Ofisi ya Waziri Mkuu yatangaza Fursa ya Kusoma bure katika fani mbalimbali

DR Mambo Jambo

JF-Expert Member
May 10, 2012
8,591
17,711
Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Imetangaza Programu ya Kukuza Ujuzi Nchini inayowezesha nguvu kazi ya Taifa kupata ujuzi na stadi za kazi stahiki ili kumudu ushindani katika soko la ajira.

Ofisi imeingia makubaliano vyuo mbalimbali kutoa mafunzo mafunzo ya ufundi stadi kukuza ujuzi na stadi za kazi kwa vijana. Miongoni mwa mafunzo yatakayotolewa ni Ubunifu wa Mitindo na Ushonaji Nguo, Ufundi Bomba, Uashi, Useremala, Uchomeleaji na Uungaji vyuma, Upakaji rangi na maandishi ya alama, Utengenezaji wa vipuri vya mitambo, Ufundi Magari na Mitambo, Umeme wa Majumbani na Viwandani, TEHAMA, Umeme wa Magari, Huduma za Hoteli na Utalii, Ukataji Madini ya Vito na Kilimo.

Mafunzo hayo yatatolewa Bure kabisa kwa vijana wote
Hivyo, tunapenda kuwatangazia vijana wa Kitanzania wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 wanaopenda kujiunga na mafunzo katika mojawapo ya fani zilizoorodheshwa hapo juu wafike katika vyuo vilivyoainishwa na Tangazo hili hapa chini ili kuchukua fomu ya kuomba kujiunga na mafunzo. Serikali itafadhili ada ya mafunzo kwa asilimia 100.

Mwanafunzi / mzazi / mlezi atagharamia gharama nyingine zikijumuisha nauli ya kwenda chuoni na kurudi nyumbani bhasi..

Maombi yawasilishwe kuanzia tarehe 01/11/2023 hadi tarehe 14/11/2023 yakiambatana na nyaraka zilizoorodheshwa...

HUENDA HAWA WAKAWA NDO WALIMU WA MAFUNZO YA AMALI KWA MTAALA WETU MPYA TUCHANGAMKIE VIJANA

Pitia hapa:
Nafasi za masomo fani mbalimbali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu
 
Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Na ajira yatangaza Masomo BURE kwa vijana Kati ya Miaka 15-35 kijana mwenye kigezo na unahitaji kusoma Fani hizi kimbilia Fursa..IMO Tehama, Usonara,na ufundi mbalimbali

Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Imetangaza Programu ya Kukuza Ujuzi Nchini inayowezesha nguvu kazi ya Taifa kupata ujuzi na stadi za kazi stahiki ili kumudu ushindani katika soko la ajira.

Ofisi imeingia makubaliano vyuo mbalimbali kutoa mafunzo mafunzo ya ufundi stadi kukuza ujuzi na stadi za kazi kwa vijana. Miongoni mwa mafunzo yatakayotolewa ni Ubunifu wa Mitindo na Ushonaji Nguo, Ufundi Bomba, Uashi, Useremala, Uchomeleaji na Uungaji vyuma, Upakaji rangi na maandishi ya alama, Utengenezaji wa vipuri vya mitambo, Ufundi Magari na Mitambo, Umeme wa Majumbani na Viwandani, TEHAMA, Umeme wa Magari, Huduma za Hoteli na Utalii, Ukataji Madini ya Vito na Kilimo.

Mafunzo hayo yatatolewa Bure kabisa kwa vijana wote
Hivyo, tunapenda kuwatangazia vijana wa Kitanzania wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 wanaopenda kujiunga na mafunzo katika mojawapo ya fani zilizoorodheshwa hapo juu wafike katika vyuo vilivyoainishwa na Tangazo hili hapa chini ili kuchukua fomu ya kuomba kujiunga na mafunzo. Serikali itafadhili ada ya mafunzo kwa asilimia 100.

Mwanafunzi / mzazi / mlezi atagharamia gharama nyingine zikijumuisha nauli ya kwenda chuoni na kurudi nyumbani bhasi..

Maombi yawasilishwe kuanzia tarehe 01/11/2023 hadi tarehe 14/11/2023 yakiambatana na nyaraka zilizoorodheshwa...

HUENDA HAWA WAKAWA NDO WALIMU WA MAFUNZO YA AMALI KWA MTAALA WETU MPYA TUCHANGAMKIE VIJANA



pitia hapa
Kama ni kweli hii safi sana
 
Mbona kwenye tangazo hawajaweka kozi za muda gani mfano short cozi au long co ya miaka level 2 ya veta,wizara wameweka tangazo kisanii mno
 
Mbona kwenye tangazo hawajaweka kozi za muda gani mfano short cozi au long co ya miaka level 2 ya veta,wizara wameweka tangazo kisanii mno
 
Back
Top Bottom