yamekuwa negative na millions zimepotea hivi hivi.

Next time mtu asiniambie sijui upuuzi gani gani unalipa. Kama unalipa dump pesa zako mwenyewe kwenye huo upuuzi ili zikulipe.
Lakini mkuu je kama mngevuna? Haya maisha hakuna formula ya nini cha kufanya ili mtu afanikiwe, ilitokea tu hivyo mvua zimezidi mkakosa. Let's not look at this in one dimension, ingia tena shambani mzee.
 
Back
Top Bottom