Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Dokta huwa nasikia kuwa kuna baadhi ya group zadamu huwa haziendani katika kupata watoto endapo mnapokuwa mke namume au wapenzi.

Swali langu je mimi mwanaume nina group O- namwenza wangu wakike ana O+ vipi hapo kwenye kupata watoto hatuwezi Pata shida
Swali zuri sana mkuu na limekua likileta shida sana kwenye familia zetu.

Kabla sijajibu swali lako fuatilia maelezo yafuatayo.

Tatizo hili Kiko kwenye group tunaloliita kitaalamu "Rhesus factor incopatibility"

Hiyo Rhesus fotor Ni aina ya protein ipo kwenye damu zetu, ambaye anayo hiyo factor tunamuita Rhesus foctor positive (Rh+), ambaye hana anaitwa Rhesus foctor negative (Rh-).

Watu wengi wako kwenye kundi la Rh+. Na factor hii uweza kurithishwa toka kwa baba kwenda kwa mtoto.

Sasa ukiwa wewe mwaume ni Rh+ na mkeo ni Rh-, mtoto wenu atakua Rh+.

Sasa mama mjamzito ambaye ni Rh- akibeba kichanga chenye Rh+ , mwili wa mama utazalisha antibodies na kukishambulia kichanga, na hapo mimba huaribika.

Mara nyingi tatizo hili utokea kwa mimba zitakazotungwa baada ya ujauzito wa kwanza. Hapa ndo unasikiaga watu wakisema mama yule alizaa mwanae wa kwanza vizuri, ila mimba zilizofuata zote zinaharibika!! Msipoelewa tatizo mtaanza kushikana uchawi.

Kitu Cha kuzingatia ,ukiwa mjamzito ,mme na mke fikeni clinic ,mtafanyiwa uchunguzi na mtaelekezwa namna bora za kuzibiti hali hiyo.

Nadhani nimekusaidia.
 
Dokta mie huku chini kati kati ya korodani na mapaja kuna aina fulani ya ugonjwa wa ngozi, ni kama panakuwa napachimbika kwa weupe hivi,
Em nishauri ni dawa gani itakuwa na matokeo mazuri na ya haraka zaidi kwangu?
 
Uzi mzuri sana huu. Tukienda hospital kupima malaria au maambukizi ya virusi vya UKIMWI huwa wanatuchoma kidoleni na tusindano ili kupata damu kwa ajili ya vipimo. Je kwa kutumia ile damu ya kidoleni unaweza Pima group lako la damu? Je kwa kutumia damu hiyo ya kidoleni unaweza pima kujua una damu kiasi gani mwilini mwako?
Pole mkuu, utakua mwoga wa kutolewa damu sana.

Kila kipimo Cha kitaalamu kina maelekezo yake ya namna kinavyopimwa. Je unakipimaje, kiasi gani cha damu , na kiwekwe kwenye container ipi?

Kwa kuzingatia mambo hayo wataalamu watakupa maelekezo based on the type of test doctor asked you to perform.

Kwa hicho ulichouliza , wingi wa damu na blood grouping, Mara nyingi wataalamu wa maabara hupenda kutumia damu nyingi kiasi Kutokana na aina ya kipimo kilichoagizwa. Mfano unaweza tambua wingi wa damu kwa kufanya kipimo tunakiita full blood picture(FBP) au unaweza fanya Hb test tu. Kwa kipimo Cha kwanza, FBP hapa mara zote damu isiyopungua mls 3 huitajika, ila Kuna mashine ndogo, zinaweza fanya Hb test just by few drops.

Kuhusu blood typing, wataalamu wa maabara hutumia damu nyingi kiasi coz Kuna series ya tests, Kama ABO typing and Rh factor testing.

My take note: usiogope, fika kwenye eneo la huduma , wataalamu watakusaidia .
 
Asante daktari kwa moyo wa kutaka kutusaidia!!

Mama yangu Anasumbuliwa na tatzo la bawasiri, mwaka 2019 alienda hospital akafanyiwa matibabu (vilikatwa) lakini baada ya mda tatzo lilirudi tena, mpka sasa mama anasumbuka sanaaaaa.

Ametibiwa kwa kienyeji lakini bado hajapona, naomba msaada wa kutibu hili tatzo!!
Pole ndg

Tatizo la bawasili ambalo kitaalamu linajulikana Kama haemorhoids, linaweza kutibiwa na kujirudia.

Tatizo hili lina aina na madaraja yake ya ukubwa wa tatizo. Kuna haemorhoids ambazo waweza zitibu kwa dawa tu lakini zingine huitaji upasuaji.

Hivyo nashauri ,Kama hali imejirudia asipoteze muda kwa wataalamu wa tiba asili, afike Hospitali ambapo huduma za surgery zitafanyika ili wamsaidie.
 
Habar Doctor, kuna mdogo wangu akinywa maziwa tumbo linapata gesi siku nzima na kuharisha juu. Sababu ni nin?
Ana miaka 25 tu
Msaidie afike hospitalini awezwe kisikilizwa na mtaalamu kwa ukaribu. Anaweza kuwa na vidonda vya tumbo yaani, peptic ulcer disease (PUD) , au just Gastroesophageo reflux disorders (GERD)

Pengine changamoto inaweza kuwa anatumia vyakula vyenye wanga na sukari kwa sana.

Unaweza wasiliana nami kwa account nilizoziweka huko juu, tuone tunavyoweza saidiana
 
Docta.. mtu wangu wa karibu hashiki mimba..kapimwa vipimo anaambiwa hana tatizo.
Lakini miaka sita iliyopita aliwahi kupata ujauzito unatoka ukiwa na mwezi mmoja.baadae tena ndani ya miezi sita alipata tena ukatoka ukiwa na mwezi vile vile.
Zote hizi alitolewa na docta kwa mrija kwa vile alisema ni changa sana ..hakuna hata ya kufanyiwa Dnc!
Baada ya hapo hajashika mimba tena..

Pia naomba kuuliza kipimo cha kujua kama mirija imeziba ni kipi? ana wasi wasi labda hawajawahi kumpima hicho kipimo.
Tatizo la infertility nimeshalieza kwa ufupi huko juu. Jaribu kupitia mkuu unaweza pata mwanga.

Kipimo Cha kujua Kama mirija ya uzazi iko patent kinaitwa hysterosalpingography (HSG)

Ukiwa unahitaji msaada zaidi tuwasiliane mkuu
 
Pureman2
Nasumbuliwa na tatizo la nguvu za kiume kwa mda mrefu sana. Nawahi kukojoa ndani ya sekunde kadhaa pamoja na uume kuwa mlegevu sana.
Mkuu pitia huko juu nimeshajibu kuhusu tatizo hili.

Ufafanuzi zaidi tuwasiliane
 
Uzi mzuri sana huu. Tukienda hospital kupima malaria au maambukizi ya virusi vya UKIMWI huwa wanatuchoma kidoleni na tusindano ili kupata damu kwa ajili ya vipimo. Je kwa kutumia ile damu ya kidoleni unaweza Pima group lako la damu? Je kwa kutumia damu hiyo ya kidoleni unaweza pima kujua una damu kiasi gani mwilini mwako?
Jana nimetumia damu ya kidoleni kujua nina blood group O+.
 
Nna tatizo la kuvimba miguu hasa joint, goti na foot na hua napata maumivu makali sana mpaka nashindwa kutembea.
Mara ya mwisho kwenda hospitali nilifanyiwa vipimo vya damu na nliambiwa Uric Acid imezidi mwilini ndo maana napata hilo tatizo.
Wakanishauri niache kula nyama ya ng'ombe na mbuzi na vitu vichachu kama mtindi,limao,ndimu n.k.
Lakini mimi sio mtumiaji wa hivyo vitu mara kwa mara hivyo sidhani kama ndio sababu ya kuwa na tatizo hili la miguu.
Je, kuna kitu kingine nje ya hivyo vyakula kinachoweza kusababisha Uric Acid kuzidi mwilini?
Pole sana, tatizo Hilo la gout mara nyingi ni chronic.

Kuna hatua za kuzuia baadhi ya vyakula kama ulivyovitaja ,Lakini pia unahitaji kutumia dawa za gout na zile za kupunguza maumivu.

Tunaweza wasiliana pia mkuu
 
Dr. Mimi nina maswala yafuatayo naomba msaada wako

1. Mwenzi wangu ana tatizo la kuvimba misuli kwenye vifundo vya miguu kupanda mpaka kwenye mapaja na uambatana maumivu makali sana hadi miguu kushimdwa kujikunja kwa muda zaidi wa masaa 24. Nini tiba yake

2. Pia amekuwa na tatizo la mwili kuishiwa nguvu kabisa kunakoambatana na homa Kali alipimwa akaambiwa ana wingi wa damu. Je kuwa na damu nyingi ni tatizo na nini tiba yake bila kutokewa damu

3. Je nini chanzo cha mimba kutoka ktk vipindi tofauti miezi 3, 5 na 7 mimba 3 zimetoka respectively

4. Kupima HIV kwa vipimo ulivyoeleza hapo juu na majibu kutofautiana hospitali Moja na nyingine tatizo linakuwa ni nn?

Ahsante.
Mkuu wewe ni hatari, maswali mengi kweli. Sehemu nimeshajibu huko juu, please pitia comment zangu. Ila badae ntarejea kujibu mengine
 
Tatizo langu ni kama unavyoona pichani kuja vitu vimetoka sivielewielewi niliuliza humu jf nikawa nakejeliwa tu,
20191120_171741.jpg
 
Tatizo langu ni kama unavyoona pichani kuja vitu vimetoka sivielewielewi niliuliza humu jf nikawa nakejeliwa tu,
View attachment 1267583
Evilspirit una mambo wewe!!

Kabla sijaandika kitu please nipe majibu yafuatayo:
Je hizo dark spots zina muda gani?
Je viko kwenye mapaja tu au na sehemu nyingine?
Je je vilianzanje, gafla(suddenly) au gradually?
Je vinawasha' bleed, au vinaongezeka ukumbwa?

Pia je wewe ni mjamzito au unatatizo la ini au kisukari? Je Kuna dawa unazitumia kwa muda mrefu?

Hapo ndo ujue udaktari ulivyo ngumu?

Ila usijali ukinijibu hayo maswali tutapata way forward
 
Dr. Habari? Mwenzi wangu anasumbuliwa na matatizo kadhaa kama ifuatavyo:-

1. Mzunguko wa hedhi hauko sawa, inaweza pita miez had 3 hajapata na akipata inakuwa mfurulizo hadi wiki, na pia inaweza kutokea tena ndan ya siku kabla ya mwez kuisha.

2. Maumivu ya kiuno hasa wakati wa haja ndogo kunakoambatana na kutokwa na uchafu unaofanana na rangi kama brown hivi.

Ahsante
 
jibu tafadhali wakuu [emoji107][emoji116]
habar mkuu naomba unisaidie kwenye kolodani zangu zina shida moja naona inapotea inakuwa ndogo sana halafu pembeni kuna kama mabonde bonde lakini haziumi na pia nikifanya mapenzi bao 2 tu shahawa hakuna, plz
 
Evilspirit una mambo wewe!!

Kabla sijaandika kitu please nipe majibu yafuatayo:
Je hizo dark spots zina muda gani?
Je viko kwenye mapaja tu au na sehemu nyingine?
Je je vilianzanje, gafla(suddenly) au gradually?
Je vinawasha' bleed, au vinaongezeka ukumbwa?

Pia je wewe ni mjamzito au unatatizo la ini au kisukari? Je Kuna dawa unazitumia kwa muda mrefu?

Hapo ndo ujue udaktari ulivyo ngumu?

Ila usijali ukinijibu hayo maswali tutapata way forward
Da umenishangaza kuuliza kama mimi mja mzito wakati mimi ni dume daktari
Hizi zilianza 2009 na zinakua
Zipo na sehemu nyingine za mwili,pia vipo ambavyo vilitokana na kuumia na vyenyewe vinafanana na hivi vilivyotokea vyenyewe,hata hivi vilivyotokana na kuumia huwa vinakua
Hivi vinavyotokea vyenyewe huwa navyo vinakua,unakuta kinaanza kidogo kinakuawa halafu kinakuja gawanyika
Sina tatizo la ini wala kisukari na hamna dawa nayotumia kwa muda mrefu,pia huwa vinawashaga sana tu hivi vya ugonjwa na hata vile ambavyo ni kama makovu ya kuumia,mfano niliwahi choma sindano ya ndui begani vikatokea vivimbe kama hivi,niki hapa chini ni kovu la kuumia
20191120_185334.jpg

.Huu ndio mutahsari wangu DOctor
 
Doc pole na majukumu
swali langu hivi mgonjwa akiambiwa ana fungus kwenye ubongo ina uhusiano wowote na ugonjwa wa Ukimwi
pili mimi na kauvimbe kichwani km kanundu hosptilin walisema ni mafuta ila sasa ni mwaka wa pili,naomba ushauri.
ASANTE
 
Back
Top Bottom