Nyerere Alifanya Makosa Makubwa...

He has been died for a long time now, and he has been out of power for even longer. So, hayo makosa yake yanasubiri afufuke ili yarekebishwe?

And why are you so obsessed with someone who has been out of power - and this world - that much? Kwa nini usituambie tujadili yanayofanywa leo na walio madarakani leo hii ambapo kila kukicha ni bora ya jana?
hayupo ila mawazo yake yanaishi,na ndio maana mpaka leo kila mwanasiasa hajiamini ila anamwamini yeye,ndio maana kaitwa baba wa taifa,kila mmoja anasema Laiti angekuwepo Nyerere sijui kama hiki angekubali,yaani tumemsukumia kila kitu yeye,mfano mzuri masuala ya Muungano hakuna hata mwanasiasa mmoja aliye tayari kurekebisha kasoro za muungano kisa tuu Mwalimu alisema mambo fulani juu ya muungano,sasa sijui mpaka lini hali hii?
 
Hakuna binadamu aliyekamilika!
Ni dhahiri atakuwa na mapungufu yake,lakini atakumbukwa kwa mema mengi

Atakumbukwa kwa mema mengi, na atakumbukwa kwa makosa pia. Kuna makosa ya kutokusudia ndiyo Mwalim aliyoyafanya. Viongozi wetu wa leo, wana fanya makosa ya kukusudia kwa manufaa yao wenyewe kwa kutumia Mali za wote huu ndiyo UCHUNGU mkubwa kwa Watanzania
 
Atakumbukwa kwa mema mengi, na atakumbukwa kwa makosa pia. Kuna makosa ya kutokusudia ndiyo Mwalim aliyoyafanya. Viongozi wetu wa leo, wana fanya makosa ya kukusudia kwa manufaa yao wenyewe kwa kutumia Mali za wote huu ndiyo UCHUNGU mkubwa kwa Watanzania
Hawa wa sasa wanapaswa waburuzwe mahakamani kwa makosa yao ya ufisadi.
Mda utafika tu
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi..
Kwa kweli FaizaFoxy leo hii ukimleta Mwl. Nyerere agombee uraisi dhidi ya Mwinyi, Mkapa, Kikwete au hata Magufuli, Mwl. Nyerere atapita kwa kura nyingi mno, mimi mmoja wapo wakumpigia.
Legacy zake ni nyingi kwa kweli, na tulipotupa kule madhara yake ndio haya tunayoyaona :-
  • Uuzaji na utumiaji wa madawa ya kulevya, na cha kushangaza mpaka viongozi wa vyama vyote kudaiwa kuhusika
  • Wizi, ufisadi, ubinafsi, ulafi na ufujaji wa mali za umma
  • Kupendeleana kwa sababu za kidini na za kikabila.
  • Kutokuwajibika, hata kama serikali imekusomesha na kukufikisha hapo, kusoma tu na kukosoa mikataba kwa manufaa ya umma hakuna, tumeisahau nchi, tumbo na familia zetu kwanza.
  • Kutokufuata sheria bila shuruti, zamani ilikuwa na ajabu na kwa nadra kuona bastola zatolewa nje nje au hata askari kutembea na SMG mtaani, au kupiga tu risasi.
  • Kufoji foji makaratasi na maombi yawe ya kutaka kusafiri au kutibiwa serikalini, ni kinyaa, hapa kidogo kumepunguwa.
  • Viongozi kusafiri safiri kila wakati kisingizio wamebeba bakuli la kuomba hela kwa wazungu au nchi zilizoendelea, kumbe wanakoenda wana yao.
  • Udini kushika hatamu.
  • Utakatishaji wa fedha za umma, kina mzee wa vijisenti, huyu mzee siku nyingi angekuwa ananyea debe na mali zote kufilisiwa.
  • Utajiri usiokifani na usio jibu maswali ya upatikanaji wake, kina Rostam, Lowassa na wengine wengi tu
  • Kuzorota kwa elimu, ustawi wa jamii na afya, wahusika hata hawaeleweki wanafanya nini?! Shaghalabagala..
  • ..
  • ..
Na mengi mengineo, kwa kweli huyu mzee (Mwl. Nyerere) alikuwa wa kipekee..
 
Wakati vijiji vya ujamaa vilipoanzishwa familia yangu ilikuwa mojawapo kuishi kwenye vijiji mbali mbali, baba yangu akiwa settlement officer. Nakumbuka hayo ingawaje wakati huo nilikuwa mtoto. Wana vijiji wengi walihama na kuacha mashamba yao kwa kupinga mwito huo. Wengine kwa fransration wakawa walevi. Wakulima wa pamba usukumani waliokuwa wakilima pamba na kuiuzua serikali, badala ya chama chao Nyanza cooperative wakaanza kucheleweshiwa malipo na walipolipwa, walilipwa na cheque AMBAYO wengi wao walikuwa hawana hata account, matokeo yake wengi walipoteza hundi hizo, kwaajili ya kukosa malipo, wengi walitupilia mbali kilimo wakawa walevi kwa frastration. Wazazi wakawa walevi, watoto wakaacha kuhudhulia shule, na wajinga tukawa wengi, ndiyo maana leo tuna Viongozi kama Bashite. Ujamaa ulikuwepo tangu zamani, watu walikuwa wakisaidiana kulimiana lakini kila mtu na shamba lake. China ilikuwa hivyo, na Mwalim alivutiwa na MTINDO wa China alipotembele huko. Ukiwa mgeni hauoni mabaya, wachina hawakumuonyesha maafa ya ujamaa, vijijini China watu walikuwa wakifa na njaa, lakini habari hizi Muchina alizificha zisijulikane. Wakati huo kila serikali ilitetetea MTINDO wa siasa zao. Hatuimbi kama kasuku, historia lazima ikumbushwe, ndiyo maana kila mwaka tunasherekea Uhuru.
Narudia tena, Mwalim alikuwa hana ubinafsi kabisa, alifikiri anachofanya kutawanufaisha Watanzania, Viongozi waliofuatia walikuwa na nafasi kubwa ya yakusahihisha makosa haswa kwa elimu, na kuyaendeleza mazuri, kwa ubinafsi wao wameididimiza elimu yetu, na kwa ubinafsi wao wamelitumia jina la Nyerere vibaya kwa manufaa yao. Tanzania ya leo sio ya Nyerere, pamoja na makosa aliyoyafanya, aliendelea kurekebisha mpaka hapo alipoachia madaraka. Walioshika madaraka badala yake wametugawa wakacreate matajiri wa kutupa wachache na masikini wengi wa kutupa. Pamoja na kuwa na fulsa ya kuibadilisha na kuimarisha education yetu, wameiteketeza, matokeo yake tunapata Viongozi kama Bashite. Hatujui tunaelekea wapi. Pamoja na nchi kuwa na maliasili nyingi, hatuna wa juzi wa kusisimia utajiri wetu. Kwa mufano tuambiwa kwenye macontainer Hakuna zaidi ya muchanga, mchanga huu, ni muchanga wa aina gani? miaka imepita , macontainer mengi yamepelekwa hatujuwi kama ni mchanga ama dhahabu. Umasikini wa elimu ni umasikini mbaya. Ni vigumu kuelewa kwa kuwa tumetosheka hatuna elimu na Viongozi wetu hawana haraka ya kuibadilisha, kwani ni rahisi kumutawala mtu asiye na elimu, lakini pia ni vigumu kuiendesha nchi ya watu wasiokuwa na elimu utegemee kuleta mabadiliko.
Hayo yote uliyoandika ndio madhara ya kukaririshwa na tafiti za wasomi koko watetezi wa ubebari. Lengo la kuwaweka pamoja ili huduma ya shule iwe karibu iweje hao wanafunzi wako wakose elimu? Waliochanganyikiwa walikuwa na sababu zao na si kukaa katika vijiji kwani mashamba yao waliendelea kulima kama kawaida.
 
Mbona hata alivyokuwa madarakani nchi ilifeli kama ulikuwepo nadhani uliona au unaweza kutupa mafanikio ya Nyerere kiuchumi wakati yupo madarakani.
Labda unaweza kutuambia imekuwaje Kikwete ameacha nchi imefilisika.
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kmabarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.
Katika utawala wangu kuna mambo mengi niliyafanya. Mengine ya kijinga na mengine mazuri ya kijinga acheni fuateni yale yalokuwa mazuri
 
Katika mambo yote nitamlaumu nyerere kwa kulimbikiza madaraka mengi kwa raisi kiac kwamba raisi Tanzania ni kama mungu mtu.
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kmabarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.
Kwa kiasi kikubwa naungana na wewe.
 
Katika utawala wangu kuna mambo mengi niliyafanya. Mengine ya kijinga na mengine mazuri ya kijinga acheni fuateni yale yalokuwa mazuri


Naam, tunataka tuyachambue hayo ya kijinga ili tusirudie makosa. Maana naona imefikia mpaka yale ambayo hata mwenyewe alikiri ni "ya kijinga" sisi tunayakumbatia.
 
Labda unaweza kutuambia imekuwaje Kikwete ameacha nchi imefilisika.

Si kweli, Kikwete ameacha nchi ina zaidi cubic feet trillion 15 za gas, utajiri wa ajabu.

Ameacha tuna akiba hazina kuliko wakati wowote wa kabla yake.

Ameacha nchi ina maghala ya taifa ya hifadhi ya chakula kingi kuliko wakati wowote ule wa kabla yake.

Ameacha Tanzania inatowa misaada ya chakula kwa nchi jirani.

Ameacha nchi ina barabara za lami nyingi kuliko wakati wowote ule wa kabla yake.

Ameacha nchi ina shule nyingi kuliko wakati wowote ule wa kabla yake.

Ameacha nchi ina vyuo vikuu vingi kuliko wakati wowote ule wa kabla yake.

Ameacha nchi ina pato la utalii kubwa kuliko wakati wowote ule wa kabla yake.

Ameacha nchi ina umeme mwingi kuliko wakati wowote ule wa kabla yake.

Ameacha nchi inafanya upasuaji wa moyo hapa hapa nyumbani, hakuna kabla yake.

Niendelee?
 
Kajifunze kuandika Kiingereza ndio uje nikuelewe una maanisha nini.

Huo ndio msingi uliowekwa na Nyerere. Hujuwi Kiingereza na nna uhakika hata Kiswahili hukijui.
jamaa anakiingereza cha darasa la tatu naona anatema past perfect contious tense hahahaha
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kmabarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.
Nyerere hayupo hai tena, wewe kama Mtanzania umefanya nini kurekebisha makosa ya viongozi wetu watangulizi na umeifanyia nini Tanzania???
 
kama nyerere hakuweka misingi viwanda vyote walivyouza hao unao washabikia vingejengwa?. Benki ya biashara imeuzwa kama takataka, kuna kiongozi mmoja ana meli iliyokamatwa na pembe za ndovu, na haijataifishwa, viongozi wengi wametajwa kuuza ngada, ila kwa kuwa ni ccm ya leo ili uendelee kula, jicho lako na hasira zako ni kwa Nyerere aliyefariki zaidi ya muongo uliopita,leo hii unashabikia uhuni unaofanywa na viongozi kama kuruhusu cuf A na cuf B kushiriki uchaguzi wa bunge la afrika mashariki bila kusajiriwa.
 
Nyerere hayupo hai tena, wewe kama Mtanzania umefanya nini kurekebisha makosa ya viongozi wetu watangulizi na umeifanyia nini Tanzania???

Hilo ni swali zuri sana.

Ningependa tuelewe makosa ya msingi yaliyofanyika ili tusirudie.

Binafsi nimerekebisha kwa kubadilika na kuwa bepari na kuajiri Watanzania wengine.
 
kama nyerere hakuweka misingi viwanda vyote walivyouza hao unao washabikia vingejengwa?Benki ya biashara imeuzwa kama takataka, kuna kiongozi mmoja ana meli iliyokamatwa na pembe za ndovu, na haijataifishwa, viongozi wengi wametajwa kuuza ngada, ila kwa kuwa ni ccm ya leo ili uendelee kula, jicho lako na hasira zako ni kwa Nyerere aliyefariki zaidi ya muongo uliopita,leo hii unashabikia uhuni unaofanywa na viongozi kama kuruhusu cuf A na cuf B kushiriki uchaguzi wa bunge la afrika mashariki bila kusajiriwa.

Ukiona kiwanda au benki imeuzwa ujuwe ilishindwa kujiendesha yenyewe na ilikuwa inangoja ruzuku kutoka serikalini.

Viwanda tulivyoweka na kujidai kuviendesha wenyewe wakati hatuna ujuzi lilikuwa ni kosa kubwa la kiuchumi. Tusirudie kosa hilo. Halikadhalika kwa benki.

Hayo mengine yote ni matunda ya misingi mibovu.
 
bepari ni mwizi na mnyonyaji

Ndivyo ulivyojazwa ujinga. Sikushangai.

Sasa fikiri, haohao unaosema wezi (nchi za kibepari) ndiyo tunawategemea watujazie kwa kutuchangia bajeti ya nchi yetu. Kulikoni?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom