Nitakuchukia for the rest of my life

Nitakuchukia for the rest of my life

ba309716d18247968720b0fe7dcabe67.jpg
 
Niliingia katika mahusiano na wewe mwanamke kipindi kile na graduate, nikakupenda kwa moyo wangu wote, pamoja na kuishi katika mikoa tofauti nikawa mwaminifu kwako sikuwahi kuchepuka hata kidogo, nilijitahidi kwa moyo wangu wote kwa kadiri kulingana na uwezo wangu kudumisha pendo langu, wakati mwingine niliwadanganya wazazi naenda kwenye interview (MUNGU anisamehe) wanaponipatia nauli na fedha ya kujikimu basi nakuja kukutembelea.

Hii ilibaki kuwa siri yangu baada ya miaka mitatu changamoto ya ajira ikaendelea, pasipo kujali upendo wangu kwako ukanipiga chini baada ya kupata wa kukuoa, miezi nane mbeleni ukafunga ndoa. Haukujali ahadi nyingi na nadhiri tulizoziweka mbele za MUNGU na pia mbele za wazazi.

Niliumia saaana siwezi kusahau, Dunia nzima ilinielemea, maisha yakawa machungu kama chloroquine... Lakn siku zikasogea. Ni mwaka wa nne huu Moyo umekufa ganzi, sijawahi kabisa kuwa na hisia za mapenzi teena, Huwa namwomba MUNGU anipe moyo wa kusamehe na kusahau ili moyo uwe na amani niweze kusonga mbele nashindwa kabisaa kusamehe na kusahau...

Nakuchukua sana na kamwe sitakusamehe we mwanamke kwa ulilonitendea
Mkuu bandiko lako linanitia hofu wanawke bilion 4 wote hata 1ankusumbua akili yako jivunie kuwa dume move on brother
 
Ingawa wote huwa tunamapungufu mbele ya Mungu, lkn najaribu kutafakari juu ya kauli yako ya kuwekeana "nadhiri" mbele ya Mungu!!
Kwa maelezo yako ulikuwa ukimtembelea mara kwa mara, basically kwa *mambo yetu* - zinaa!

Hivi mtu anayefanya zinaa nadhiri yake inakubalika kwa Mungu?

Au la useme katka miaka hiyo hamkuwahi kukutana kimwili! Na kama ni hivyo kwa generation hii ni ngumu sana msichana akuvumilie mwanaume unamwangalia tu kwa zaidi ya miaka mitatu!! Sasa kama nj hivyo, alipata mtu akampacha akakuona boya huna maana.

Take it easy uendelee na maisha!
 
Hii hali ilinitokea toka 2012 mpaka sasa nimeshindwa kusamehe kwakwel mungu nisaidie
 
Katika hii dunia, wakupendwa ni Mungu tu, mwanadam ishia kumheshim tu!
Addition Wakumpenda ni mama tu mama yeye pekee hawezi kuwa msaliti Baba mwenyewe ukikaa vibaya anakumwaga, Mpende mama tu wengine waheshimu
 
Unajiendekeza brother, kubali kuwa hutakuwa naye tena maishani na uamue kumsamehe ili maisha yaendelee kwa furaha. Mola atakusaidia kusamehe kama una imani kuwa utamsamehe.
 
Hauwezi kujifunza ktk dunia hii bila kupitia ayo mkuu.samehe na sahau.
 
Shukuru Mungu kwa kila jambo huwez juu kitu gani? Umeepushiwa, msamehe bure Omba Mungu na wewe pia utapata wako kwa imani, Pole sana kaka.
 
Teh teh teeeh!!
Unavyozidi kumchukia ndivyo unavyozidi kujiumiza na kujinyima baraka.
Tunapokosa tujifunze kushukuru pia sio tunapopata tu.
 
Story yako kama yangu kidogo japo mimi nimesamee,, niliwahi kuwa na mpenzi ambae nilimpenda sana na nilijua lazima aje kuwa mke wangu,,, nilijitoa kwake kwa kila kitu ili tu afurahi,,, sikupenda kabisa kumuona akiwa na huzuni lakini yeye alinichukulia tofauti kabisa,,, nilishawahi kwenda kigamboni kwa mguu nikitokea magomeni mapipa(nilivuka wilaya tatu kwa mguu) kwenda kumtumia mzigo wa chakula maana yeye alikuwa akisoma chuo mkoani coz nilikuwa sina nauli hata ya Costa,,,, ghafla akabadilika akaanza jeuri nikawa nikipiga simu hapokei mara anasema yupo bize yaani vurugu mwanzo mwisho,,, nilijitahidi sana kumweka sawa lakini ilishindikana mpaka akawa anajisifu kuwa yeye ni maskini jeuri daaah aisee niliumia sana lakini baadae nikaja gundua kumbe kapata mshikaji na akawaambia rafiki zake mimi na force love kwake,,, mara akaanza kumpost jamaa ake mpya kwenye mitandao ya kijamii kila siku anampost whatsupp na status za kimahaba eti" my husband love yuuu mingi mingi kwako" nilifuta namba na nikajilazimisha kumsahau japo haikuwa rahisi ila nilijikaza kiume,,,,, ikajatokea bahati mbaya nilipata suprimentary kwenye somo flani chuoni na rafiki zake wakamwambia huwezi amini alishangilia sana kwa furaha lakini mimi nilijikaza kiume tu,,, nikamsamee na kuendeleza maisha yangu,,, na mimi nikabahatika kupata mshamba mwenzangu nikampenda na yeye akanipenda,,, sasa yule nyau akaanza visa mara anitumie message za ajabu ajabu eti anadai mi bado ni wake na yule mpenzi wangu atamroga,, hakuishia hapo akaanza kuwaambia rafiki zake mimi namnyanya sana kwasababu ananipenda,, ikabidi nimpe full story beby wangu ili asijetuvuruga,,, wanawake wanapendaa kutuona tukiwa kwenye matatizo tu jiongee
 
Punguza hasira kaka,hapo unajimaliza mwenyewe alafu huyo binti huko alipo anakula bata kinoma yani.
 
Nipate alotayari kunioa na nampenda afu eti nikae kusubiri miaka inaenda kisa tumewekeana ahadi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom