nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
OFISI YA BUNGE YAPOKEA RASMI NYUMBA MPYA YA SPIKA MJINI DODOMA LEO
Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge Bw. John Joel (kushoto) akijadili jambo na Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango na Teknologia ya Mawasiliano Bw. Didas Wambura kabla ya makabidhiano rasmi ya jengo la nyumba atakayokuwa anatumia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyopo eneo la Uzunguni nje kidogo ya mji wa Dodoma leo.
Mshauri Mwelekezi (consultant) wa Pacha Building Construction Company ( ambayo ndiyo imejenga jengo hilo) Bw. Shaban Mwatawala (kulia) akitoa maelezo ya ujumla kabla ya kuwapitisha viongozi wa Ofisi ya Bunge katika jengo hilo. Kulia kwake ni Mhandisi wa Miradi wa Pacha Bw. Johanes Maganga, Mkurugenzi wa Mipango na Teknolojia ya Mawasiliano wa Bunge Bw. Siegfied Kuwite, na Mkurugenzi wa Sgighuli za Bunge Bw. John Joel.
Bwana Mwatawala akimkabidhi Msanifu Majengo M. F. M Msangi (kulia) anayewakilisha Wakala wa Majengo ya Serikali. Wakala wa Majengo Tanzania ndiye Meneja wa Mradi huu.
Muonekano wa nyumba hiyo kwa mbele. Jengo hili ambalo litakuwa makazi ya Spika yeyote atakayeliongoza Bunge la Tanzania lilianza kujengwa Disemba 2009 na limegharimu takriban sh. 1.5 bilioni. Hapakuwahi kuwa na nyumba rasmi ya Spika wa Bunge Dodoma.
Mlango wa mbele wa jengo.
Ngazi ndani ya jengo ambalo lina vyumba vinne vya kulala, sehemu ya mapumziko, sehemu ya chakula, maktaba na jiko.
Upande wa nyuma wa jengo.
Chanzo:Michuzi
Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge Bw. John Joel (kushoto) akijadili jambo na Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango na Teknologia ya Mawasiliano Bw. Didas Wambura kabla ya makabidhiano rasmi ya jengo la nyumba atakayokuwa anatumia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyopo eneo la Uzunguni nje kidogo ya mji wa Dodoma leo.
Mshauri Mwelekezi (consultant) wa Pacha Building Construction Company ( ambayo ndiyo imejenga jengo hilo) Bw. Shaban Mwatawala (kulia) akitoa maelezo ya ujumla kabla ya kuwapitisha viongozi wa Ofisi ya Bunge katika jengo hilo. Kulia kwake ni Mhandisi wa Miradi wa Pacha Bw. Johanes Maganga, Mkurugenzi wa Mipango na Teknolojia ya Mawasiliano wa Bunge Bw. Siegfied Kuwite, na Mkurugenzi wa Sgighuli za Bunge Bw. John Joel.
Bwana Mwatawala akimkabidhi Msanifu Majengo M. F. M Msangi (kulia) anayewakilisha Wakala wa Majengo ya Serikali. Wakala wa Majengo Tanzania ndiye Meneja wa Mradi huu.
Muonekano wa nyumba hiyo kwa mbele. Jengo hili ambalo litakuwa makazi ya Spika yeyote atakayeliongoza Bunge la Tanzania lilianza kujengwa Disemba 2009 na limegharimu takriban sh. 1.5 bilioni. Hapakuwahi kuwa na nyumba rasmi ya Spika wa Bunge Dodoma.
Mlango wa mbele wa jengo.
Ngazi ndani ya jengo ambalo lina vyumba vinne vya kulala, sehemu ya mapumziko, sehemu ya chakula, maktaba na jiko.
Upande wa nyuma wa jengo.
Chanzo:Michuzi