Libya
JF-Expert Member
- Nov 11, 2016
- 783
- 1,918
#Sasa basi
===
Taarifa ya awali inasema Watu ambao hawajajulikana, usiku wa kuamkia leo wamevamia na kumwagia petroli kisha kuchoma moto Ofisi za CHADEMA Kaskazini na ofisi za Mkoa na Wilaya
Uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea kubaini wahusika na madhara yaliyojitokeza
ZAIDI:
Ofisi za kanda ya Kaskazini zilizopo Arusha, zimechomwa moto. Jengo lote limepigwa petroli, madirisha yakavunjwa, moto ukawashwa mlango wa mapokezi. Moto ulizimwa na "fire". Mlinzi hajukikani alipo, silaha zake zimeokotwa, jirani anasema alimsikia Mlinzi akipiga kelele kuwa amevamiwa akiomba msaada akiwa anakimbia - anafukuzwa, hajapatikana hadi sasa.
Yote hayo yanatokea wakati mgombea urais wa CHADEMA ndg. Tundu Lissu akiingia Arusha leo kutafuta saini za wadhamini akitokea Katesh, Hanang
===
Taarifa ya awali inasema Watu ambao hawajajulikana, usiku wa kuamkia leo wamevamia na kumwagia petroli kisha kuchoma moto Ofisi za CHADEMA Kaskazini na ofisi za Mkoa na Wilaya
Uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea kubaini wahusika na madhara yaliyojitokeza
ZAIDI:
Ofisi za kanda ya Kaskazini zilizopo Arusha, zimechomwa moto. Jengo lote limepigwa petroli, madirisha yakavunjwa, moto ukawashwa mlango wa mapokezi. Moto ulizimwa na "fire". Mlinzi hajukikani alipo, silaha zake zimeokotwa, jirani anasema alimsikia Mlinzi akipiga kelele kuwa amevamiwa akiomba msaada akiwa anakimbia - anafukuzwa, hajapatikana hadi sasa.
Yote hayo yanatokea wakati mgombea urais wa CHADEMA ndg. Tundu Lissu akiingia Arusha leo kutafuta saini za wadhamini akitokea Katesh, Hanang