Niliingia katika mahusiano na wewe mwanamke kipindi kile na graduate, nikakupenda kwa moyo wangu wote, pamoja na kuishi katika mikoa tofauti nikawa mwaminifu kwako sikuwahi kuchepuka hata kidogo, nilijitahidi kwa moyo wangu wote kwa kadiri kulingana na uwezo wangu kudumisha pendo langu, wakati mwingine niliwadanganya wazazi naenda kwenye interview (MUNGU anisamehe) wanaponipatia nauli na fedha ya kujikimu basi nakuja kukutembelea.
Hii ilibaki kuwa siri yangu baada ya miaka mitatu changamoto ya ajira ikaendelea, pasipo kujali upendo wangu kwako ukanipiga chini baada ya kupata wa kukuoa, miezi nane mbeleni ukafunga ndoa. Haukujali ahadi nyingi na nadhiri tulizoziweka mbele za MUNGU na pia mbele za wazazi.
Niliumia saaana siwezi kusahau, Dunia nzima ilinielemea, maisha yakawa machungu kama chloroquine... Lakn siku zikasogea. Ni mwaka wa nne huu Moyo umekufa ganzi, sijawahi kabisa kuwa na hisia za mapenzi teena, Huwa namwomba MUNGU anipe moyo wa kusamehe na kusahau ili moyo uwe na amani niweze kusonga mbele nashindwa kabisaa kusamehe na kusahau...
Nakuchukua sana na kamwe sitakusamehe we mwanamke kwa ulilonitendea