Tambukareli
Member
- May 8, 2020
- 35
- 64
Nitawashangaa CHADEMA kama watampitisha Tundu Lissu kuwa mgombea wao wa Urais
Sababu ni hizi;
Mosi, Tundu Lissu ni mgonjwa. Baada ya matatizo yaliyompata huyu ndugu yetu kule dodoma, uwezo wake wa kujenga hoja umeporomoka kwa kiasi kikubwa. I mean, Tundu lissu wa sasa ni tofauti kabisa na Tundu lissu wa kabla ya shambulio. Hii ni ishara kwamba Tundu hayuko sawa kiafya hasa afya ya akili, hivyo anahitaji matibabu zaidi ya kisaikolojia ili kumrudisha katika hali yake ya kawaida na siyo kumpa ridhaa ya kuwa mgombea Urais.
Kama CHADEMA wanataka Lisu kuwa mgombea wao, basi mwaka huu wampumzishe apatiwe matibabu na kumaliza msongo wa mawazo alionao aje ajipime ifikapo mwaka 2025.
Pili, Tundu lissu ni dikiteta. Baadhi ya watu wachache hudhania kuwa Rais magufuri ni dikiteta. Kiukweli hudhania hivyo kimakosa au labda kwakuwa hawajawahi kukaa na Tundu lissu wakajua tabia zake.
In fact, nchi hii hakuna dikiteta kama Tundu Lissu.
Lissu ni mtu wa mabavu, asiyekubali kushindwa na mwenye kujiona bora kuliko wengine. Kielelezo kizuri ni kipindi hiki cha mchakato wa uchaguzi ndani ya chama, yeye ata kabla ya kupitishwa na chama chake tayari ameanza kuitisha harambee ya kuchangiwa pesa za kampeni kana kwamba ameshajua kuwa yeye ndie bora na atakae pitishwa. Yote haya anafanya kinyume kabisa na taratibu za chama chake na ni mwendelezo wa matumizi ya mabavu na kujiona bora kuliko wengine.
Tatu, Tundu Lissu siyo mzalendo. Lissu ni muumini mkubwa wa siasa za unyang'au na utegemezi wa mabeberu badala ya siasa za ujamaa na kujitegemea. Katika hili, Lisu anakosa sifa za uzalendo na kukubali kuwa kibaraka wa mabeberu. Kielelezo kizuri ni pale alipojitokeza hadharani bila aibu na kuanza kuwatetea mabeberu Accacia katika mikataba mibovu ya kutuibia madini yetu.
Nne, Tundu lissu hana sifa za kuwa Rais. Lissu hawezi kuwa kiongozi bora kwa sababu hana busara, hekima na staha. Mara nyingi hufanya maamuzi kwa kukurupuka na kuhemka, vile vile ni msema hovyo.
Tano, Tundu Lissu ni mtu mwenye jazba na visasi. Ukisoma kwa umakini hotuba yake ya kuomba kuteuliwa kuwania Urais ndani ya chama chake, Lisu amejipambanua kuja kupambana na mtu (JPM) na siyo kutatua kero za wanachi watanzania. Katika hili, Lissu kwenye fikra zake anaamini waliomshambulia walitumwa na serikali hivyo anataka kugombea Urais kama njia ya kulipiza kisasi. Mtu kama huyu hafai kuwa Rais
CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani naamini ninyi mna hazina ya viongozi wazuri, Chagueni mtu sahihi, mzalendo mwenye kulipenda taifa lake apeperushe bendera yenu kwenye uchaguzi huu dhidi ya Rais mtetezi, kipenzi cha wanyonge Dr. Jonh pombe Magufuri
Asalaam aleykum
Sababu ni hizi;
Mosi, Tundu Lissu ni mgonjwa. Baada ya matatizo yaliyompata huyu ndugu yetu kule dodoma, uwezo wake wa kujenga hoja umeporomoka kwa kiasi kikubwa. I mean, Tundu lissu wa sasa ni tofauti kabisa na Tundu lissu wa kabla ya shambulio. Hii ni ishara kwamba Tundu hayuko sawa kiafya hasa afya ya akili, hivyo anahitaji matibabu zaidi ya kisaikolojia ili kumrudisha katika hali yake ya kawaida na siyo kumpa ridhaa ya kuwa mgombea Urais.
Kama CHADEMA wanataka Lisu kuwa mgombea wao, basi mwaka huu wampumzishe apatiwe matibabu na kumaliza msongo wa mawazo alionao aje ajipime ifikapo mwaka 2025.
Pili, Tundu lissu ni dikiteta. Baadhi ya watu wachache hudhania kuwa Rais magufuri ni dikiteta. Kiukweli hudhania hivyo kimakosa au labda kwakuwa hawajawahi kukaa na Tundu lissu wakajua tabia zake.
In fact, nchi hii hakuna dikiteta kama Tundu Lissu.
Lissu ni mtu wa mabavu, asiyekubali kushindwa na mwenye kujiona bora kuliko wengine. Kielelezo kizuri ni kipindi hiki cha mchakato wa uchaguzi ndani ya chama, yeye ata kabla ya kupitishwa na chama chake tayari ameanza kuitisha harambee ya kuchangiwa pesa za kampeni kana kwamba ameshajua kuwa yeye ndie bora na atakae pitishwa. Yote haya anafanya kinyume kabisa na taratibu za chama chake na ni mwendelezo wa matumizi ya mabavu na kujiona bora kuliko wengine.
Tatu, Tundu Lissu siyo mzalendo. Lissu ni muumini mkubwa wa siasa za unyang'au na utegemezi wa mabeberu badala ya siasa za ujamaa na kujitegemea. Katika hili, Lisu anakosa sifa za uzalendo na kukubali kuwa kibaraka wa mabeberu. Kielelezo kizuri ni pale alipojitokeza hadharani bila aibu na kuanza kuwatetea mabeberu Accacia katika mikataba mibovu ya kutuibia madini yetu.
Nne, Tundu lissu hana sifa za kuwa Rais. Lissu hawezi kuwa kiongozi bora kwa sababu hana busara, hekima na staha. Mara nyingi hufanya maamuzi kwa kukurupuka na kuhemka, vile vile ni msema hovyo.
Tano, Tundu Lissu ni mtu mwenye jazba na visasi. Ukisoma kwa umakini hotuba yake ya kuomba kuteuliwa kuwania Urais ndani ya chama chake, Lisu amejipambanua kuja kupambana na mtu (JPM) na siyo kutatua kero za wanachi watanzania. Katika hili, Lissu kwenye fikra zake anaamini waliomshambulia walitumwa na serikali hivyo anataka kugombea Urais kama njia ya kulipiza kisasi. Mtu kama huyu hafai kuwa Rais
CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani naamini ninyi mna hazina ya viongozi wazuri, Chagueni mtu sahihi, mzalendo mwenye kulipenda taifa lake apeperushe bendera yenu kwenye uchaguzi huu dhidi ya Rais mtetezi, kipenzi cha wanyonge Dr. Jonh pombe Magufuri
Asalaam aleykum