Nikikuita mjinga nitakupa hadhi, wewe ni mpumbavu hasa, Mandela aliwapa wazungu sh ngapi ili wampaishe?
Na wazungu walipata faida gani kumpaisha Mandela?
Pathetic zero brain!
Sent using
Jamii Forums mobile app
Hapa unachemka mkuu; usidhani unafahamu kila kitu ndugu, huu ni ulimwengu wa sayansi jamii; mitazamo, uzoefu na mazingira uliyokulia vina umuhimu mkubwa katika mjada uliouanzisha.
Watu wengi tunawakubali mashujaa wetu ambao kwa namna moja ama nyingine waliiletea heshima bara letu. Hili la Mandela vs Mwalimu, huhitaji kukaza misuli ya shingo, kuna ukweli mkubwa Mandela anaweza asimpate Mwalimu. Labda tuweke vigezo ndiyo tutaelewana. Huhitaji kutukana au kudhihaki ili uonekane bingwa, hapa tunajifunza tu. Mfano, wa vigezo ni:
1. Eneo ambalo kila mwanaharakati kati ya wawili hawa walifanya harakati zao. Kumbuka Nyerere ana mchango pia katika kuwasapoti kina Mandela. Mpaka leo waafrika kusini huja kuzuru kambi kama Mazimbu na Dakawa, zote zikiwa ni kambi za wanaharakati wao wakijipanga kwenda kukomboa nchi. Si, Afrika ya kusini pekee, ni nchi nyingi Tz ilifanya haya, mfano, Msumbiji, Zimbabwe n.k
Hapo juu unamshambulia mchangiaji wa mada yako eti Mandela ana nini cha kuwapa wazungu. Hujiulizi kwa hiki Nyerere alikifanya, kama kweli wazungu ni wakweli huoni Nyerere alipaswa kupata tuzo zaidi ya Mandela? Kwa kifupi, hatubezi juhudi za Mandela lakini ule umaarufu ulitiwa chumvi na wazungu kwa sababu zao binafsi. Kumbuka huyu ndiye alikuwa gaidi kwao hadi kumyima viza kuingia nchi zao lakini baada ya kukubaliana namna ya kuindesha Afrika ya kusini bila kuwadhuru wazungu na mali zao akageuka shujaa wa kimataifa.
2.Kigezo kingine ni kukaa madarakani huku ukiendeleza nchi yako na kusaidia wengine. Sote tunajua alichofanya Mandela, kuanzia muda aliokaa madarakani na hata kile alichokifanya ili kuwakomboa raia wa Afrika ya kusini kiuchumi. Fine, hapa hatuwezi kumlaumu kulingana na mazingira ya taifa lao, mpaka leo bado kiuchumi weusi wenyeji ni bilabila. Lakini huwezi kulinganisha na Tz, pamoja na wanasiasa kutufanya vibaya, bado hali zetu si sawa na wazulu. Ninarudia, hili si la kumlaumu Mandela, ni historia yao ndiyo imewafikisha hapo. Lakini kwakuwa tunalinganisha, basi tutumie kuwatathimini wote iwe ni sababu binafsi au za nje yao.
Aidha, pamoja na sifa nyingi tunazowapa watu hawa, huwa tunakosea sana kuona ama kufikiri hawa watu walikuwa peke yao. Wengi hulalamika kuhusu Mwalimu na namna alizima nyota za watu walioshiriki kuliletea taifa uhuru na heshima. Inashangaza sana vijana tunafunzwa na kukaririshwa Mwalimu peke wakati kuna wanaharakati wengi tu, wengine mwalimu aliwakuta wakiwa washakinukisha. Hata Afrika ya kusini ni hivyohivyo, wapo wengi saaaana waliofanya pengine hata zaidi ya Nelson. Lakini hao ndiyo nyota zao ziling'aa, wakatokelezea. Ni jukumu letu sisi wachambuzi, kuyajua haya na kuweka rekodi sahihi kuliko kushambuliana mradi tu fulani awe mshindi.
Kuhusu wanaharakati na kufaidi ama kutofaidi maisha kiasi cha kusema Mwalimu alimkosea nini Mungu, kuna ukweli kabisa ukiwa mtu si wa kutamani ufahari basi maisha yako hayawezi kuwa hivyo. Pamoja na mapungufu ya Mwalimu kama hayo niliyogusia hapo juu, kwa uoni wangu, hakuwa mtu mwenye tamaa ya maisha hayo pengine mimi na wewe tunaona ni ndiyo maisha.Lakini ujue, aliwajengea watoto msingi mzuri tu, namba moja ikiwa ni elimu. Sisi tunataka mtu kama yeye afuje mali, alazimishe watoto kuwa mawaziri na wakuu wa majeshi, wamiliki midege n.k, huku hatuna vitanda vya wagonjwa, hakuna sehemu za kina mama kuzalia, watu tunakufa njaa n.k., hapo ndiyo tunaona haki inatendeka kwa watu wa kaliba hiyo. Huu si uungwana!
Asante