mafutamingi
JF-Expert Member
- Feb 14, 2011
- 2,772
- 2,171
Tukio la kukamatwa kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Mh Freeman Mbowe na kushitakiwa kwa kosa la ugaidi limevuta hisia
za watu wengi ndani na nje ya nchi.
Suala hili limegusa pia hisia zangu hasa nikitafakari kwamba amekamatwa masaa machache tu kabla kuhudhuria kongamano la katiba.
Kwa upande mwingine ni vizuri kwamba kesi hii itaanza kusikilizwa hivi karibuni ili kila upande utoe ushahidi wake utakaoiwezesha mahakama kutoa uamuzi wake.
Wakati haya yanaendelea, nimepanga kuchapisha T-shirt kama 15,000 zitakazokuwa na maneno "TUMWOMBEE FREEMAN MBOWE"
na kugawa bure T-shirt hizo kila wilaya katika ofisi za CHADEMA.
Je, nitakuwa salama na zoezi hili hasa ukizingatia kwamba wakati wa jaribio la mauaji yaTundu Lissu watu waliovaa T-shirt kuhusu TL walikamatwa na kuwekwa mahabusu!
za watu wengi ndani na nje ya nchi.
Suala hili limegusa pia hisia zangu hasa nikitafakari kwamba amekamatwa masaa machache tu kabla kuhudhuria kongamano la katiba.
Kwa upande mwingine ni vizuri kwamba kesi hii itaanza kusikilizwa hivi karibuni ili kila upande utoe ushahidi wake utakaoiwezesha mahakama kutoa uamuzi wake.
Wakati haya yanaendelea, nimepanga kuchapisha T-shirt kama 15,000 zitakazokuwa na maneno "TUMWOMBEE FREEMAN MBOWE"
na kugawa bure T-shirt hizo kila wilaya katika ofisi za CHADEMA.
Je, nitakuwa salama na zoezi hili hasa ukizingatia kwamba wakati wa jaribio la mauaji yaTundu Lissu watu waliovaa T-shirt kuhusu TL walikamatwa na kuwekwa mahabusu!