grafani11
JF-Expert Member
- May 24, 2011
- 15,441
- 5,820
Watoto fumbebi macho wakubwa wanashughulikia maandalizi ya kula K.
Watoto fumbebi macho wakubwa wanashughulikia maandalizi ya kula K.
kwani hiyo picha iliwekwa hapo ili tuipake rangi si ili tuidadavue?kha maneno yamekushinda pita hiyo ndio khabari ya mujini sasa
Utamaduni ndio kila kitu?, mbona sasa huendi kucheza ngoma za jadi , mbona huvai ngozi, hata kama ni utamaduni kama kitu hakina maana hakuna sbbu ya kuendelea nachoTamaduni ndo kila kitu... Huoni ajabu kwa kuwa ume adopt utamaduni usio wako...
waafrika washamba sana . Sasa hapo kuna tatizo gani?
Sasa JK anaingiaje hapa.....wabongo kwa kuforce mambo....ngoja tusubiri za slaa na josephine 2015:madgrin:
Asante kwa msamaha wako mamangu. Baada ya kuona umenisamehe labda nifafanue tu kidogo kukutaarifu kuwa nimeishi Amerika kwa jumla ya miaka kama minne hivi. Wakati wa Orientation ya Chuo Kikuu tulipelekwa kwenye Swimming Pool ya Mkuu wa Chuo nyumbani kwake. Nilipata shida sana na utamaduni wa wale watu. Tusichana tudogo kama wewe hivi nusu uchi kwenye swimming pool. We mastimu ya Mwafrika unayajua lakini? Sasa uniambie inakuwaje hapo kama tukiamua tunaiga kila kitu. Hizo Swimming pool hapa Bongo zitakuwa salama kweli? Kwenye foleni za kulipia umeme tu watu wahashindwa kuvumilia.
Belinda mdogo wangu; au pengine mwanangu tamaduni zinajengwa kutegemea mazingira ya watu wanaounda tamaduni husika. Maumbile, mazingira na sirka ya Mwafrika vinakataza kuiga kila kitu wanafanya wazungu. Mengine tuwaachiage tu wenyewe.
Wakati nikiwa na umri mdogo wasichana walikuwa na namna yao ya kukuambia mtoto wa kiume wanakupenda--kama kukubali kukumbatiana upenuni mwa jengo au kwenye kichaka cha michongoma ambako hakuna mtu anaona. Ilikuwa nyie wawili tu ndo mnajua mnapendana sana. Mama alimpa lip kis mtoto wake. Sikumbuki lip kiss kwa mume hadharani. Hilo lilikuwa na tatizo gani Belinda. Na ndoa za wakati ule zilidumu sana. Huko Amerika miaka ya 80 takwimu zilikuwa zinaonesha zaidi ya nusu ya ndoa zote ambazo zinafungwa huvunjika katika miaka miaka miwili.
Si kila utamaduni unafaa kuigwa!
Nimekusoma vizuri sana mkuu Highlander. hii ni picha tu tunaishangaa, mie mwenyewe sibusu mupenzi hadharani. Si unajua tamaduni tofauti na madhara yake tunayajua kwenye jamii.
Natamani kweli nijue umri wako, nimekuwa curious ghafla.
Halafu ukiacha mtoto wao anayewashangaa raia wengine wako busy na mambo yao.
Usikute huyo mtoto ndio aliwaambia wafanye hivyo, majuu hamnazo.
Utajua kuwa ni mjaluo? Hiyo ndio Americano bwana, hata jamaa yangu Pazi wa mwanerumango akienda anakuwa waziri
50something mamangu. pale Mlimani wanatuita bbc. born before computers. na wewe je?
50 bado unatesa sana na hivi ni mwanaume..mie late 20!!..kizazi cha obamacare au bbm🙂) he he
Du!... Belinda, mtoto wa mwanaume mwenzangu. Watoto wa siku hizi mnavojua kutupamba?! "Hivi sasa [mimi] ni mwanaume," unasema. Haya basi. Asante.... Uwe na siku njema binti wa mwanaume mwenzangu.
Boflo unamuonea wivu huyo mama.....ha hahahahahaha