Nitaendelea kutokuwa na dini

Nitaendelea kutokuwa na dini

Inayosema watu wakifa wasizikwe Na majeneza! Kumbe sababu ya ukame Na Jangwa kipindi cha Mtume! Kupelekea kutokuwepo kwa miti ambayo inngekatwa mbao!?
Ungepakoti hapo panaposema hivyo ningekuona mtu makini kwelikweli, lakini neno kwa sababu halina mantiki ni kama wale wanaosema Nguruwe ni haramu kwa sababu ana vijidudu ambavyo vina madhara kwa binadamu na kwamba hawafi kwa nyuzi joto mia moja, swali kwa wenye mawazo ya kwasababu, Je endapo itagundulika tiba ya kuwachoma sindano yenye dawa ambayo nguruwe anaondokewa na wadudu hao ndio itakuwa halali kuliwa na waislamu? Kikubwa ni utaratibu wa dini husika katika kutekeleza jambo fulani katika imani yao na si kwasababu kadha wa kadha.........Na Mwenyezimungu anajua zaidi.
 
Kupitia Quran imeeleza mambo yaliyofanyika,yanayofanyika yatakayo fanyika,ukisema sijui funguo ya zaman ifungue gar la sasa kwenye Quran hyo halipo,,Quran haiitaji Editing kuendana na mambo ya sasa,kwani yenyewe ina mambo hadi yajayo,,QURAN NI KITABU KISICHOKUWA NA SHAKA NDANI YAKE.....We baki hvyo hvyo,walikuwepo kama wewe SODOMA
 
Habari wana jamvi.
Kwanza kabisa naomba niwiwe radhi kwa nitakachozungumza hapa kama nitawakwaza baadhi ya watu, ashankum si matusi.
Pili napenda niweke wazi kuwa ninaheshimu imani ya kila mtu na mimi natumaini kila mtu ataheshimu imani na msimamo wangu.

Ninapatwa wakati mgumu sana pale ninapotaka kuzungumza kuhusu dini na mungu kwani mambo haya yanatazamwa kwa mtazamo tofauti endapo mtu atathubutu kusema hakuna mungu ama hakuna dini.
Mimi naamini mungu yupo(kama sitapata shaka ya kutokuwepo)

Lakini ninaamini pasi na shaka kwamba ideology ya dini ni propaganda na si kitu sahihi kukifuata.
Labda niweke sababu chache ambazo zimenifanya nisiamini kwa dini yeyote (Islam and Christianity to bespecific)

1.Dini zimetoka wapi?
Dini kubwa zinazodominate Tanzanian zimeletwa na wageni. Islam imetoka Asia na Christianity imetoka Europe. Lakini unadhani kabla ya wazungu na waarabu kuja tulikua sisi waafrika hatuna imani? Je hizo imani zetu zimeenda wapi? Wazungu na waarabu walizipiga vita imani zetu na kuziita primitive na wao wakaleta imani zao na dini zao "civilization" Hivi unadhani kati ya imani tulizokua nazo sisi na hizo walizoleta waarabu na wazungu zipi ni "primitive"

Ninaamini kwamba dini zilikuja na wageni kwa mission zao (ukoloni na biashara) na baada ya mishen hizo kwisha wametuachia ujinga waafrika wa kukomaa na dini wakati wao wameshaacha huo upuuzi zamani. Tujaribu kuona misa za makanisa ya ulaya zinavyokosa waumini na tulinganishe mafuriko ya waumini wa makanisa na misikiti yetu afrika.

2. Dini zote hazitaki kupokea mabadiliko

Vitabu vikubwa vya dini ni Qur'an na biblia. Lakini maandishi yaliyo kwenye vitabu hivi na matakatifu na hatuwezi kubadilisha kwa namna yoyote.
Kama vitabu hivi viliandika zaidi ya miaka 1000 iliyopita basi vilikuwa valid kwa watu wa kipindi hiko na si kwa kizazi hiki ambacho kina mabadiliko makubwa katika kila nyanja ya maisha. Na sawa nabkutunza funguo yako ya gari la zamani na kulazimisha iendeshe kila gari jipya utakalonunua.

3. Dini ni mifumo mikubwa inayowanyonya ndugu zangu masikini walioamini.
Kama umefanikiwa kwenda katika vijiji vya hapa Tanzanian basi endapo utaona jenho zuri lolote lilioezekwa kwa bati na kujenga kwa tofali na kupakwa rangi vizuri ilihali majengo yote maeneo hayo ni tope na nyasi basi dhahiri jengo hilo litakuwa kanisa ama msikiti. Ni upuuzi kuona tuna makanisa manne na miskiti minane katika kijiji chetu ilihali hatuna hata zahanati. Pesa za ujenzi wa kanisa tulichanga lakni kanisa halina hata msaada mkubwa kilunganisha na dhahanati.
Sitaki kuzungumzia mashekh, maaskofu , mapadri na maimamu ambayo wanaishi maisha ya kitakatifu na anasa ilihali mimi muumini wananikwangua mpaka jasho langu la mwisho eti namtolea bwana.

Nina mengi ya kuzungumza na ninaahidi nitatoa sababu nyingine tele zinzofanya nisiwe na dini pundi nitakapopata wasaa.
Nawasilisha
Nakubaliana na wewe isipokuwa usije kuwa unataka kuhalarisha ushoga. Mimi mwenyewe niko makini kufuatilia haya mambo ya wakoloni.
 
Nakubaliana na wewe isipokuwa usije kuwa unataka kuhalarisha ushoga. Mimi mwenyewe niko makini kufuatilia haya mambo ya wakoloni.
Siwezi kuhalalalisha ushoga. Ushoga sio mfumo wetu wa afrika na mfumo wa hao hao wazungu waliotuletea dini na ndo wanatuletea ushoga sasa.
 
Dini ya Kikristo chimbuko lake si kwa wazungu kama ulivyoeleza bali waisrael(kiyahudi) ambayo pia inamlolongo mrefu hadi tuweza kuwagusa IBRAHIM na YAKOBO!
 
Dini ya Kikristo chimbuko lake si kwa wazungu kama ulivyoeleza bali waisrael(kiyahudi) ambayo pia inamlolongo mrefu hadi tuweza kuwagusa IBRAHIM na YAKOBO!
Sikusema dini ya kikristo chimbuko lake ni kwa wazungu bali nimesema dini ya kikiristo imeletwa hapa nchini na wazungu.
Asante
 
qur an tukufu inaendana na mabadiliko ya dunia na utandawazi.kwahiyo haina hajanya kufanyiwa marekebisho

Very True,
QURAN SAYS"jesus gave life to dead people" jesus went to heaven;he is still alive; and he will come again
 
  • Thanks
Reactions: PNC
kuna mikanganyiko miki katika hizi nini. ushahidi ni kuibuka kwa madhehebu yanayopingana katika dini moja. siku zinavyozidi mikanganyiko nayo inazidi. haya ndiyo yanayowafanya baadhi ya watu kufikiri upya kuhu dini hizi.
 
Kupitia Quran imeeleza mambo yaliyofanyika,yanayofanyika yatakayo fanyika,ukisema sijui funguo ya zaman ifungue gar la sasa kwenye Quran hyo halipo,,Quran haiitaji Editing kuendana na mambo ya sasa,kwani yenyewe ina mambo hadi yajayo,,QURAN NI KITABU KISICHOKUWA NA SHAKA NDANI YAKE.....We baki hvyo hvyo,walikuwepo kama wewe SODOMA
Sodoma ilikuwajekuwaje na je? Hyo sodoma ipo kwenye Biblia au Quran
 
Kutokuwa na dini ni dini pia.
Hakuna mtu asiyekuwa na dini duniani.

Hata hivyo sioni sababu ya kuwa na negative attitude kuhusu imani za wengine. Kwa Tanzania kila mtu anayo haki ya kuabudu dini yoyote popote ilimradi asivunje sheria za nchi wala kuwanyima wengine haki zao.
 
Hajasema hakuna mungu ,amesema anajua mungu yupo na hana mashaka na hilo,ndugu yangu hata mimi nina mawazo kama yako sina dini na sipendi hata kuzisikia.wanaosoma vitabu wengine na wanaotenda matendo yaliyomo ndani wengine.ni hivi hakuna watu wenye roho mbaya kama watu wanaojifanya wa dinidini ni wagumu kusaidia wengine.lakini hawa watu wasiojifanya wadini wanahuruma sana na wanasaidia yaani mambo ni ni kinyume,siamini katika dini naamini katika mungu,wewe mungu mmoja dini kibaaaaaa0
 
Kasema Mtume (s.a.w) “Anamwijia mmoja wenu shetani katika sala, basi anapuliza (anampuliza) katika matako yake, basi yule mtu inamwijia fikiria ya kuwa umemtoka upepo (kajamba) nae haukumtoka, basi akiona hali hiyo asiondoke kwenye sala mpaka asikie sauti ya kumtoka huo upepo au anuse harufu yake”. (KITABU CHA MKWELI MWAMIU, JUZUU YA 1 -2 HADITHI NA. 74, UK 42)
Duh mtume katisha
 
Hajasema hakuna mungu ,amesema anajua mungu yupo na hana mashaka na hilo,ndugu yangu hata mimi nina mawazo kama yako sina dini na sipendi hata kuzisikia.wanaosoma vitabu wengine na wanaotenda matendo yaliyomo ndani wengine.ni hivi hakuna watu wenye roho mbaya kama watu wanaojifanya wa dinidini ni wagumu kusaidia wengine.lakini hawa watu wasiojifanya wadini wanahuruma sana na wanasaidia yaani mambo ni ni kinyume,siamini katika dini naamini katika mungu,wewe mungu mmoja dini kibaaaaaa0
Sina hata cha ku comment maana umeongea fact tupu. Unajua watu ambao wameingia katika dini wanakuwa blind folded hata ufanye nini hawawezi kuuona ukweli na hivyo ndivyo mafunzo ya dini nyingi yanavyowatengeneza ili wasije wakastuka. Yaani utakapojidai kutaka kujua undani tu unaambia unakufuru na ndo inakuwa full stop yako. Hahaha dini bwana!
 
we muache tu ndugu zake wanamsikilizia tu, akifa utawaona nduguze wanavyohangaika kwa mashekhe/maaskofu ili azikwe kidini huyo, dini ni raha sana.
Ndugu zetu wahadzabhe ambao hawajui msikiti ama kanisa mbona wanaishi maisha yao ya furaha kuzidi sisi. Mbona wao wakifa hawamuhitaji sheikh wala padri kwani wanapungukiwa na nn?
 
At first Africans had their direction but with the coming of foreigners the direction was changed. Africans no longer knew where they were leading to. since then they have lost everything and things have fallen apart. they have been slaves of every thing in their own land.
 
Kupitia Quran imeeleza mambo yaliyofanyika,yanayofanyika yatakayo fanyika,ukisema sijui funguo ya zaman ifungue gar la sasa kwenye Quran hyo halipo,,Quran haiitaji Editing kuendana na mambo ya sasa,kwani yenyewe ina mambo hadi yajayo,,QURAN NI KITABU KISICHOKUWA NA SHAKA NDANI YAKE.....We baki hvyo hvyo,walikuwepo kama wewe SODOMA
Sitaki kufikia hatua nikazungumza na nikaonekana nakashifu imani za watu wengine kwa sababu mm naheshimu sana imani zote. Lakini ww inakuingia akilini eti yameandika yaliyomo na yatakayokuja ktk Qur'an! Si dhihaka ila unawwza kuniambia kama ktk Qur'an iko aya inayosema watu watawasiluana kupitia internent? Je kuna hadithi mtume aepanda tren ya umeme ama ndege! Haya mambo huwezi kuyakuta kabisa ila unaweza kuona ngamia, jahazi punda nk kwa sababu zama hizi ndo vitu vilivyokuwepo. Sasa Qur'an nzima tunaambia mara ngamia mara punda wakati kizazi chetu cha treni za umeme huyo ngamia tunamuona zoo tu na wewe bado unaamini kuwa kwa kitabu hiki faded uongoze maisha yako ya sasa. Tafakari
 
Watu wanapiga hela na wanamchezea mungu ,mimi niaendelea kuamini mungu yupo nitatenda mema maana upendo ni muhimu hapa duniani.ila dini mtanisameee wenzangu
 
Ndugu zetu wahadzabhe ambao hawajui msikiti ama kanisa mbona wanaishi maisha yao ya furaha kuzidi sisi. Mbona wao wakifa hawamuhitaji sheikh wala padri kwani wanapungukiwa na nn?
Umetumia kigezo gani cha kuwa wanafuraha kuliko nyie? hilo neno sisi ulilotumia mimi humo simo kwani mimi naamini uwepo wa dini, na nani ka kuambia kuwa Wahadzabe hawana dini?Nina wasiwasi maana ya dini huenda ukawa huijui.
 
Umetumia kigezo gani cha kuwa wanafuraha kuliko nyie? hilo neno sisi ulilotumia mimi humo simo kwani mimi naamini uwepo wa dini, na nani ka kuambia kuwa Wahadzabe hawana dini?Nina wasiwasi maana ya dini huenda ukawa huijui.
Hebu soma vizuri comment yangu halafu highlight sehemu ambayo nimesema wahadzabe hawana dini. Nadhani umenicot vibaya.
 
Back
Top Bottom