"Nitakuona Bonge la Mwanamme......"

"Nitakuona Bonge la Mwanamme......"

mpotezeeeee kwani yuko peke yake? ndio lugha zao hizo!!! akili kumukichwa yako, atakuona bonge la mwanaume ukimtumia, akishapokea atakuona bonge la juha mpaka atakapokuhitaji tena!!
 
potezea bana lakini kama mliachana bila ugomvi then unaweza msaidia sio kwamba kuachana ndo mmekuwa maadui.
 
Kuna sister du 1 kipindi cha nyuma nilikuwa nikimpa mpa hela , kuna kipindi akawa ananilalamikia kuwa

hela ninazompa ni kidogo, nikaachana naye....

Sasa leo kanipigia ananiomba nimrushie elfu 30 ana shida sana, na akaniambia kuwa

nikimrushia hizo pesa ataniona BONGE LA MWANAMME!!

Ningeomba mnishauri, nimrushie nionekane Bonge la Mwanamme?

au nisimrushie na nionekane sio Mwanamme?

Mkuu weka picha yake hapa tuone kama analipa ......
 
kimsingi anakuona sio mwanaume mpaka umpe 30 ndio utajustify kuwa wew ni mwanaume. basi pima mwenyewe kama your manhood is justifiable by only 30,000.
 
ukiona kwenye mapenzi pesa ndo petrol ya penzi na ww ndo unatakiwa utoe kila wakati ujue ww buzi siyo mwanaume
 
hii pesa hii siku hizi ukia huna hela hujakamilika kazi si utani!!
 
Ukmrushia ata kuona mbulula walai tena...usijarbu
 
Huku mitaani kuna vituko!

Alikuwa mpenzi wako? Maskini, lkn bado alikuwa hajakuona bonge la mwanaume!
 
Sasa mtu tayari anaitwa boflo......maji ya chai kidogo tu kwishaaaa............lol
 
Mwambie akutumie kwanza elfu 60 afu utamtumia elfu 30, azawaizi achana nae
 
wenzako tunakula kwa mkopo kama kawaida,wewe unatoa laki kila wiki?hana mapenzi huyo anakuchuna tuu
 
Mkuu kwani wewe unajionaje? Hivi siku hizi uanaume haujulikani mpaka uambiwe na mtu mwinginee... duuuhh
 
usijali bro,sababu uanaume so hela bali jinsi ulivyo,uwezo wako wa kutatua matatizo,misimamo yako na mambo mengine mengi but not money (to be a man is to be strong)
 
Achana na huyo malaya, kakuona wewe ni ATM yake ndo maana anapokuwa na shida anakuja kwako! Tena ukimpa hiyo hela atakuona wewe ni BONGE LA LOFA/FARA, wanawake wenye hulka hiyo wanamwona mwanamme wa thamani pale tu anapokuwa na shida!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom