Nitatoa zawadi ya 200,000

Nitatoa zawadi ya 200,000

ongeza dau mkuu nikusaidie kumkamata🙂🙂🙂🙂,

ila anaonekana innocent etii?mnh kweli simba mwenda pole ndie mla nyama😕
Hahaahaaaaa.......
Hata wewe wa kunifanyia hivi...
 
Uyo jamaa aliekataa kurudisha hela nae analo kosa maana kataarifiwa na yeye kakiri kuwa hela imeingia na kapewa offer ya elfu 50 lakini hakurudisha na hapatikani hewani
Asante kwa kunielewa ndugu
 
Ila usingeweka picha maana watubsk hizi wanaweka picha za ndg zao kwahyo umewahi sana kutuma picha zake mitandaoni

But pole sana kwa hilo ndivyo maisha yalivyo

Pia usimchukie maana hali ya hewa ni ngumu sana na uliekosea ni ww kwahyo kwa upande mwingine amekuweka pagumu na upande mwingine umemsababishia tamaa
 
Nenda Instagram katika zile page za umbea umbea maana wabongo wengi wanapenda umbea,Waambie hao wenye page wakutangazie pamoja na picha ya jamaa waiweke followers watamjua tu.
Asante mkuu, nitatumia ushauri wako
 
Mkuu...
Huyu jamaa nilimtumia pesa kwa bahati mbaya nikiwa nafanya malipo kwa watu kadhaa.... Sasa baada ya kuwalipa wengine wote, nikapata sim toka kwa jamaa mmoja akiulizia malipo yake. Nami nikamjibu kwamba tayari nimefanya malipo kwa watu wote, lakini nikaamua kurudi kuhakiki kama nilikua sahihi.... Toba... , nikakuta nimezituma kwa Venance Chiwalala.
Hapo nikaamua kumpigia sim na kumtaarifu kuhusu kilicho tokea king makosa kwa kumtumia pesa asio stahiki, kisha huyu jamaa akakubali na akaniahidi kuirudisha baada ya muda mchache, nami bila hiyana nikamwambia achukue 50,000 kwakua amekua muungwana.
Baada ya kuona muda unapita, ndipo nikaamua kumpigia tena na jamaa akawa amezima sim.
Hajapatikana kwenye namba ile hadi leo.
Hapo nikaamua kwenda toa taarifa police kuhusu tukio lile, na nikafungua kesi ya kuibiwa kwa njia ya mtandao.
Hapo bila kuchelewa nikaanza kufanyia kazi jambo hili na nikapata informations zake kadhaa
Sasahapo kakuibia wakati wewe mwenyewe ndoumekosea kutuma ulivyodai mwizi wa kwenye mtandao nikajua ameibia watu wengi sana ahaaa! umejuaje kama amezima cm labda huko alipo cm imemuishia chaji akijakukupigia na akakupa maelezo yanayoeleweka akakurudishia pesa zako upo tayari kumsafisha na kumlipa fidia? Mawazo yangu tu
 
Pole Sana. Nina hakika zitarudi.utampata tu
Kumpata atampata ila kurudi pesa hazitarudi maanake ukiona mpk kaamua kutopatikana kubadili na namba ya simu ujue pesa aliyopokea kaona ni kubwa sana kwake mpk akatokwa na imani. Hapo kesi tu mahakamani ndo ninachokiona.

Anyway pole sana mkuu.
 
Anatafutwa kwa kosa la wizi kwa njia ya mtandao. Pia namba alio tumia kupokelea pesa haipatikani.
Kwa mujibu wa maelezo kadhaa.... Inasemekana anaishi maeneo ya kimara Dar.
Kama nilivyo toa angalizo kwamba zawadi ya 200,000 itatolewa kwa yeyote atakae toa informations zake na exactly location anayo patikana naomba ani PM.
Nimeambatanisha picha na machache niliyo yapata kuhusu mtu huyu.
Asanteni.View attachment 492396View attachment 492397View attachment 492398

Kosa ni lako wewe. Huwezi kumuita mwizi. Siyo lazima akurudishie hizo pesa kwani hauna mkataba naye kama ilivyo kati ya benki na mteja ambao ni legal binding mteja kurudisha pesa kama benki ikitokea kuweka pesa kwenye akaunti yako kimakosa. Kwa hiyo kwa hili lililokutokea utakuwa unatumia vibaya dhana ya wizi wa kimtandao
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Sasahapo kakuibia wakati wewe mwenyewe ndoumekosea kutuma ulivyodai mwizi wa kwenye mtandao nikajua ameibia watu wengi sana ahaaa! umejuaje kama amezima cm labda huko alipo cm imemuishia chaji akijakukupigia na akakupa maelezo yanayoeleweka akakurudishia pesa zako upo tayari kumsafisha na kumlipa fidia? Mawazo yangu tu
Basi sawa kwakua haya ni mawazo yako
 
Check facebk page yake utawapata nduguze wa karibu na pengine hadi mkewe hao ndo watakuwezesha kumpata,
kama fcbk page cheki posting history yake ya insta hutakosa kuwapata marafiki zake na watu wa karibu wanaomfahamu ambao watakuwezesha kumpata
 
Kosa ni lako wewe. Huwezi kumuita mwizi. Siyo lazima akurudishie hizo pesa kwani hauna mkataba naye kama ilivyo kati ya benki na mteja ambao ni legal binding mteja kurudisha pesa kama benki ikitokea kuweka pesa kwenye akaunti yako kimakosa. Kwa hiyo kwa hili lililokutokea utakuwa unatumia vibaya dhana ya wizi wa kimtandao
Asante kwa ushauri wako pia
 
Mitandao hii kweli shida! Yaani pesa utume mwenyewe, ukosee namba, ni huruma yake tu kukubali unakuja hapa kumwita mwizi! Ipo hivi mi ningeitoa na ungepiga simu na mkwara wako wa kunipa hiyo hamsini ningekwambia nishaitoa na simu nisingezima! Hii mitandao hii yaani hapo nahisi kama mna yenu unamdhalilisha tu
 
Kumpata atampata ila kurudi pesa hazitarudi maanake ukiona mpk kaamua kutopatikana kubadili na namba ya simu ujue pesa aliyopokea kaona ni kubwa sana kwake mpk akatokwa na imani. Hapo kesi tu mahakamani ndo ninachokiona.

Anyway pole sana mkuu.
Ni afadhali
 
hahahha haya mambo bwana nilikosea nkamtumia jamaa mkwanja flan badae nkamcheki anirudushie alicho nijibu nilicheka peke yangu kwa upole alinambia

"bro nna dhiki ya kufa mtu, nkisema ntakurudishia ni uongo nisamehe sana bro."
 
Back
Top Bottom