Nitamwambia Nini M/Mungu kesho mbele zake

Nitamwambia Nini M/Mungu kesho mbele zake

Kevzy

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2026
Posts
969
Reaction score
1,695
Msio amini M/Mungu habari zenu

Moja Kwa Moja kwenye sikitiko langu hili, msaada Kwa wenye mahitaji, walemavu wa aina mbali mbali

Yaani natoka asubuhi nashindwa hata kuandaa japo TSH 500 ya kutoa sadaka barabarani na isitoshe nyumbani nimeshaacha kibaba Cha unga na mboga mlo wa siku, na kwenye pochi nna pesa ya ziada, yaani nawapita tu wenye mahitaji barabarani bila hata kuwapa hata mia mbili au tatu , aisee roho imenikereketa sana Leo, mwaka nzima huu sijatoa hata mia Kwa wenye mahitaji barabarani wanaokaa na kuomba chochote , M/Mungu naomba msamaha wako

Kibaya zaidi nawaona na nawapita na kikubwa Zaid Wana visipika vya kutangaza kuomba msaada yaani nawasikia hata wakisimama Kwa mbali, roho inaniuma sana

Naomba niweke ahadi yangu hapa jf, Mwaka kabla haujapinduka huu nitafanya jambo Kwa walemavu na wenye mahitaji wanaoomba mabarabarani,🙏 panapo majaaliwa na nikiwa na uzima, kwanza nitaanza kuandaa hizi jero jero nitoe kila siku alaf nitandaa sadaka kubwa zaidi Kwa ajili Yao, amiiina

Kwani kanisani najipindaga natoaga sadaka kubwa tu, sisemi nakosea hapana ila natakiwa nitoe na Kwa Hawa wa barabarani kwani sijui kesho yangu au sijui kwenye mgongo wangu M/Mungu ameweka nn? Na sijui kesho Yao

Na hii Kwa wote wale kama Mimi tunaowapita walemavu na wenye mahitaji barabarani, tusiwapite tuwape chenji zilizobakia

Asante
 
Msio amini M/Mungu habari zenu

Moja Kwa Moja kwenye sikitiko langu hili, msaada Kwa wenye mahitaji, walemavu wa aina mbali mbali

Yaani natoka hasubuhi nashindwa hata kuandaa hapo TSH 500 ya kutoa sadaka barabarani na isitoshe nyumbani nimeshaacha kibaba Cha unga na mboga mlo wa siku, na kwenye pochi nna pesa ya ziada, yaani nawapita tu wenye mahitaji barabarani bila hata kuwapa hata mia mbili au tatu , aisee roho imenikereketa sana Leo, mwaka nzima huu sijatoa hata mia Kwa wenye mahitaji barabarani wanaokaa na kuomba chochote , M/Mungu naomba msamaha wako

Kibaya zaidi nawaona na nawapita na kikubwa Zaid Wana visipika vya kutangaza kuomba msaada yaani nawasikia hata wakisimama Kwa mbali, roho inaniuma sana

Naomba niweke ahadi yangu hapa jf, Mwaka kabla haujaponduka huu nitafanya jambo Kwa walemavu na wenye mahitaji wanaoomba mabarabarani,🙏 panapo majaaliwa na nikiwa na uzima, kwanza nitaanza kuandaa hizi jero jero nitoe kila siku alaf nitandaa sadaka kaubwa zaidi Kwa akili Yao, amiiina

Kwani kanisani najipindaga natoaga sadaka kubwa tu, sisemi nakosea hapana ila natakiewa nitoe na Kwa Hawa wa barabarani kwani sijui kesho yangu au sijui kwenye mgongo wangu M/Mungu ameweka nn? Na sijui kesho Yao

Na hii Kwa wote wale kama Mimi tunaowapita walemavu na wenye mahitaji barabarani, tusiwapite tuwape chenji zilizobakia

Asante
Wasioamini Mungu wanahusikaje na uzi wako??
 
Siku ukikua na kujua kuwa hao wapo kazini na wana network kubwa hautakaa kuwapa hata mia
Haijalishi Mkuu, Hana miguu Wala mikono aisee , muache awe kazini tu, nitampa 500 yangu , M/Mungu angechukua mikono yangu na miguu yangu nafikiri hata mimi ningekuwa kazini tu kama wao
 
Haijalishi Mkuu, Hana miguu Wala mikono aisee , muache awe kazini tu, nitampa 500 yangu , M/Mungu angechukua mikono yangu na miguu yangu nafikiri hata mimi ningekuwa kazini tu kama wao
Upo sahihi kabisa,ukitoa sadaka kwa ajili ya kutaka radhi za Mungu haijalishi mpokeaji ataitumiaje,wewe unapata thawabu zako

Na huwezi ukawa na dhana juu ya mpokeaji labda sijui ni biashara au utapeli kwakuwa hujui ya rohoni au moyoni mwake,mwenye kujua ya siri ni Allah/God pekee,kwahiyo maadam unamuona mtu kwa muonekano wake ni muhitaji basi msaidie na Mungu atakulipa
 
Upo sahihi kabisa,ukitoa sadaka kwa ajili ya kutaka radhi za Mungu haijalishi mpokeaji ataitumiaje,wewe unapata thawabu zako

Na huwezi ukawa na dhana juu ya mpokeaji labda sijui ni biashara au utapeli kwakuwa hujui ya rohoni au moyoni mwake,mwenye kujua ya siri ni Allah/God pekee,kwahiyo maadam unamuona mtu kwa muonekano wake ni muhitaji basi msaidie na Mungu atakulipa
Nashukuru sana Mkuu 🙏
 
Kwani wewe ndio upo responsible nao?

Wewe fanya Kadiri ya uwezo na moyo wako.
Ufanye usifanye Mungu hahusiki hata kidogo.

Zaidi naona unatoa kwa maslahi yako ili ujisikie vizuri kutokana na udhaifu wa moyo wako kuwa na huruma itokanayo na doctrine ulizolishwa
 
Inawezekana tu. Kwani kuna utaratibu kwamba walio juu wote siku moja lazima wafilisike?

Huzi mentality za vijiji gani mlipo?
Inabidi ujitafakari ukiwa juu Mkuu, usiwadharau na kuwakebei waliokuwa chini Yako , unaweza usishuke chini ila usiwanyanyapae wa chini, kesho Yetu
ni fumbu
 
Kwani wewe ndio upo responsible nao?

Wewe fanya Kadiri ya uwezo na moyo wako.
Ufanye usifanye Mungu hahusiki hata kidogo.

Zaidi naona unatoa kwa maslahi yako ili ujisikie vizuri kutokana na udhaifu wa moyo wako kuwa na huruma itokanayo na doctrine ulizolishwa
Imani kila mtu ana guswa na anapoamini
 
Usitoe kizembe hiyo 500 yako barabarani wengine sio wahitaji utafirisika shauri yako, kabla haujawafikiria hao wa barabarani vipi majirani wanaokuzunguka
Ni sehemu Moja wapo, sijui nilipofanikiwa kupata zaidi, neema Gani zilinipa hivi so sitajal kama Kuna mbaya atachukua neema yangu kwakumsaidia, ninachofahamu Mimi ni ninamsaidia tu, mengine yeye afanye anavyoweza, M/Mungu ninayemuamini Yu hai
 
Ni sehemu Moja wapo, sijui nilipofanikiwa kupata zaidi, neema Gani zilinipa hivi so sitajal kama Kuna mbaya atachukua neema yangu kwakumsaidia, ninachofahamu Mimi ni ninamsaidia tu, mengine yeye afanye anavyoweza, M/Mungu ninayemuamini Yu hai
Wengine ni shetani Mkuu, dunia sio salama
 
Imani kila mtu ana guswa na anapoamini

Kuguswa hakuhusiani na Mungu.
Ni suala la mtazamo na maslahi ya mtu husika.

Mfano; unapomwona Nyati akimsaidia Swala dhidi ya Simba, huo mguso wa Nyati unasababishwa na imani kwa Mungu?

Hapo ni suala la Maslahi
 
Back
Top Bottom