Njombe: Wanandoa 61 waomba Talaka ndani ya siku 44

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Katavii.jpg
Imeripotiwa kuwa takribani Wanandoa 61 wamepeleka maombi ya Talaka kwa ajili kuvunja ndoa katika Baraza la Kata ya Kivavi, Halmashauri ya Mjini wa Makambako Mkoani Njombe kwa kipindi cha mwezi mmoja na wiki mbili kuanzia Novemba hadi Desemba 20, 2023.

Mwenyekiti wa Baraza la Kata ya Kivavi, Muhimba Payovela amebainisha kuwa ni kweli kwa sasa anapokea migogoro mingi ya Wanandoa kuliko ya ardhi huku akieleza kuwa sababu kubwa ya Wanandoa wengi kudaiana Talaka ni kutoaminiana na wengine kuendekeza tamaa.

"Ndoa 61 kila mmoja anataka kuvunja ndoa yake hakuna anayekuja kusema anataka kusuluhisha ndoa ila kila mmoja anasema sitaki tena ndoa," amesema Payovela.

Baadhi ya Wananchi wa Mji wa Makambako wamesema maombi ya Talaka kwa Wanandoa yanachangiwa na wengi wao kutoridhika na walichonacho na baadhi ya Wanawake kutaka usawa ndani ya ndoa zao huku wengine ikiwa ni vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa.
 
Imeripotiwa kuwa takribani Wanandoa 61 wamepeleka maombi ya Talaka kwa ajili kuvunja ndoa katika Baraza la Kata ya Kivavi, Halmashauri ya Mjini wa Makambako Mkoani Njombe kwa kipindi cha mwezi mmoja na wiki mbili kuanzia Novemba hadi Desemba 20, 2023.

Mwenyekiti wa Baraza la Kata ya Kivavi, Muhimba Payovela amebainisha kuwa ni kweli kwa sasa anapokea migogoro mingi ya Wanandoa kuliko ya ardhi huku akieleza kuwa sababu kubwa ya Wanandoa wengi kudaiana Talaka ni kutoaminiana na wengine kuendekeza tamaa.

"Ndoa 61 kila mmoja anataka kuvunja ndoa yake hakuna anayekuja kusema anataka kusuluhisha ndoa ila kila mmoja anasema sitaki tena ndoa," amesema Payovela.

Baadhi ya Wananchi wa Mji wa Makambako wamesema maombi ya Talaka kwa Wanandoa yanachangiwa na wengi wao kutoridhika na walichonacho na baadhi ya Wanawake kutaka usawa ndani ya ndoa zao huku wengine ikiwa ni vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa.
Hela za mapalachichi zinawazingua
 
Back
Top Bottom