Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Ndg kwa uandishi wako unaonekana ni mtaalamu wa fani ya Afya.
Nakushauri Kama Kuna mass na pia ni painful sio dalili nzuri.
Je Kuna discharge?
Je kuna ulcer
Je kuna lymphnode enlargement kwapani,au shingoni?

Ukiwa na moja au zaidi ya mambo hayo niliyouliza fanya hima kwenda Hospitali kwa uchunguzi zaidi.
But chief most of the malignant lesions huwa ni painless unless ikiwa kwny benign stage...lakn pia uvimbe kwenye matiti ambao unaambatna na discharge could posibbly be breast abscess unless proven otherwise though inawz pia kuwa breast CA...nafkria hvo chief wangu
 
Uzi mzuri sana huu. Tukienda hospital kupima malaria au maambukizi ya virusi vya UKIMWI huwa wanatuchoma kidoleni na tusindano ili kupata damu kwa ajili ya vipimo. Je kwa kutumia ile damu ya kidoleni unaweza Pima group lako la damu? Je kwa kutumia damu hiyo ya kidoleni unaweza pima kujua una damu kiasi gani mwilini mwako?
 
Asante daktari kwa moyo wa kutaka kutusaidia!!

Mama yangu Anasumbuliwa na tatzo la bawasiri, mwaka 2019 alienda hospital akafanyiwa matibabu (vilikatwa) lakini baada ya mda tatzo lilirudi tena, mpka sasa mama anasumbuka sanaaaaa.

Ametibiwa kwa kienyeji lakini bado hajapona, naomba msaada wa kutibu hili tatzo!!
 
Habar Doctor, kuna mdogo wangu akinywa maziwa tumbo linapata gesi siku nzima na kuharisha juu. Sababu ni nin?
Ana miaka 25 tu
 
Dokta nna miak 23 tatzo la chunus uson vipele vidogvdgo kw miak mitano ss nitumie nn
 
Hello guys....!!!

Mniwie radhi kwa kuchelewa kujibu maswali yenu. Nilikua kwenye msiba. Ratiba zikikaa vyema nitarajea kutoa ufafanuzi kwa maswali yaliyoulizwa.

Asanteni
 
Docta.. mtu wangu wa karibu hashiki mimba..kapimwa vipimo anaambiwa hana tatizo.
Lakini miaka sita iliyopita aliwahi kupata ujauzito unatoka ukiwa na mwezi mmoja.baadae tena ndani ya miezi sita alipata tena ukatoka ukiwa na mwezi vile vile.
Zote hizi alitolewa na docta kwa mrija kwa vile alisema ni changa sana ..hakuna hata ya kufanyiwa Dnc!
Baada ya hapo hajashika mimba tena..

Pia naomba kuuliza kipimo cha kujua kama mirija imeziba ni kipi? ana wasi wasi labda hawajawahi kumpima hicho kipimo.
 
Pureman2
Nasumbuliwa na tatizo la nguvu za kiume kwa mda mrefu sana. Nawahi kukojoa ndani ya sekunde kadhaa pamoja na uume kuwa mlegevu sana.
 
Nna tatizo la kuvimba miguu hasa joint, goti na foot na hua napata maumivu makali sana mpaka nashindwa kutembea.
Mara ya mwisho kwenda hospitali nilifanyiwa vipimo vya damu na nliambiwa Uric Acid imezidi mwilini ndo maana napata hilo tatizo.
Wakanishauri niache kula nyama ya ng'ombe na mbuzi na vitu vichachu kama mtindi,limao,ndimu n.k.
Lakini mimi sio mtumiaji wa hivyo vitu mara kwa mara hivyo sidhani kama ndio sababu ya kuwa na tatizo hili la miguu.
Je, kuna kitu kingine nje ya hivyo vyakula kinachoweza kusababisha Uric Acid kuzidi mwilini?
 
Mkuu, nahisi kuvutiwa na hyo principal or state ya "Big heart," So unaweza kuniwekea hapa nami nijifunze kitu..?
Bila kuhoji sana, hata kwa hapa tu ulipofika nikupongeze Dr. Kutumia muda wako kutoa majibu kwa wadau, sio kitu kidogo, inahitaji moyo.

Ila usihau kuwa makwazo hayana budi kuja. Kuna members humu watakuja kuharibu tu, kukejeli nk, ndio pale as a physician unabaki na ile kanuni ya "Big Heart" ili mambo yaende. Kazi njema.
 
Dr. Mimi nina maswala yafuatayo naomba msaada wako

1. Mwenzi wangu ana tatizo la kuvimba misuli kwenye vifundo vya miguu kupanda mpaka kwenye mapaja na uambatana maumivu makali sana hadi miguu kushimdwa kujikunja kwa muda zaidi wa masaa 24. Nini tiba yake

2. Pia amekuwa na tatizo la mwili kuishiwa nguvu kabisa kunakoambatana na homa Kali alipimwa akaambiwa ana wingi wa damu. Je kuwa na damu nyingi ni tatizo na nini tiba yake bila kutokewa damu

3. Je nini chanzo cha mimba kutoka ktk vipindi tofauti miezi 3, 5 na 7 mimba 3 zimetoka respectively

4. Kupima HIV kwa vipimo ulivyoeleza hapo juu na majibu kutofautiana hospitali Moja na nyingine tatizo linakuwa ni nn?

Ahsante.
 
Dokta pole na majukumu, naomba msaada.

Nasikia maumivu upande wa kulia chini ya kifua hasa ninapo inhale.
 
Hello guys....!!!

Mniwie radhi kwa kuchelewa kujibu maswali yenu. Nilikua kwenye msiba. Ratiba zikikaa vyema nitarajea kutoa ufafanuzi kwa maswali yaliyoulizwa.

Asanteni
Pole sana Dr, na Mungu akutie nguvu
Ndugu mungu akubariki sana kwa kujitolea kuusaidia uma, hakika Mungu yuko upande wako na nina amini kuna thawabu unazipata,
Mimi nipo kwenye fifties, nasumbuliwa na maumivu upande wa kushoto chini kidogo ya kitovu. Sometimes nikikaa sana kwenye kiti nahisi maumivu inabidi niebend upande wa kulia ili kuupa ahueni huu upande wa kushoto, pia ninaposafiri mf toka dar hadi singida inafika muda naienjeka kwa kulia hasa nikihisi maumivu upande huu wa kushoto, kama nimekaa, nikibend leftwards nahisi ka maumivu eneo hilo ila nikibend rightwards sina maumivu. Naomba msaada wako, eneo lenyewe ni maeneo ya kiuno, chini ya kitovu upande wa kushoto
 
Salaam JF,

Kama mtaalamu wa afya Mungu amenipa msukumo wa kukusaidia kiushauri juu ya changamoto ya kiafya inayokukabiri. Wataalamu tunaamini kutambua msingi wa tatizo ni hatua mhimu katika kulitatua. Natarajia kukusaidia wewe mwana JF na kama si wewe basi ndg yako au jamaa wako wa karibu.

Kimaadili ya kitaaluma sitakiwi kujitangaza nafanya kazi wapi ili isionekane najipigia upatu unaoweza kulenga kujinufaisha, ila ntaomba ushirikiano wako ili ku-maintain doctor- patient relationship, utakaojengwa kwa msingi wa mutual respect.

Kimsingi, mimi ni mtaalamu wa fani za afya. Ni mtumishi wa umma na ninauzoefu wa miaka isiyozidi kumi kwenye field hii. Hivyo mambo ya msingi kiutendaji na kimfumo ninayafahamu na kwa msingi huo ninao uwezo wa kukusaidia kitaalamu juu ya issue mbalimbali za kiafya japo kwa sehemu ili kufanikisha wewe au ndugu yako kuwa na afya njema na ustawi

Context ambayo nataka uitumie ni kuuliza swali la kiafya linalokusibu either kwa kutaja dalili za hali ya kiafya inayokutatiza nami nitakusaidia kujua msingi wa tatizo na kukupa options za tiba kwa muktadha wa conventional medicine yaani tiba ya kitaalamu na sio tiba asili.

Kwa kuzingatia unyeti wa suala la afya, nitakuwa huru kupokea maoni ya wataalamu wenzangu ili kuboresha na kuhakiki kile ntakachokua nakishauri ili ku-ensure safety ya watu wetu. Na kwa msingi huo ntajitahidi kushauri kile tu kinachokubarika as best practice kwenye fani yetu na si vinginevyo.

Kwa watakaojitokeza kupata msaada wangu ninaomba uvumilivu wao hata Kama nitachelewa kukupa msaada unaoutaka. Kumbuka ninashughuri zingine nyeti kwa ujenzi wa Taifa ila nimekusudia kutenga muda ili nitoe mchango wangu kwa jamii.

Idea hii nitaanza kuitekeleza kwa familia hii ya JF ila baadaye na kusudia kuipanua kwa jamii pana ya Watanzania. Hivyo wale wadau wa afya ntaomba ushirikiano wao ili kusaidiana kufikia lengo la uzi huu.

Nakukaribisha ndg yangu ili unufaike na ushauri wa kitaalamu kwa tatizo lako la kiafya yaani medical consultation




Ahsante mkuu. Nimuda wa miezi Saba saizi nasumbuliwa na tatizo ambalo silielewi tatizo lenyewe liko hivi.

Mishipa ya kwenye taya inabana Sana mpaka huwa napiga mihayo kwa tabu Sana.
Pia halii hii husababisha kichwa kuwa kizito na kuwasha kwa ndani na maumivu upande wa masikio na pia naweza kukosa balance kwa mda mchache.

Matatizo haya Yana ambatana na tatizo la kujaa gas tumboni pia nakuwa nahisi clicking sound masikio I.
 
Ndg physìcian, natumaini hujambo hebu mwaga chini hapa nutrution guide kwa diabet 2
Kaka, somo la nutrition kwa watu wenye diabetes 2 ni topic ndefu sana ambayo siwezi ieleza kwa kutumia platform hii.

Ila ni mhimu mambo yafuatayo kujulikana vyema.

Diabetes 2 utokana na either mwili kushindwa kuitambua homoni ya insulin yaan insulin resistance, au kufifia kwa uzalishwaji wa homoni hiyo, au vyote viwili. As results, sugar metabolism inakua impared .

So kwa mtu wa tatizo hili nivizuri afahamu kuwa mwili wake utakuwa na shida sana kutafuta kubalance sukari mwilini coz homoni inayofanya kazi hiyo inakuwa imepata tatizo either la kutotambuliwa au kutozalishwa.

Kwa ujumla ,hakuna tiba lishe maalumu kwa mgonjwa wa diabetes 2. Bado mgonjwa huyu anahitaji makundi yote ya lishe bora.

Ila msisitizo mkuu uko kwenye kiwango cha calories za makundi hayo ya vyakula Kama wanga, mafuta, protein, vitamins, na maji. Tatizo kubwa lipo katika jamii zetu coz hatuna mfumo wa kupima kiwango cha Nishati katika vyakula tunavyokula kila siku, so Mara nyingi tunaelekezana kupunguza portion kwa kuzingatia mazoea ya chakula tulivyokua tunakula Wakati hatujaugua.

Hivyo kati ya nutritional guide zinazoshauriwa ni Kama zifuatazo:

Punguza vyakula vyenye wanga na sukari kwa wingi
Punguza vyakula vyenye mafuta pia ili kuzibiti ongezeko la uzito
Punguza chumvi kwenye misosi tunayoitumia.
Punguza pombe au acha kabisa
Ongeza kundi la mbogamboga na matunda kwenye diet yako
Kunywa maji kwa wingi


Mambo hayo juu yaendane na mazoezi na kuzibiti ongezeko la uzito.

Pia ni vizuri guidance hii iratibiwe na kufuatiliwa na mtaalamu wa afya ili awe msaada kwa hatua zote mhimu.

Topic hii ina mengi ya kujifunza naomba niishie hapa kwa leo.
 
Ndugu mungu akubariki sana kwa kujitolea kuusaidia uma, hakika Mungu yuko upande wako na nina amini kuna thawabu unazipata,
Mimi nipo kwenye fifties, nasumbuliwa na maumivu upande wa kushoto chini kidogo ya kitovu. Sometimes nikikaa sana kwenye kiti nahisi maumivu inabidi niebend upande wa kulia ili kuupa ahueni huu upande wa kushoto, pia ninaposafiri mf toka dar hadi singida inafika muda naienjeka kwa kulia hasa nikihisi maumivu upande huu wa kushoto, kama nimekaa, nikibend leftwards nahisi ka maumivu eneo hilo ila nikibend rightwards sina maumivu. Naomba msaada wako, eneo lenyewe ni maeneo ya kiuno, chini ya kitovu upande wa kushoto
Asante kwa feedback mzuri mkuu.

Kuhusu dalili hizo ni ngumu kidogo kutambua tatizo ni lipi. Kifupi upande wa kushoto chini ya kitovu hakuna organ nyingi, labda utumbo mpana, mrija ya mkojo toka kwenye Figo ya kushoto, visceral layers au bandama iliyopanuka . Ila mtu anaweza pata na maumivu Katika maeneo hayo japo kitu kiletacho maumivu Kiko mbali toka eneo hilo yaani "referred pain", Kutokana na figure ya mtu.

Nashauri ufike hospitalini kwa detailed history, physical examination na kipimo Cha Ultrasound.

Ukiwa na informations zitokanazo na hatua hizo nilizozitaja , itarahisisha kutambua tatizo na tiba itakayokuwa guided by that check up

Nakushauri pia usiendelee kutumia dawa za maumivu kwa wingi Wakati Bado haujafahamu unatibu kitu gani.
 
Salaam JF,

Kama mtaalamu wa afya Mungu amenipa msukumo wa kukusaidia kiushauri juu ya changamoto ya kiafya inayokukabiri. Wataalamu tunaamini kutambua msingi wa tatizo ni hatua mhimu katika kulitatua. Natarajia kukusaidia wewe mwana JF na kama si wewe basi ndg yako au jamaa wako wa karibu.

Kimaadili ya kitaaluma sitakiwi kujitangaza nafanya kazi wapi ili isionekane najipigia upatu unaoweza kulenga kujinufaisha, ila ntaomba ushirikiano wako ili ku-maintain doctor- patient relationship, utakaojengwa kwa msingi wa mutual respect.

Kimsingi, mimi ni mtaalamu wa fani za afya. Ni mtumishi wa umma na ninauzoefu wa miaka isiyozidi kumi kwenye field hii. Hivyo mambo ya msingi kiutendaji na kimfumo ninayafahamu na kwa msingi huo ninao uwezo wa kukusaidia kitaalamu juu ya issue mbalimbali za kiafya japo kwa sehemu ili kufanikisha wewe au ndugu yako kuwa na afya njema na ustawi

Context ambayo nataka uitumie ni kuuliza swali la kiafya linalokusibu either kwa kutaja dalili za hali ya kiafya inayokutatiza nami nitakusaidia kujua msingi wa tatizo na kukupa options za tiba kwa muktadha wa conventional medicine yaani tiba ya kitaalamu na sio tiba asili.

Kwa kuzingatia unyeti wa suala la afya, nitakuwa huru kupokea maoni ya wataalamu wenzangu ili kuboresha na kuhakiki kile ntakachokua nakishauri ili ku-ensure safety ya watu wetu. Na kwa msingi huo ntajitahidi kushauri kile tu kinachokubarika as best practice kwenye fani yetu na si vinginevyo.

Kwa watakaojitokeza kupata msaada wangu ninaomba uvumilivu wao hata Kama nitachelewa kukupa msaada unaoutaka. Kumbuka ninashughuri zingine nyeti kwa ujenzi wa Taifa ila nimekusudia kutenga muda ili nitoe mchango wangu kwa jamii.

Idea hii nitaanza kuitekeleza kwa familia hii ya JF ila baadaye na kusudia kuipanua kwa jamii pana ya Watanzania. Hivyo wale wadau wa afya ntaomba ushirikiano wao ili kusaidiana kufikia lengo la uzi huu.

Nakukaribisha ndg yangu ili unufaike na ushauri wa kitaalamu kwa tatizo lako la kiafya yaani medical consultation.
habar mkuu naomba unisaidie kwenye kolodani zangu zina shida moja naona inapotea inakuwa ndogo sana halafu pembeni kuna kama mabonde bonde lakini haziumi na pia nikifanya mapenzi bao 2 tu shahawa hakuna, plz
 
Nina mgojwa alipata ajali kidonda kina miaka mitano hakiponi kabisa amepima sukari hana,,,msaada wako tafadhali.
 
Back
Top Bottom