The Knowledge Seeker
JF-Expert Member
- Apr 13, 2019
- 3,001
- 4,172
Viongozi wa Africa waache kutumia nguvu kuendesha nchi zao na watumie akili kwa maendelea ya jamii zao
Nakuhakikishia kwa tabia zenu mtateseka sana miaka mingi bila kufulahi katika mioyo yenu hadi mtakapo iheshimu nchi yenu na kumuomba mungu awaondolee ushetani ulioko mioyoni mwenu.Yule anaotoa macho kama "TAA ZA BENZI OLD MODEL" akiwa kwenye press na kujifanya anawakemea na kuwafokea wanao tufadhili misaada, ndio tumwone mhaini. Na yule aliokula € Million 27 za Covid-19.
Wanatutafutia kibinyo cha lazima kama taifa.
Sijui kwa nini corona iliwaacha nyie watu wa ibirisi,Wewe ndio mwenye moyo kama hio "Avatar" yako.
Tatizo lenu nyinyi mnadhani watanzania wote ni wajinga na wanaishi kwa siasa. Mnadhani mtapita kule na kule mkishawishi tuwekewe vikwazo tuwekewe vikwazo na sisi watanzania tuwatazame tu na turidhike kuwa tunawekewa vikwazo na tukishawekewa vikwazo tukae kuwapa nyinyi uongozi.Hili bandiko lote ni ili kutetea umwagaji wa damu na zile kura za kwenye mabeg? Ni kwa kuwa tu sina ushawishi kwa mzungu yoyote mwenye nguvu kwenye vyombo vya maamuzi. Ningekuwa na ushawishi huo, ningetaka vikwazo vianze mara moja. Usihalalishe uhuni kwa kigezo cha nchi. Kwani hao walionajisi uchaguzi ww huwezi kuwapelekea huu ujumbe, kuwa uchu wao wa madaraka ni balaa kwetu wote? Ni hivi, ule haukuwa uchaguzi bali maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Hao wazungu kama inawezekana wachukue hatua haraka sana.
Tatizo lenu nyinyi mnadhani watanzania wote ni wajinga na wanaishi kwa siasa. Mnadhani mtapita kule na kule mkishawishi tuwekewe vikwazo tuwekewe vikwazo na sisi watanzania tuwatazame tu na turidhike kuwa tunawekewa vikwazo na tukishawekewa vikwazo tukae kuwapa nyinyi uongozi.
Kama miaka ya 1960 watu walikuwa wakifanya vurugu na baadae kusema tukae mezani tuzungumze tugawane madaraka, au mpite huko na kushawishi tuwekewe vikwazo tambue mazingira ya sasa si ya miaka ya 1960 na kamwe hatutakubali ujinga.
Changamoto zinaweza kuwepo lakini kama wananchi wanawaona nyinyi ni bora hakuna changamoto inayoweza kuwazuia wananchi kuwapa madaraka.
Mku Cheyo, Merma,Lipumba,Mbatia,na wenyeviti wa vyama vingine.Tunachokisema "dhana ya kutengeneza kura" ni dhana ambayo inajengwa na watu wachache na nimesema hiyo hailalalishi mtu yeyote kutuvuruga.
Na dhana hiyo haiwezi kuondolewa na vikwazo mnavyovitafuta ndio maana watanzania wanatakiwa kuelimishwa na kuelewa.
nikupe mfano wa vyama vya upinzani vyenyewe, chama kinaweza kuongozwa na mtu mmoja miaka nenda rudi. Siamini kwamba katika vyama hivyo hakuna watu wengine wanaofaa kuongoza katika vyama hivi bali binadamu yeyote unayempa madaraka fulani, na huyo huyo ukamwambia asimamie mchakato wa kutafuta mtu mwingine ni wazi yeye huyu anakuwa na "added" advantage.
Ndiyo maana utakuta wengi mko maofisini, sio kwa sababu demokrasia ilifanyika, mkafanya interview mkapita bali kwa sababu mlifanyiwa mpango na watu wanaowafahamu.
ndio maana unakuta mtu anakuwa mwenyekiti wa chama miaka nenda miaka rudi kwa sababu anatengeneza mazingira ya yeye kila kukifanyika uchaguzi anashinda.
Nenda kwenye nafasi za viti maalumu za vyama vya upinzani waliokuwa bungeni, wafuatilie huyu ninani na alitoka wapi kupata nafasi utaona unachokilalamikia kinatendeka kila sehemu.
sasa kwa nini msinzie kusafisha vyama vyenu ndiyo mje kusafisha nchi?
Sisi wengine sio wanasiasa na tunasema haya mnayoyalalamikia ni mambo ya nyakati yamejaa kila idara. kupata kazi lazima uunganishwe na mtu ila kuna matapeli wanatambua changamoto hii katika jamii na hawaji na suluhisho bali kutumia hiyo kutafuta madaraka.