Nunua gari kali, jenga ghorofa

Nunua gari kali, jenga ghorofa

Upambane ili iweje mkuu, ili ugundue nini? Upambane ili uwe na ghorofa na gari kali? Hayo ni matumizi mabaya ya muda mchache uliopewa kuwa hapa duniani

Huhitaji kupambana kwa ajili ya chochote, everything is already in abundance

Unapopambana kichwani unakuwa na scarcity mindset

Usimlazimishe mtoto apate A tu kwenye masomo yote darasani, hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa maisha mazuri na kupata A darasani.

Bado unahitaji ukombozi wa fikra no wonder mwanao naye ameanza kufikiri kuwa na ghorofa ndiyo kufanikiwa maishani
Mimi Kuna mambo nilikua natamani niwe nayo ,nilipokua nayo nikaona kawaida tu ,nilikuja gundua Kuna vitu Wala hatuvihitaji kihivyo zaidi ni kutaka kuwatambia wengine wasivyo navyo tu 🤔
 
Ila amini usiamini maelfu ya watu wanaamini kuwa na gari ni ishara ya mafanikio
Mkuu,mafanikio unayatafsiri wewe mwenyewe muhusika na sio kusubiri kutafsiriwa na watu wengine,

Mafanikio ni kutimiza malengo uliyojiwekea,mfano ukiwa na Baiskeli ila ukawa una malengo ya kuja kununua Pikipiki,na ukainunua hiyo Pikipiki,basi hayo ni mafanikio kwako,umepiga hatua na umefanikisha lengo lako,

Jambo lolote ukiliwekea mikakati,plani na juhudi kisha ukalitimiza,basi hayo ni mafanikio kwako,

Tusisubiri maisha yetu kutafsiriwa na watu wengine.

Love the life you live
Live the life you love.
 
Mimi Kuna mambo nilikua natamani niwe nayo ,nilipokua nayo nikaona kawaida tu ,nilikuja gundua Kuna vitu Wala hatuvihitaji kihivyo zaidi ni kutaka kuwatambia wengine wasivyo navyo tu 🤔
Upo sahihi kabisa

And you don't need to fight for anything. Everything is already there.
 
Upambane ili iweje mkuu, ili ugundue nini? Upambane ili uwe na ghorofa na gari kali? Hayo ni matumizi mabaya ya muda mchache uliopewa kuwa hapa duniani

Huhitaji kupambana kwa ajili ya chochote, everything is already in abundance

Unapopambana kichwani unakuwa na scarcity mindset

Usimlazimishe mtoto apate A tu kwenye masomo yote darasani, hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa maisha mazuri na kupata A darasani.

Bado unahitaji ukombozi wa fikra no wonder mwanao naye ameanza kufikiri kuwa na ghorofa ndiyo kufanikiwa maishani
Tuko tofauti, ila nenda kamwambia mtu ambaye hajala tangu jana kwamba yuko na abundance of everything in this complex world. Umeondoa kigezo cha muda na complexity kwenye kuzungumzia abundance, ambayo Mtaalamu Amartya Sen aliita 'Opulence' kabisa. Ila ukijua complexity zilizopo kwenye kufanya uendelevu, utajua we have limited resources ambazo zinahitaji fikra.

Hayo mambo ya maisha na kufanya vizuri darasani, I wont argue hapa, ila nitakuambia tu takwimu zimeshaonesha popote kwenye degrees nyingi kunakuwa na maisha mazuri relative na kusikokuwa na elimu. So ukikomaa na extreme cases utaona hivyo, ila unajua medium income (hata avarage income) ya waliofanya vizuri darasani nitofauti na medium and mean income ya wasiokuwa wazuri darasani. Sasa ukibaki na exceptional cases na kutaka kila mtu a-rely on just chances, nitawaza sana. i.e leo Tz unamzungumzia tajiri mkubwa utakuta kasoma Havard au Stanford, unadhani unaweza kufika huko bila kuwa na marks nzuri. Utachukua kesi ya mmoja aliyefeli na kutoboa unaacha kesi za 20 waliofeli ambao hawakufika sehemu.

Anyaway, namalizia na hii "Be What you are and be what is at its the best"
 
Ila amini usiamini maelfu ya watu wanaamini kuwa na gari ni ishara ya mafanikio
Kwa usafiri wa bongo jamani kua na gari ni mafanikio, hivi kuna mtu yeyote mwenye uwezo wa kumiliki gari atathubutu kugombania gari za mbagala/kariakoo asubuhi na jioni deilee 🤣
Any ways jana ilikua harusi ya mtoto wa gsm nasikia wamefanya kufuru hapo daslam!
 
Mwisho wa siku atakuambia mnunue sayari yenu.
Hayo ni maneno ya mwanangu, akitaka ninunue gari kali, means hajaridhika na nilililonalo. Matokeo ya kidato cha pili yametoka na amefaulu kidogo nikaona nimtembeze mjini kuangalia vitu mbali mbali.

Mtoto wangu akataka tuende Mlimani City, kama mnavyojua jana pale Mlimani kulikuwa na watu wazito wana sherehe. Basi nikazurura nae madukani, tulivyotoka nikasema twende upande wa sherehe (tupite karibu na ukumbi kwenda kwenye lile duka lingine la wachina kula upande wa pili). Basi nikapita na mwanangu pale, nje kulikuwa na askari kibao wakiona gari halihusiki wanakuelekeza kupita kwa haraka. Nikawaza kunanini hapa? Maana ukumbi ulipambwa hadi nje.

Mwanangu akaona magari makali yamepaki nje, akaniambia "enhee kama hili". Nikasema sawa mwanangu tutanunua. Oya yeyote aliyefanya sherehe jana pale Mlimani City hall ni tajiri haswa maana nje pale waliweka Fountains za kutosha kwa sample. Halafu ukumbi mzima ulininginizwa taa kwa nje. Wale walinzi as if ni mkutano wa kitaifa. Gari ya bei rahisi zilizopaki nje pale ni la milioni 100 nadhani.

Anyway, nimekuwa inspired na mimi kuwa na maisha ya vile, na nitafika kwa dua za mwanangu maana amesema anaendelea kupiga dua ili mashavu yafunguke nimiliki gari kali na ghorofa. Nikasema Amen!
 
Tatizo ni ulimbukeni na lack of exposure.

Ndio maana unakuta hata wasanii wetu wakipata hela kidogo, wanaanza kushindana kujenga mijengo mikali na kununua ndinga kali.
Kujenga ni kufukia pesa chini , huu ujinga niliufanya kwa masifa tu na sikukosa mahali pa kulala , Sasa nimejengea mijusi na popo😣
 
Mkuu,mafanikio unayatafsiri wewe mwenyewe muhusika na sio kusubiri kutafsiriwa na watu wengine,

Mafanikio ni kutimiza malengo uliyojiwekea,mfano ukiwa na Baiskeli ila ukawa una malengo ya kuja kununua Pikipiki,na ukainunua hiyo Pikipiki,basi hayo ni mafanikio kwako,umepiga hatua na umefanikisha lengo lako,

Jambo lolote ukiliwekea mikakati,plani na juhudi kisha ukalitimiza,basi hayo ni mafanikio kwako,

Tusisubiri maisha yetu kutafsiriwa na watu wengine.

Love the life you live
Live the life you love.
Hilo nalifahamu mkuu na ninayaishi hayo. Mimi ni mtu wa ndani, sina muda na mali za kidunia. Zikija Sawa, zisipokuja pia Sawa. Ila siwezi kuharibu muda wangu eti niwaze niwe na ghorofa ndiyo watu waniheshimu au ndiyo nionekane nimefanikiwa.

Unachotakiwa kuelewa ni kuwa watu wenye mtizamo kama huu wangu au huo wako tunaonekana vituko mbele ya macho ya watu wengi sana hapa duniani ambao wao ni materialistic oriented
 
Mimi Kuna mambo nilikua natamani niwe nayo ,nilipokua nayo nikaona kawaida tu ,nilikuja gundua Kuna vitu Wala hatuvihitaji kihivyo zaidi ni kutaka kuwatambia wengine wasivyo navyo tu 🤔
Tatizo kuu la WAAFRIKA ni kutambiana tu. Hakuna kingine.

Ndio maana mtu akinunua gari, hata kama alikuwa haendi kanisani. Ataanza kwenda kanisani na hilo gari ili aonekane kajipata.

Au kama alikuwa anapeleka watoto shule kwa school bus, atafanya namna yoyote awapeleke shuleni na gari lake tena mpaka getini kabisa. Ili watu waone kajipata.

Kumbe ni ulimbukeni tu.
 
Kilimo na ufugaji ukiwa makini unamiliki gari yoyote unayotaka bwashee 😅
Bwashee,kwenye huu uzi naona wengi wanashindwa kujua au kutafsiri neno Mafanikio ni nini?

Tungeanza kujadili tafsiri ya neno Mafanikio,basi hata kusingekua na mabishano ya kusema kumiliki kitu fulani sio mafanikio au ni mafanikio.
 
Kilimo na ufugaji ukiwa makini unamiliki gari yoyote unayotaka bwashee 😅
Sawa bwashee ningekuwa nishawaona wakulima kibao waliotajirika, vibali vya kusafirisha mazao napo wanakwepa ndio konakona zenyewe nazozizungumzia.
 
Kujenga ni kufukia pesa chini , huu ujinga niliufanya kwa masifa tu na sikukosa mahali pa kulala , Sasa nimejengea mijusi na popo😣
Siyo mbaya weka wapangaji, vile vile kama kweli pesa unayo siyo vibaya kufanya hivyo mhimu tu usiattach hivyo vitu na mafanikio

Tunachopinga hapa ni mtu kukosa usingizi ili apate mali kwa lengo la kuonekana tu na wengine kwamba amefanikiwa
 
Bwashee,kwenye huu uzi naona wengi wanashindwa kujua au kutafsiri neno Mafanikio ni nini?

Tungeanza kujadili tafsiri ya neno Mafanikio,basi hata kusingekua na mabishano ya kusema kumiliki kitu fulani sio mafanikio au ni mafanikio.
Binafsi naona gari ni mahitaji muhimu ya binadamu ili kurahisisha shughuli zake tu kama zilivyo simu tu , sema Kuna namna kwenye jamii zetu ukiwa na kagari Cha kuzugia wanakuabudu kabisa
 
Sawa bwashee ningekuwa nishawaona wakulima kibao waliotajirika, vibali vya kusafirisha mazao napo wanakwepa ndio konakona zenyewe nazozizungumzia.
Nina mjomba wangu mmoja ni Mkulima mkubwa wa mpunga, ni tajiri wa kutisha na amepata huo utajiri kwa kilimo tu na aliishia darasa la 7
 
Bwashee,kwenye huu uzi naona wengi wanashindwa kujua au kutafsiri neno Mafanikio ni nini?

Tungeanza kujadili tafsiri ya neno Mafanikio,basi hata kusingekua na mabishano ya kusema kumiliki kitu fulani sio mafanikio au ni mafanikio.
Binafsi naona gari ni mahitaji muhimu ya binadamu ili kurahisisha shughuli zake tu kama zilivyo simu tu , sema Kuna namna kwenye jamii zetu ukiwa na kagari Cha kuzugia wanakuabudu kabisa
 
Bwashee,kwenye huu uzi naona wengi wanashindwa kujua au kutafsiri neno Mafanikio ni nini?

Tungeanza kujadili tafsiri ya neno Mafanikio,basi hata kusingekua na mabishano ya kusema kumiliki kitu fulani sio mafanikio au ni mafanikio.
Kwa mimi mafanikio ni

1. Utulivu wa nafsi
2. Kulala usingizi muda wowote ninaotaka
3. Kuwa na afya bora
4. Kuwa na amani moyoni
5. Kuridhika
 
Hilo nalifahamu mkuu na ninayaishi hayo. Mimi ni mtu wa ndani, sina muda na mali za kidunia. Zikija Sawa, zisipokuja pia Sawa. Ila siwezi kuharibu muda wangu eti niwaze niwe na ghorofa ndiyo watu waniheshimu au ndiyo nionekane nimefanikiwa.

Unachotakiwa kuelewa ni kuwa watu wenye mtizamo kama huu wangu au huo wako tunaonekana vituko mbele ya macho ya watu wengi sana hapa duniani ambao wao ni materialistic ororiented.
Kuna content creators wakubwa hapa Afrika nawa fuatiliaga sana Wodemaya na Tayo aina wanaishi maisha safi sana. Wanaweza kwenda nchi yoyote, wakati wowote.

Kwanza wao, hawana haja ya kumiliki material things. Kama nyumba, Gari, mashamba n.k

Wanasema vitu hivi, vinakufanya ukae sehemu moja kwa muda mrefu, kuvilinda na kuviangalia.

Wao hawana muda navyo. Wao ni full time travellers . Wao utajiri wao ni kusafiri duniani kila wakati.

Mcheki hata Bongo zozo. Yeye ni full time traveller. Hana haja ya kumiliki materials thing mengi.

Interview moja ya tajiri Aliko Dangote, alihojiwa akasema yeye hana hata muda wa kusafiri, muda mwingi yupo bize ku monitor makampuni yake.

Kwa hiyo suala la utajiri ni tofauti sana, kulingana na mtazamo wa mtu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom