Kwanza kabisa niseme wazi kuwa mimi binafsi sio kwamba naridhika na kila kitu kinavyotendeka katika nchi yangu hii lakini ustawi wa watanzania wote, ustawi wa nchi yangu ni bora kuliko matakwa yangu binafsi.
Nilivyokuwa mdogo niliwaza sana kufanya kazi katika taasisi kubwa za nchi hii kwa maana mafanikio tuliyaona kama yanatokana na kuajiriwa na taasisi kubwa, lakini nilivyokuwa mkubwa haikuwezekana kuweza kufanya kazi katika taasisi hizo. Nadhani kila mtanzania anaelewa kuwa kwa mazingira tuliyokuwa haikuwezekana kwa kila mtanzania kupata ajira TRA, Bandarini, Benki kuu n.k. Kwa busara zetu watanzania hatuwezi kuzusha uhasama miongoni mwetu kwa mambo kama haya ila tunaamini kadiri mda unavyosonga mambo mengi yanabarika.
kwa kifupi hakuna mtanzania yeyote ambaye anaweza kujiona kila sehemu katendewa kama alivyostahili.
Hoja yangu kubwa leo ni kwa Wanasiasa wetu.
kuna wanasiasa wanatuaminisha wanatendewa ndivyo sivyo hivyo wameamua kututafutia njaa kwa kujaribu kushawishi jumuiya za kimataifa zituwekee vikwazo n.k.
Daima mimi huwa naamini hakuna familia isiyokuwa na ugomvi au changamoto ndani, kuna familia baba ananyimwa unyumba, kuna familia kutukanana kila siku ndiyo mfumo wa maisha, kuna familia kuna baadhi ya watoto wanapendwa zaidi kuliko watoto wengine. Yote haya hayampi kibali mmoja wa wanafamilia hii kuombea njaa familia yao.
kwamba baba ukinyimwa unyumba ambao ni haki yako ya msingi na kila mmoja anaelewa haihalalishi wewe baba wa familia kwenda kuchukua shoka na kuchinja mke na watoto wa familia. baba kunyimwa unyumba haikupi kibali cha kuwalaza na kuwashindisha njaa watoto wa familia yako. Siku ukifanya hivyo watu watakushangaa na kukudharau wewe baba.
Kwamba mtoto, kama baba yako anampendelea sana ndugu yako katika kila kitu na ninyi wengine mnabezwa na kudharauliwa na kunyimwa mahitaji, je hilo linaweza kuhalalisha wewe mtoto kuendesha harakati za kuhakikisha nyumbani kwenu hampati chakula au mahitaji? huo ndiyo ujinga ambao shule zetu zilitakuwa kuuondoa kwamba hauwezi kufocus kwenye tatizo dogo na kutengeneza tatizo kubwa kama suluhu la kutatua tatizo dogo.
Wapo wanasiasa wanapita pita jumuiya za kimataifa kutafuta sapoti kwa watanzania kuwekewa vikwazo na kunyimwa misaada eti kisa wanaona wanatendewa ndivyo sivyo.
Sijui kama watanzania wanaelewa maana ya jambo hili wanalolifanya hawa wenzetu.
Jambo la kwanza tanzania kunyimwa misaada na kuwekewa vikwazo hakuwezi kuwaathiri viongozi walioko madarakani hata kidogo bali wananchi wa kawaida tulioko mitaani ndiyo tutaumia na hatua hii. Watanzania wenzangu hebu tuitazame Zimbabwe ilivyokuwa.
Wazimbabwe walikuwa na siasa za mvutano baina ya Robert Mugabe aliyekuwa raisi wa nchi hiyo na Morgani Tsvangirai aliyekuwa upinzani. Waliendesha mivutano na wapinzani wakafanya kampeni za kutokuwepo demokrasia na kadhalika na kuishawishi jumuiya ya kimataifa kuiwekea vikwazo nchi yao. Kwa kifupi vikwazo viliwekwa maana mkishaanza kupiga kelele kutafuta vikwazo huko nje watatafuta kila namna na kila sababu watawawekea vikwazo hata kama havihusiani na hoja za wapiga kelele. Leo Hii tumesahau yale yote na kila mtu anapiga kelele Zimbabwe iondolewe vikwazo baada ya kubaini mateso makubwa wanayopitia Wazimbabwe kutokana na vikwazo.
Hivi vikwazo vimebadili siasa za Zimbabwe? Siasa zimebaki vilevile watawala wameendelea kuwa watawala na watawaliwa wakaendelea kuwa wataliwa. Hivi kweli mtanzania anayepita huko kutuombea vikwazo anatutakia mema sisi watanzania wa kawaida? na je mtu kama huyo tunaweza kumuwaza hata kumpa uongozi wa kijiji kimoja tu?
Sisi Tunatamani mtu ambaye anahitaji kuwa kiongozi wetu, ikitokea akaulizwa tuwatese watanzania tukufanye tajiri au kiongozi ? na yeye ajibu Kuwatesa watanzania kwa ajili ya mimi kuwa kiongozi au tajiri ni bora utajiri na uongozi niviache na watanzania waishi salama. Lakini hapo simaanishi kuwa ukiwa kiongozi basi wakitokea wahuni wakaaanza kuwatesa watu eti ili uachie madaraka na wao waongoze basi hapo nchi huwezi kuwaachia wahuni na huko ndiko kutetea watu wako.
Tuchukue mfano mwingine, tutazame libya jinsi watu walivyoamini Gadhafi alikuwa anawatawala kidekiteta na kutafuta msaada kumuondoa ghadafi, tutazame libya ya leo na libya ya Ghadafi. Tazama nchi zote ambazo watu wake wamekimbilia nje kutafuta msaada kwa "ujinga wa demokrasia" nchi zao wamezipeleka wapi?
Watanzania ni lazima tuelewe kuna mambo ambayo ni ya nyakati na kuondoka kwake, yanaondoka na nyakati.
Huko zamani tulikuwa na tawala za kifalme ambazo mfumo wake ulikuwa wa kibaguzi kabisa kwamba kuna familia moja ndiyo imechaguliwa sijui na nani ? na hiyo familia ndiyo ilitoa wafalme wa kutawala jamii zetu na kuna familia zilikuwa "branded" familia za mikosi. wazee wetu waliishi kwa amani kwa walikubaliana na mambo hayo ambayo yalikuwa ya nyakati hizo.
Hivi tujiulize kuna mtu gani angeweza kuleta mabadiriko ya kweli katika jamii za kifalme kama angewezakupambana kukataa utawala wa kifalme? kiukweli hakuna yeyote bali ni mtu kujiona hawezi kutawaliwa na mfalme na kutafuta yeye kujiweka kuwa mfalme na wengine kutawaliwa.
Lakini wahenga walisema " time heals" sasa Leo hii tawala hizi za kifalme ziko wapi? maana yangu ni kwamba yapo mambo ni ya nyakati na yataondoka na nyakati. hata hao hao wanaojifanya kupigana nayo ukweli ni kwamba wanatafuta kukalia nyadhifa za juu tu lakini wakifika huko na wao utawala wao utakuwa vilevile. kama uamini basi jaribu kufuatilia taasisi zinazopiga kelele juu ya demokrasia na uzitazame zenyewe zinaendeshaje demokrasia hiyo hiyo ndani ya tasisi zao?
ni mambo yaleyale ya kuwapa wake zao nafasi za viti maalumu, au watu kupita bila kupingwa kugombea katika majimbo au mwenyekiti hachalenjiwi.
Kuhusu uchaguzi mkuu mimi naamini vyama vya upinzani vimeshindwa kihalali kwa maana wananchi wameviadhibu kwa kuacha sera zinazochochea maendeleo ya wananchi na kubeba hoja za kupinga serikali kila inachokifanya.
Hebu tuvitazame vya vya upinzani miaka iliyopita vilikuwaje?
vyama hivi vilijenga hoja ambazo zilikuwa zikiwapendeza wananchi. walikuwa wakihoji iweje nchi yetu iwe na ndege moja na ka nchi kama rwanda kana ndege, uwekezaji katika miundo mbinu kama ya kuzalisha umeme walisema tanzania tangu ilipowekeza miaka ya 1970 basi, reli imekufa n.k
wananchi walivipenda na kuongeza ushawishi na uwakilishi.
leo hii watu wamebadilika wanapinga mambo yote ambayo waliyapigania mda mrefu na yakawapandisha chati, unategemea nini?
Sasa tutulie tujenge nchi yetu.
swala la kwamba mimi ninataka kuwa msanii lakini ma promota wana upendeleo wana wabeba badhi ya wasanii na kuwakataa wengine na hivyo unataka kutuharibia nchi kisa eti mapromota wamekubagua hilo haliwezekani.
swala la kwamba na wewe una vigezi na haki ya kuajiriwa BOT lakini eti wameajiriwa watu kwa upendeleo hivyo unataka kuvuruga maisha ya watanzania hilo halikubaliki
yapo mambo tunaweza kuyaona hayako sawa lakini ukitazama kile unachokitafuta nacho hakiko sawa hivyo tuvumiliane tujenge nchi yetu na yeyote anayewaza kubomoa nchi yetu kwa kigezo yeye kanyimwa kitu fulani huyo tumkatae sote.
mimi nilivyokuwa mdogo wazazi wangu walimpenda sana ndugu yetu ambaye alikuwa anasoma seminari na sisi kuonekana hatuna lolote. Ninachokuhahakishia Leo hii ninavyoongea ukubwani mambo yamebadirika na wazazi hawa hawataki hata kukumbuka kama kuliwahi kuwepo na mazingira hayo.
Nyakati zimeondoa hali iliyokuwepo na ninaamini chochote ambacho watanzania wanaona hakiko sawa, waendelee kuelimishana na mambo hayo yataondoka lakini watanzania tusitafute shida kwa watanzia wenzetu
Nilivyokuwa mdogo niliwaza sana kufanya kazi katika taasisi kubwa za nchi hii kwa maana mafanikio tuliyaona kama yanatokana na kuajiriwa na taasisi kubwa, lakini nilivyokuwa mkubwa haikuwezekana kuweza kufanya kazi katika taasisi hizo. Nadhani kila mtanzania anaelewa kuwa kwa mazingira tuliyokuwa haikuwezekana kwa kila mtanzania kupata ajira TRA, Bandarini, Benki kuu n.k. Kwa busara zetu watanzania hatuwezi kuzusha uhasama miongoni mwetu kwa mambo kama haya ila tunaamini kadiri mda unavyosonga mambo mengi yanabarika.
kwa kifupi hakuna mtanzania yeyote ambaye anaweza kujiona kila sehemu katendewa kama alivyostahili.
Hoja yangu kubwa leo ni kwa Wanasiasa wetu.
kuna wanasiasa wanatuaminisha wanatendewa ndivyo sivyo hivyo wameamua kututafutia njaa kwa kujaribu kushawishi jumuiya za kimataifa zituwekee vikwazo n.k.
Daima mimi huwa naamini hakuna familia isiyokuwa na ugomvi au changamoto ndani, kuna familia baba ananyimwa unyumba, kuna familia kutukanana kila siku ndiyo mfumo wa maisha, kuna familia kuna baadhi ya watoto wanapendwa zaidi kuliko watoto wengine. Yote haya hayampi kibali mmoja wa wanafamilia hii kuombea njaa familia yao.
kwamba baba ukinyimwa unyumba ambao ni haki yako ya msingi na kila mmoja anaelewa haihalalishi wewe baba wa familia kwenda kuchukua shoka na kuchinja mke na watoto wa familia. baba kunyimwa unyumba haikupi kibali cha kuwalaza na kuwashindisha njaa watoto wa familia yako. Siku ukifanya hivyo watu watakushangaa na kukudharau wewe baba.
Kwamba mtoto, kama baba yako anampendelea sana ndugu yako katika kila kitu na ninyi wengine mnabezwa na kudharauliwa na kunyimwa mahitaji, je hilo linaweza kuhalalisha wewe mtoto kuendesha harakati za kuhakikisha nyumbani kwenu hampati chakula au mahitaji? huo ndiyo ujinga ambao shule zetu zilitakuwa kuuondoa kwamba hauwezi kufocus kwenye tatizo dogo na kutengeneza tatizo kubwa kama suluhu la kutatua tatizo dogo.
Wapo wanasiasa wanapita pita jumuiya za kimataifa kutafuta sapoti kwa watanzania kuwekewa vikwazo na kunyimwa misaada eti kisa wanaona wanatendewa ndivyo sivyo.
Sijui kama watanzania wanaelewa maana ya jambo hili wanalolifanya hawa wenzetu.
Jambo la kwanza tanzania kunyimwa misaada na kuwekewa vikwazo hakuwezi kuwaathiri viongozi walioko madarakani hata kidogo bali wananchi wa kawaida tulioko mitaani ndiyo tutaumia na hatua hii. Watanzania wenzangu hebu tuitazame Zimbabwe ilivyokuwa.
Wazimbabwe walikuwa na siasa za mvutano baina ya Robert Mugabe aliyekuwa raisi wa nchi hiyo na Morgani Tsvangirai aliyekuwa upinzani. Waliendesha mivutano na wapinzani wakafanya kampeni za kutokuwepo demokrasia na kadhalika na kuishawishi jumuiya ya kimataifa kuiwekea vikwazo nchi yao. Kwa kifupi vikwazo viliwekwa maana mkishaanza kupiga kelele kutafuta vikwazo huko nje watatafuta kila namna na kila sababu watawawekea vikwazo hata kama havihusiani na hoja za wapiga kelele. Leo Hii tumesahau yale yote na kila mtu anapiga kelele Zimbabwe iondolewe vikwazo baada ya kubaini mateso makubwa wanayopitia Wazimbabwe kutokana na vikwazo.
Hivi vikwazo vimebadili siasa za Zimbabwe? Siasa zimebaki vilevile watawala wameendelea kuwa watawala na watawaliwa wakaendelea kuwa wataliwa. Hivi kweli mtanzania anayepita huko kutuombea vikwazo anatutakia mema sisi watanzania wa kawaida? na je mtu kama huyo tunaweza kumuwaza hata kumpa uongozi wa kijiji kimoja tu?
Sisi Tunatamani mtu ambaye anahitaji kuwa kiongozi wetu, ikitokea akaulizwa tuwatese watanzania tukufanye tajiri au kiongozi ? na yeye ajibu Kuwatesa watanzania kwa ajili ya mimi kuwa kiongozi au tajiri ni bora utajiri na uongozi niviache na watanzania waishi salama. Lakini hapo simaanishi kuwa ukiwa kiongozi basi wakitokea wahuni wakaaanza kuwatesa watu eti ili uachie madaraka na wao waongoze basi hapo nchi huwezi kuwaachia wahuni na huko ndiko kutetea watu wako.
Tuchukue mfano mwingine, tutazame libya jinsi watu walivyoamini Gadhafi alikuwa anawatawala kidekiteta na kutafuta msaada kumuondoa ghadafi, tutazame libya ya leo na libya ya Ghadafi. Tazama nchi zote ambazo watu wake wamekimbilia nje kutafuta msaada kwa "ujinga wa demokrasia" nchi zao wamezipeleka wapi?
Watanzania ni lazima tuelewe kuna mambo ambayo ni ya nyakati na kuondoka kwake, yanaondoka na nyakati.
Huko zamani tulikuwa na tawala za kifalme ambazo mfumo wake ulikuwa wa kibaguzi kabisa kwamba kuna familia moja ndiyo imechaguliwa sijui na nani ? na hiyo familia ndiyo ilitoa wafalme wa kutawala jamii zetu na kuna familia zilikuwa "branded" familia za mikosi. wazee wetu waliishi kwa amani kwa walikubaliana na mambo hayo ambayo yalikuwa ya nyakati hizo.
Hivi tujiulize kuna mtu gani angeweza kuleta mabadiriko ya kweli katika jamii za kifalme kama angewezakupambana kukataa utawala wa kifalme? kiukweli hakuna yeyote bali ni mtu kujiona hawezi kutawaliwa na mfalme na kutafuta yeye kujiweka kuwa mfalme na wengine kutawaliwa.
Lakini wahenga walisema " time heals" sasa Leo hii tawala hizi za kifalme ziko wapi? maana yangu ni kwamba yapo mambo ni ya nyakati na yataondoka na nyakati. hata hao hao wanaojifanya kupigana nayo ukweli ni kwamba wanatafuta kukalia nyadhifa za juu tu lakini wakifika huko na wao utawala wao utakuwa vilevile. kama uamini basi jaribu kufuatilia taasisi zinazopiga kelele juu ya demokrasia na uzitazame zenyewe zinaendeshaje demokrasia hiyo hiyo ndani ya tasisi zao?
ni mambo yaleyale ya kuwapa wake zao nafasi za viti maalumu, au watu kupita bila kupingwa kugombea katika majimbo au mwenyekiti hachalenjiwi.
Kuhusu uchaguzi mkuu mimi naamini vyama vya upinzani vimeshindwa kihalali kwa maana wananchi wameviadhibu kwa kuacha sera zinazochochea maendeleo ya wananchi na kubeba hoja za kupinga serikali kila inachokifanya.
Hebu tuvitazame vya vya upinzani miaka iliyopita vilikuwaje?
vyama hivi vilijenga hoja ambazo zilikuwa zikiwapendeza wananchi. walikuwa wakihoji iweje nchi yetu iwe na ndege moja na ka nchi kama rwanda kana ndege, uwekezaji katika miundo mbinu kama ya kuzalisha umeme walisema tanzania tangu ilipowekeza miaka ya 1970 basi, reli imekufa n.k
wananchi walivipenda na kuongeza ushawishi na uwakilishi.
leo hii watu wamebadilika wanapinga mambo yote ambayo waliyapigania mda mrefu na yakawapandisha chati, unategemea nini?
Sasa tutulie tujenge nchi yetu.
swala la kwamba mimi ninataka kuwa msanii lakini ma promota wana upendeleo wana wabeba badhi ya wasanii na kuwakataa wengine na hivyo unataka kutuharibia nchi kisa eti mapromota wamekubagua hilo haliwezekani.
swala la kwamba na wewe una vigezi na haki ya kuajiriwa BOT lakini eti wameajiriwa watu kwa upendeleo hivyo unataka kuvuruga maisha ya watanzania hilo halikubaliki
yapo mambo tunaweza kuyaona hayako sawa lakini ukitazama kile unachokitafuta nacho hakiko sawa hivyo tuvumiliane tujenge nchi yetu na yeyote anayewaza kubomoa nchi yetu kwa kigezo yeye kanyimwa kitu fulani huyo tumkatae sote.
mimi nilivyokuwa mdogo wazazi wangu walimpenda sana ndugu yetu ambaye alikuwa anasoma seminari na sisi kuonekana hatuna lolote. Ninachokuhahakishia Leo hii ninavyoongea ukubwani mambo yamebadirika na wazazi hawa hawataki hata kukumbuka kama kuliwahi kuwepo na mazingira hayo.
Nyakati zimeondoa hali iliyokuwepo na ninaamini chochote ambacho watanzania wanaona hakiko sawa, waendelee kuelimishana na mambo hayo yataondoka lakini watanzania tusitafute shida kwa watanzia wenzetu